Podcasts by Category
- 11619 - Joram Nkumbi na Vivian Joseph: Vijana wa Afrika lazima tuchangamkie fursa na kujifunza toka kwa wenzetuFri, 19 Apr 2024
- 11618 - Francesco La Camera: Ushirikiano wa kimataifa utasaidia kuhamia haraka katika nishati jadidifuFri, 19 Apr 2024
- 11617 - 19 APRILI 2024
Ushirikiano wa kimataifa utasaidia kufanikisha kuhamia katika nishati jadidifu - Francesco La Camera.
Vijana wa Afrika lazima tuchangamkie fursa na kujifunza: Joram Nkumbi na Vivian Joseph.
Lugha ya kichina imepanua fursa za ajira kwa wanafunzi wa SAUT – Tanzania.
Mashinani ni nchini Kenya kusikia jinsi ambavyo mafunzo ya ukulima endelevu na mikopo ya fedha katika mzunguko wa kijamii (Merry-go) inavyowasaidia wakulima kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
Fri, 19 Apr 2024 - 11616 - Jifunze Kiswahili: Tofauti ya maneno “Adhiri na hadhiri.”Thu, 18 Apr 2024
- 11615 - 18 APRILI 2024
- Wataalam wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa wameelezea hofu yao juu mwenendo wa mashambulizi dhidi ya shule, vyuo vikuu, waalimu na wanafunzi kwenye Ukanda wa Gaza hali ambayo wamesema ni ishara ya mpango wa uharibifu mkubwa wa mfumo wa elimu wa Palestina.Muungano wa chanjo duniani GAVI na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF wamekaribisha taarifa kwamba chanjo mpya ya matone ya kipindupindu Euvichol-S, sasa imepokelewa na shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO na inaweza kupatikana katika nchi mbalimbali duniani. Kupitishwa kwa chanjo hiyo mpya kutasaidia kuongeza usambazaji wake kwa takriban dozi milioni 50 mwaka huu ikilinganishwa na dozi milioni 38 zilizosambazwa mwaka 2023. Mkutano wa Wiki ya Uendelevu ya Umoja wa Mataifa unaendelea hapa Makao Makuu New York Marekani, leo ukijikita na mada ya miundombinu endelevu na inayoaminika ambayo Umoja wa Mataifa unasema itazisaidia nchi kuelekea kwenye maendeleo yenye miumbombinu bora, isiyo ya hatari na itakayoongeza kasi ya kufikia malengo ya maendeleo endelevu SDGs.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili, mchambuzi wetu Dkt. Josephat Gitonga, kutoka Kenya ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi kwenye kitivo cha tafsiri na ukalimani anatufafanulia tofauti ya “Adhiri; na hadhiri.”.
Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Thu, 18 Apr 2024 - 11614 - Vijana wakiwezeshwa wanaweza kuvumbua teknolojia ya kusongesha malengo ya maendeleo endelevu
Hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa kunafanyika jukwaa la vijana la Baraza la kiuchumi na kijamii ECCOSOC ambalo linatoa ukumbi wa kimataifa wa mazungumzo kati ya nchi wanachama na viongozi vijana kutoka kote ulimwenguni kujadili suluhu za changamoto zinazoathiri ustawi wa vijana. Hafla hii pia hutumika kama nafasi ya kipekee kwa vijana kushiriki maono na hatua zao ili kuharakisha utekelezaji wa Ajenda ya 2030 na SDGs ikiwemo masuala ya uvumbuzi na teknolojia. Miongoni mwa wanaohuduria jukwaa hilo kutoka Tanzania ni Vivian Joseph Afisa tabibu na mkuu wa wa kitengo cha afya akiwasilisha vijana katika jumuiya ya maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika SADC na Joramu Nkumbi mkurugenzi mtendaji wa jukwaa la Afrika la viongozi vijana kwa upande wa Tanzania. Wameketi na Flora Nducha na kumweleza walichoambulia hadi sasa katika jukwaa hilo litakalokunja jamvi kesho..
Wed, 17 Apr 2024 - 11613 - Mapigano na mizozo DR Congo yanyima wananchi manufaa ya utajiri wa nchi yao - Türk
Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu Volker Türk ambaye yuko katika ziara rasmi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC amestaajabu ni kwa vipi utajiri wa maliasili uliosheheni kwenye taifa hilo umeleta manufaa kidogo kwa wananchi wako kutokana na ghasia na mapgano. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.
Video ya Umoja wa Mataifa inaanzia Kinshasa mji mkuu wa DRC ambako Bwana Türk na aafisa mmoja wa Umoja wa Mataifa wanatazama ramani ya taifa hilo lililoko Maziwa Makuu na kisha anasema ni moja ya nchi tajiri zaidi duniani, lakini tunaona ni kwa vipi utajiri huu kwa bahati mbayá hauko kunufaisha wananchi kwa sababu ya mapigano.
Na kisha anaelezea mipango ya ziara yake ya kutathmini hali ya haki za binadamu akisemakwanza ni kukutana na watu waliofurushwa makwao kutokana na ghasia na vile vile kuonana na mamlaka husika na mashirika ya kiraia.
Baada ya hapo safari inaanza akiambatana na Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini humo, Bintou Keita, mwelekeo ni Mashariki mwa nchi jimboni Ituri. Taswira ya angani kutoka ndege hii ya Umoja wa Mataifa na kisha wanawasili. Mapokezi hapa Bunia, kutoka kwa wenyeji wao.
Moja kwa moja msafara wao wa magari unafika kwenye kambi ya wakimbizi nje kidogo ya mji wa Bunia na wanaingia ndani ambako wanawake, wanaume na watoto, wazee na vijana, nyuso zao zinaonesha matuamini kwani wahenga walinena mgeni njoo mwenyeji apone.
Mkalimani akamweleza Turk kuwa wanachosema maeneo yao yametawaliwa na waasi na hawawezi kurejea makwao.
Na ndipo Kamishna huyu Mkuu wa Haki za Binadamu baada ya kuwasikiliza wakimbizi na kuzungumza nao akatoka nje na kusema, “Nimekutana na kundi la watu ambao wamefurushwa makwao kutokana na mauaji ya kikatili na ya kutisha yaliyotekelezwa kwenye makazi yao. Na wamekuweko hapa kwa miaka minne sasa. Tamanio lao kubwa kabisa ni kuweza kurejea makwao.”
Kwa sasa kuna takribani watu milioni 1.8 waliofurushwa makwao jimboni Ituri kati ya wakimbizi wote wa ndani milioni 7.2 nchini kote DRC.
Kesho Bwana Turk atakuwa na mazungumzo na Rais President Félix Tshisekedi na maafisa wengine wa serikali, Umoja wa Mataifa, wanadiplomasia na vyama vya siasa pamoja na watetezi wa haki za binadamu na kisha atazungumza na waandishi wa habari.
Wed, 17 Apr 2024 - 11612 - 17 APRILI 2024
- Kaminshna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu Volker Türk ambaye yuko katika ziara rasmi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC amestaajabu ni kwa vipi utajiri wa maliasili uliosheheni kwenye taifa hilo umeleta manufaa kidogo kwa wananchi wako kutokana na ghasia na mapgano.Mkutano wa Ngazi ya Juu wa Kutoa ahadi kwa ajili ya ufadhili wa kukwamua hali ya Kibinadamu nchini Ethiopia uliokamilika jana mjini Geneva, Uswisi umetangaza kwamba wafadhili 20 wametangaza msaada wa kifedha wa Dola za Marekani milioni 610 angalau kuhakikisha misaada kwa miezi michache ijayo. Makala inaturejesha hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa kunakofanyika jukwaa la vijana la Baraza la kiuchumi na kijamii ECCOSOC ambalo linatoa ukumbi wa kimataifa wa mazungumzo kati ya nchi wanachama na viongozi vijana kutoka kote ulimwenguni kujadili suluhu za changamoto zinazoathiri ustawi wa vijana. Pia hutumika kama nafasi ya kipekee kwa vijana kushiriki maono na hatua zao ili kuharakisha utekelezaji wa Ajenda ya 2030 na SDGs ikiwemo masuala ya uvumbuzi na teknolojia. Miongoni mwa wanaohuduria jukwaa hilo kutoka Tanzania ni Vivian Joseph Afisa tabibu na mkuu wa wa kitengo cha afya akiwasilisha vijana katika jumuiya ya maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika SADC na Joramu Nkumbi mkurugenzi mtendaji wa jukkwaa la Afrika la viongozi vijana kwa upande wa Tanzania.Na mashinani tutakupeleka nchini Madagascar kusikia ujumbe kuhusu hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, lakini kwanza ni makala.
Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Wed, 17 Apr 2024 - 11611 - Mkutano wa ufadhili wapata msaada wa fedha wa dola milioni 610 kwa ajili ya Ethiopia
Mkutano wa Ngazi ya Juu wa Kutoa ahadi kwa ajili ya ufadhili wa kukwamua hali ya Kibinadamu nchini Ethiopia uliokamilika jana mjini Geneva, Uswisi umetangaza kwamba wafadhili 20 wametangaza msaada wa kifedha wa Dola za Marekani milioni 610 angalau kuhakikisha misaada kwa miezi michache ijayo.
Mkutano huo uliolenga kukusanya dola bilioni 1 za kimarekani kwa ajili ya miezi mitano ijayo, ulikuwa umeandaliwa kwa pamoja kati ya Umoja wa Mataifa, Serikali ya Ethiopia na Uingereza, na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa masuala ya kibinadamu.
Mara tu baada ya mkutano huo Naibu Mkuu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Kibinadamu na Masuala ya Dharura OCHA, Joyce Msuya, aliwashukuru wafadhili hao na kusema kuwa huo ni mwanzo tu na matumaini ni kuendelea na kuongeza msaada kwa mwaka mzima.
Dharura ya kibinadamu nchini Ethiopia imekuwa ikiongezeka kupitia mizunguko ya ukame na mafuriko, na migogoro. Ukosefu wa uhakika wa chakula na utapiamlo unatarajiwa kufikia kiwango cha juu kwa watu milioni 10.8 wakati wa msimu wa muwambo kati ya mwezi Julai na Septemba.
Viwango vya utapiamlo katika sehemu za Afar, Amhara, Tigray na mikoa mingine vinatia wasiwasi mkubwa na vinaendelea kuwa vibaya zaidi. Wakati huo huo, migogoro katika Tigray na mikoa mingine imeharibu maelfu ya shule, vituo vya afya, mifumo ya maji na miundombinu mingine ya jamii.
Mama huyu ambaye jina lake limehifadhiwa kwa sababu za kiusalama ni wa eneo la Afar, mashariki mwa Ethiopia ambako pia kumeathiriwa na mafuriko anapaza sauti akisema, “Ninataka kulea na kusomesha watoto wangu vizuri. Nawatakia watoto wangu mema.”
Umoja wa Mataifa na wadau wa kibinadamu wanaunga mkono mwitikio wa kitaifa wa kuongeza msaada wa kuokoa maisha kwa watu milioni 15.5, na msaada wa chakula kwa watu milioni 10.4 nchini humo Ethiopia. Kwa mwaka mzima, ili mpango huo ufanikiwe unahitaji dola za Marekani bilioni 3.24.
Wed, 17 Apr 2024 - 11610 - 16 APRILI 2024
- Leo mashirika ya Umoja wa Mataifa yameendelea kuonya juu ya vita inayoendelea kukatili maisha ya watu Gaza, na kusambaratisha miundombinu yakitaja kuwa wanawake karibu 10,000 wamepoteza Maisha tangu vita kuanza miezi sita iliyopita huku mtoto mmoja anajeruhiwa au kuuawa kila dakika 10.Jukwaa la vijana la Baraza la Kiuchumi na Kijamii la Umoja wa Mataifa ECOSOC leo limeng’oa nanga hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa New York Matrekani likiwaleta maelfu ya vijana kutoka kila kona ya Dunia. Joramu Nkumbi ni miongoni mwa washiriki wa jukwaa hilo kutoka Tanzania na anafafanua wanachokijadili mwaka huu. Shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM kwa shirikiana na mashirika mengine 48 ya kibinadamu, ya maendeleo na serikali wametoa ombi la haraka la dola milioni 112 ili kuwasaidia zaidi ya wahamiaji milioni 2.1 na jamii zinazowahifadhi. Kwa mujibu wa IOM wahamiaji na jamii hizo ni katika njia za uhamiaji za Mashariki na Kusini zkijumuisha Djibouti, Ethiopia, Somalia, Yemen, Kenya na Tanzania.Na mashinani leo tunakwenda mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC hususan jimboni Ituri ambako huko ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani, MONUSCO umechukua hatua kukabili mashambulizi kutoka waasi, mashambulizi ambayo kila uchao yanazidi kufurusha raia. Mzungumzaji wetu ni Luteni Kanali Mensah Kedagni, msemaji wa kijeshi wa MONUSCO.
Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Tue, 16 Apr 2024 - 11609 - Ni dhana potofu kudai Wamaasai wanaua Simba ili kupata mke - Alois Porokwa
Katika harakati za kupambana na mabadiliko ya tabianchi, kuna wakati jamii ambazo bado zinaishi kiasili zimekuwa zikilaumiwa kwamba zinachangia kuharibu mazingira kutokana na wao kuishi katika mazingira fulani; mathalani misitu na mbuga jambo ambalo linakanushwa na jamii hizo wakidai kwamba kimsingi wao ndio watunzaji wazuri wa mazingira kwani wanayategemea moja kwa moja kwa mustakabali wa maisha yao ya kila siku na siku zijazo. Hivi karibuni wakati wa Mkutano wa 6 wa Baraza la Mazingira la Umoja wa Mataifa UNEA 6 uliofanyika jijini Nairobi, Kenya, Afisa habari wa kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIS Kenya, Stella Vuzo alimhoji Alois Porokwa, Mkurugenzi wa shirika la NALEPPO kutoka jamii ya Wamaasai aliyesafiri kutoka Kijiji cha Emboreet, Wilaya ya Simajiro, Mkoa wa Manyara, Tanzania. Ni katika mazungumzo hayo ndipo Stella Vuzo akakumbuka kumuuliza Alois Porokwa swali hili ambalo ni dhana inayohusisha jamii ya Wamaasai kuua wanyama.
Mon, 15 Apr 2024 - 11608 - Jukwaa la Jamii za watu wa asili lafungua pazia katika makao Makuu ya Umoja wa Mataifa
Hii leo katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa hapa jijini New York Marekani, Jukwaa la Kudumu la Umoja wa Mataifa la watu wa asili limeanza rasmi na litadumu kwa muda wa wiki mbili likiwaleta pamoja zaidi ya washiriki 2000 wa jamii za asili kutoka kila pembe ya dunia kujadili masuala mbalimbali.
Hiki ni kikao cha 23 cha jukwaa hili la kudumu la watu wa jamii za asili ambao leo mkutano wa kwanza umefunguliwa rasmi ukihudhuriwa na viongozi wa ngazi za juu wa Umoja wa Mataifa akiwemo Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Balozi Dennis Francis.
Majadiliano ya wiki mbili za mkutano huu yataongozwa na dhima ya kuangazia haki za watu wa asili kujitawala pamoja na sauti za vijana wa jamii ya asili.
Sehemu muhimu ya majadiliano haya inalenga kuhakikisha watu wa jamii za asili wanapata haki ya kujiamulia na kupata ufadhili utakao wawezesha kudai haki zao vyema, kuendeleza maendeleo yao ya kiuchumi, kijamii na kiutamaduni na kufadhili miundo ya utawala wao, kama ilivyoainishwa katika Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Watu wa Kiasili.
Mwenyekiti wa Jukwaa la kudumu la Umoja wa Mataifa kuhusuu watu wa asili Bi. Hindou Oumarou Ibrahim akizungumza katika jukwaa hilo amesema “Kuondolewa vikwazo kwenye upatikanaji wa fedha ni muhimu ili kuhakikisha watu wa asili wanatekeleza kwa vitendo mipango yao na kuwa na njia ya kudumisha kujitawala,”
Kwa upande wake Bwana Li Junhua, ambaye ni msaidizi waKatibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa masuala ya kiuchumi na kijamii (DESA) amesema “unahitaji ufadhili wa muda mrefu, unaotabirika, na wa moja kwa moja kwa Watu wa Asili, ikijumuisha kupitia mifumo ya ufadhili ya umma, ya kibinafsi, na inayoongozwa na Wenyeji ambayo inashirikisha kikamilifu Wanawake na vijana wa kiasili.”
Unaweza kufuatilia moja kwa moja matangazo ya jukwaa hili yanayorushwa mubashara na Umoja wa Mataifa kupitia wavuti wake wa UN Web TV,matangazo yanarushwa kwa lugha rasmi sita za umoja wa Mataifa ambazo ni Kingereza, Kifaransa, Kiarabu, Kichina, Kispanishi na Kirusi.
Mon, 15 Apr 2024 - 11607 - 15 APRILI 2024
- Nigeria inapotimiza miaka 10 tangu tukio la utekwaji nyara la watoto wa kike 275 huko Chibok, kaskazini magharibi mwa taifa hilo, hadi sasa bado watoto 90 wamesalia mateka na nchi hiyo inasalia na kumbukumbu ya tukio linguine la wanafunzi wa shule kutekwa nyara jimboni Kaduna mwezi Machi mwaka huu, hali inayosababisha Umoja wa Mataifa kutoa wito mahsusi.Hii leo katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa hapa jijini New York Marekani, Jukwaa la Kudumu la Umoja wa Mataifa la watu wa asili limeanza rasmi na litadumu kwa muda wa wiki mbili likiwaleta pamoja zaidi ya washiriki 2000 wa jamii za asili kutoka kila pembe ya dunia kujadili masuala mbalimbali. Makala Stella Vuzo, Afisa habari wa kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIS Kenya, anatuletea mazungumzo kati yake na Alois Porokwa, Mkurugenzi wa shirika la NALEPPO kutoka jamii ya Wamaasai aliyesafiri kutoka Kijiji cha Emboreet, Wilaya ya Simajiro, Mkoa wa Manyara, Tanzania kuhudhuria wa Mkutano wa 6 wa Baraza la Mazingira la Umoja wa Mataifa UNEA 6 uliofanyika mwezi uliopita jijini Nairobi, Kenya. Kwa kuwa jamii zinazoishi kiasili wakati mwingine zimekuwa zikilaumiwa kuwa zinachangia katika uharibifu wa mazingira ndipo Stella Vuzo akakumbuka kumuuliza Alois Porokwa swali hili ambalo ni dhana inayohusisha jamii ya Wamaasai kuua wanyama.Na mashinani tunamulika vita nchini Sudan ambayo inaendelea kuwalazimisha mamilioni ya watu kukimbia kuokoa maisha yao. Kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, mkimbizi ambaye alikimbia machafuko nchini humo kuelekea Chad anasimulia changamoto alizozipitia.
Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Mon, 15 Apr 2024 - 11606 - UNICEF: Miaka 10 ya watoto kutekwa Chibok, bado hakuna mifumo ya ulinzi
Nigeria inapotimiza miaka 10 tangu tukio la utekwaji nyara la watoto wa kike 275 huko Chibok, kaskazini magharibi mwa taifa hilo, hadi sasa bado watoto 90 wamesalia mateka na nchi hiyo inasalia na kumbukumbu ya tukio linguine la wanafunzi wa shule kutekwa nyara jimboni Kaduna mwezi Machi mwaka huu, hali inayosababisha Umoja wa Mataifa kutoa wito mahsusi.
Ilikuwa usiku wa tarehe 15, Jumatatu ndipo watoto hao wa kike wenye umri wa kati ya miaka 12 hadi 17 walitekwa na kundi la Boko Haram huko jimboni Borno, na ndio maana kwa mazingira yalivyo sasa, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF linasema safari bado ni ndefu kwa watoto nchini Nigeria kutimiza ndoto yao ya kusoma kwenye mazingira yaliyo salama, kwani ni asilimia 37 tu ya shule kwenye majimbo 10 yaliyo kwenye mazingira hatarishi ndio zina mifumo ya kubaini mapema vitisho kama vile shule kushambuliwa.
Ripoti ya UNICEF iliyotolewa leo Abuja, miji Mkuu wa Nigeira ikipatiwa jina Viwango vya Chini Vya Usalama Shuleni au MSSS kwa lugha ya kiingereza, inaonesha ukweli mchungu wa kufanikisha safari hiyo kwa mtoto nchini Nigeria kuweko shuleni bila uoga.
Mwakilishi wa UNICEF nchini humo Cristian Munduate amesema tukio la kutekwa nyara wasichana wa Chibok ni kengela ya kutuamsha juu ya hatari kubwa watoto wetu wanakabiliwa nayo wanaposaka elimu.
Anasema leo tunapotafakari janga hili na mengine ya hivi karibuni ni dhahiri kuwa juhudi zetu za kulinda mustakabali wa watoto wetu lazima ziimarishwe.
Mwakilishi huyo anasema kwa kuzingatia takwimu zilizotolewa na ambazo zinatia hofu kubwa, ni lazima kupata majawabu ya sio tu dalili bali pia chanzo cha janga hilo la utekaji nyara watoto.
Bi. Munduate amekumbusha kuwa elimu ni haki ya msingi na ni njia muhimu ya kuelekea kuondokana na umaskini. Lakini kwa watoto wengi nchini Nigeria inasalia kuwa ndoto isiyotimizika.
Ripoti ilimulika maeneo 6 ikiwemo mifumo thabiti ya shule, ukatili dhidi ya watoto, majanga ya asili,mizozo ya kila siku na miunmdombinu ya shule na kubaini utofauti mkubwa wa vigezo hivyo katika majimbo yote 36.
Jimbo la Borno liko thabiti kwani limekidhi viwango kwa asilimia 70 ilhali majimbo ya Kaduna na Sokoto bado yako nyuma.
Uchambuzi huu unakuja wakati kuna ripoti za ongezeko la ghasia dhidi ya shule ambapo katika miaka 10 iliyopita, matukio ya mashambulizi yamesababisha watoto zaidi ya 1,680 kutekwa nyara wakiwa shuleni au kwinigneko.
UNICEF inataka Nigeria pamoja na mambo mengine ihakikishe shule kwenye majimbo yote zina rasilimali za kutekeleza MSSS.
Pia itatue pengo la uwiano wa usawa katika hatua za kuimarisha usalama shuleni. Nigeria pia iimarishe usimamizi wa sheria na mikakati ya usalama ya kulinda taasisi za elimu na jamii dhidi ya utekwaji.
Kwa sasa UNICEF inashirikiana na serikali kuhakikisha kila mtoto anakuwa na mazingira salama ya kusomea.
Soma ripoti nzima hapa.
Mon, 15 Apr 2024 - 11605 - Guterres/Kwibuka 30: Vijana kemeeni kauli za chuki kokote muisikiapo na muionapo
Hii leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa, Baraza Kuu limekuwa na tukio maalum la kumbukizi ya miaka 30 ya mauaji ya kimbari nchini Rwanda au KWIBUKA30, ambapo Katibu Mkuu wa Umoja huo, Antonio Guterres ametumia hotuba yake pamoja na mambo mengine kuwasihi vijana kutoka taifa hilo la Afrika Mashariki kukemea chuki kokote wanapoisikia au kuiona.
Tukio lilianza kwa ukumbi kuwa giza na video ya dakika tano ikachezwa kueleza kuwa watu wengi wanaijua Rwanda kuanzia 1994, lakini ilikuweko hata kabla ya ukoloni, na kwamba wakoloni ndio waligawa watu kwa misingi ya makundi licha ya kwamba lugha yao ilikuwa moja. Manusura na watekelezaji wa mauaji walizungumza pia kwenye video hiyo!
Video ikafuatiwa na kuwasha mishumaa kukumbuka waliouawa na kisha hotuba ambapo Katibu Mkuu Guterres akawa ana ujumbe mahsusi kwa vijana wa Rwanda walioshiriki kimtandao na pia ukumbini.
Anasema rafiki zangu, katu hatutasahau vitisho vya siku 100. Lakini tunahitaji msaada wenu. Tunahitaij sauti na uchechemuzi wenu kusongesha kumbukizi za wale waliouawa. Na kukemea chuki kokote muisikiako au muionapo. Mijini kwenu, vitongojini, shuleni, mtandaoni, popote pale na kila mahali.
Akaendelea kusema kuwa hebu na tuondoe chuki na ukosefu wa stahmala kokote tuvionapo. Kumbukumbu za waliouawa zichochee vitendo vyetu, na azma yetu ya kuhakikisha dunia bora na salama kwa watu wote.
Guterres amesema Umoja wa Mataifa kila wakati utashikamana na vijana katika juhudi hizo muhimu.
Mauaji ya kimbari Rwanda ya mwaka 1994 yalifanyika kwa siku 100 kuanzia tarehe 7 Aprili na zaidi ya watu milioni moja waliuawa, wengi wao Watutsi, halikadhalika wahutu wenye msimamo wa kati na watu wengine waliokuwa wanapinga mauaji hayo.
Katibu Mkuu amesema siku hizo 100 ziliakisi ubaya zaidi wa ubinadamu. Lakini kipindi baada ya mauaji kilidhihirisha ubora wa roho ya ubinadamu: mnepo, maridhiano, ujasiri na nguvu.
Amesema simulizi za manusura ni ushahidi wa nguvu ya matumaini na msamaha ambapo amemtaja manusura Laurence Niyonangira ambaye alipoteza jamaa zake 37 wakati wa mauaji hayo.
“Alichagua kusamehe mmoja wa wahusika wa mauaji ya familia yake baada ya mhusika kuungama na kutumikia muda jela kwa makosa aliyotenda. Kama manusura, Laurence alisema ‘tunaweza kuponya vidonda kwa kushirikiana wale waliovisababisha.” Amesema Guterres.
Hivyo Katibu Mkuu amesema mwaka huu ambapo kumbukizi inajikita kwenye mzizi wa mauaji ya kimbari ambao ni chuki, ambayo sasa inakolezwa na mitandao ya kijamii, “ni lazima tushikamane pamoja na kurejelea shinikizo la dunia la kuridhia na kutekeleza kikamilifu Mkataba wa Kimataifa wa Kuzuia na Kuadhibu Uhalifu wa Mauaji ya kimbari, huku tukiimarisha mifumo ya kuzuia, kuelimisha vizazi vipya kuhusu mauaji ya kimbari yaliyopita na kukabili taarifa potofu na za uongo ambazo huchochea kauli za chuki na nia na vitendo ya mauaji ya kimbari.”
Fri, 12 Apr 2024 - 11604 - Kikosi cha 11 cha walinda amani kutoka Tanzania, TANZBATT-11 watoa matibabu kwa raia nchini DRC
Kikosi cha 11 cha walinda amani kutoka Tanzania, TANZBATT-11 kinachohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO wametekeleza wajibu wao wa kulinda raia kwa kuwapatia huduma ya matibabu kwenye Kijiji cha Matembo kilichoko mjini Beni jimboni Kivu Kaskazini. Shuhuda wetu ni Kapteni Fadhila Nayopa, Afisa habari wa kikosi hicho.
Fri, 12 Apr 2024 - 11603 - 12 APRILI 2024
- Hii leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa, Baraza Kuu limekuwa na tukio maalum la kumbukizi ya miaka 30 ya mauaji ya kimbari nchini Rwanda au KWIBUKA30, ambapo Katibu Mkuu wa Umoja huo, Antonio Guterres ametumia hotuba yake pamoja na mambo mengine kuwasihi vijana kutoka taifa hilo la Afrika Mashariki kukemea chuki kokote wanapoisikia au kuiona.Tarehe 15 April wiki ijayo siku ya jumatatu nchi ya Sudan itatimiza mwaka mmoja rasmi tangu kuanza kwa mzozo kati ya Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) na Vikosi vya jeshi la Sudan (SAF). Vita hiyo imesababisha maelfu ya watu kuwa wakimbizi wa ndani na wengine kusaka hifadhi nchi Jirani. Mashirika ya misaada ya kibinadamu nayo yamekuwa mstari wa mbele kusaidia wananchi wenye uhitaji japo yanakabiliwa na ufinyu wa bajeti. Makala tunakupeleka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako kikosi cha 11 cha walinda amani kutoka Tanzania, TANZBATT-11 kinachohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO wametekeleza wajibu wao wa kulinda raia kwa kuwapatia huduma ya matibabu kwenye Kijiji cha Matembo kilichoko mjini Beni jimboni Kivu Kaskazini.Na mashinani tunakuletea ujumbe wa Marthe Nyangoma, mtumishi wa umma kutoka eneo la Irumu, huko Ituri nchini DRC, ambaye kwa uwezeshaji wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa MONUSCO, anahamasisha jamii dhidi ya taarifa potofu na kauli za chuki akisistiza kuwa kabla ya kuwasilisha taarifa, lazima zidhibitishwe ili kuepusha mgawanyiko.
Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Fri, 12 Apr 2024 - 11602 - Wakimbizi kutoka Sudan wanoingia Sudan Kusini wanaendelea kuongezeka
Tarehe 15 April wiki ijayo siku ya jumatatu nchi ya Sudan itatimiza mwaka mmoja rasmi tangu kuanza kwa mzozo kati ya Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) na Vikosi vya jeshi la Sudan (SAF). Vita hiyo imesababisha maelfu ya watu kuwa wakimbizi wa ndani na wengine kusaka hifadhi nchi Jirani. Mashirika ya misaada ya kibinadamu nayo yamekuwa mstari wa mbele kusaidia wananchi wenye uhitaji japo yanakabiliwa na ufinyu wa bajeti.
Video ya shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP inaanza kwa kuonesha wananchi wakiwa na vifurushi mikononi, wengine wakiwa wamepanda usafiri unaosukumwa na ngombe na wengine mabasi wakiingia katika mpaka wa Joda nchini Sudan kusini wakitokea nchini Sudan.
“Tumesafiri kwakutumia basi na imetuchukua siku mbili kufika hapa”, ndivyo anavyosema Hamida Ibrahim mkimbizi kutoka Sudan. Anaendelea kwa kueleza kile wanachohitaji kwa sasa.
“Tunahitaji chakula. Huo ndio msaada wa haraka tunaohitaji ili tuweze kuishi. Kwa sababu tupo na watoto na hawana uwoga wanachojua wanakuja hapa kufata usalama”
Kiongozi wa WFP katika eneo hili Leonidace Rugemalila anasema mzozo huu wa Sudan umemuathiri kila mtu.
“Katika kipindi cha miezi mitatu idadi ya watu wanaovuka mpaka huu kila siku imeongezeka kutoka watu 1,500 mpaka takriban watu 2,500.”
Naye Mkuu wa lishe Aachal Chand anasema wengi wa waaathirika wa mzozo nchini Sudan ni wanawake na watoto, na walioathirika zaidi ni wajawazito, wanawake wanaonyonyesha na watoto wenye umri chini ya miaka mitano.
“Wanapovuka mpaka, mtu yeyote mwenye umri zaidi ya miaka mitano anapatiwa biskuti za lishe kama chakula cha haraka chakumpa lishe. Kwa watoto chini ya miaka mitano tunawapa chakula maalum cha lishe. Kuanzia saa mbili asubuhi mpaka wakati huu saa 10 jioni wameshatoa lishe kwa takriban watoto 400 ambao wamepokea matibabu ya utapiamlo au huduma za matibabu.”
Chand ameeleza kuwa WFP na wadau wake wanaendelea kutoa msaada hata hivyo wanakabiliwa na ufinyu wa bajeti.
“Watu wanahitaji msaada wa afya na lishe, watu wanahitaji usaidizi katika kupata uhakika wa chakula, watu wanahitaji msaada wa kuweza kuwasaidia kufika katika maeneo wanayotaka kuelekea.Sudan na athari zake kwa nchini ya Sudan Kusini zinasahaulika na tunatakiwa kuhakikisha hatusahau mzozo huu kwasababu hawa ni watu na wanapata athari halisi katika maisha yao.”
Fri, 12 Apr 2024 - 11601 - 11 APRILI 2024
- Wakati mgogoro nchini Sudan ukiingia katika mwaka wake wa pili, Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kutafuta Ukweli nchini Sudan umezitaka pande zinazokinzana zisitishe mapigano, zilinde raia na kuruhusu mtiririko wa misaada. Taarifa iliyochapishwa leo na OHCHR imemnukuu Mwenyekiti wa ujumbe huo, Mohamed Chande Othman akisema, "Pande zinazopigana Sudan zina wajibu wa kisheria kuwalinda raia, lakini zimeonesha kutojali kufanya hivyo.Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF, limetangaza kwamba moja ya magari yake jana yakisubiri kuingia kaskazini mwa Gaza lilishambuliwa kwa risasi za moto. Pia UNICEF imechapisha katika ukurasa wake wa mtandao wa X video ya Msemaji wa shirika hilo, Tess Ingram akiwa katika hospitali ya Deir Al Balah, akizungumza kuhusu mtoto Omar mwenye umri wa miaka saba ambaye amelazwa hapo akisumbuliwa na utapiamlo baada ya kula nyasi kwa wiki kadhaa zilizopita. Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) limezindua mradi wa thamani ya euro milioni 15 sawa na dola milioni 16.29 unaofadhiliwa na Muungano wa Ulaya (EU) ili kusaidia sekta ya misitu ya Uganda kuchangia kwa uendelevu zaidi kwa uchumi na mazingira. Mpango wa miaka mitano wa Minyororo ya Thamani Endelevu ya malighafi za miti nchini Uganda, unalenga kuhakikisha upatikanaji endelevu wa malighafi halali za miti kutoka katika misitu iliyopandwa, kuongeza uwezo wa usindikaji na mahitaji ya soko ya bidhaa za mbao na kuboresha uwepo na upatikanaji wa ufadhili nafuu.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo fursa ni yake mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania , BAKITA anafafanua maana ya neno “PAMBAJIO”.
Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Thu, 11 Apr 2024 - 11600 - Jifunze Kiswahili: Pata uchambuzi wa neno “PAMBAJIO”Thu, 11 Apr 2024
- 11599 - Alice Nderitu: Dunia bado haijajifunza lolote kuhusu mauaji ya kimbari ya Rwanda dhidi ya Watutsi
Miaka 30 iliyopita mauaji ya kimbari dhidi ya Watutsi nchini Rwanda yaliyoishangaza, dunia yalitokea kuanzia Aprili 7 mwaka 1994 na kudumu kwa siku 100 zilioghubikwa na ukatili wa hali ya juu na mamilioni ya watu kufurushwa makwao. Tangu wakati huo Umoja wa Mataifa umekuwa mstari wa mbele kuchukua hatua kuhakikisha asilani jinamizi hilo halitokei tena popote pale duniani. Manusura wa mauaji hayo wanasemaje kuhusu kumbukumbu hii? Na je dunia imejifunza nini kutokana na mauaji hayo ya Rwanda taifa ambalo limeshafungua ukurasa mpya na kuyapa kisogo? Twende mjini Kigali ambako kumbukumbu kubwa imefanyika mwishoni mwa wiki na itaendelea kwa siku 100, shuhuda wetu ni Eugene Uwimana afisa mawasiliano wa ofisi ya mratibu mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Rwanda.
Tue, 09 Apr 2024 - 11598 - 09 APRILI 2024
- Baada ya huduma ya ulinzi wa amani kwa zaidi ya miaka 20 huko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO, walinda amani kutoka China, hii leo wameondoka kutoka kambi yao iliyoko nje kidogo ya mji mkuu wa jimbo la Kivu Kusini, Bukavu ambako walishiriki kwa kiasi kikubwa katika ujenzi wa miundombinu.Msemaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) Olga Sarrado Mur katika mkutano na waandishi wa habari leo mjini Geneva, Uswisi ameeleza kwamba vita nchini Sudan ikikaribia kutimiza mwaka mmoja kamili na ikiendelea kupamba moto, idadi ya Wasudan waliolazimika kukimbia sasa imepita watu milioni 8.5, huku milioni 1.8 kati yao wakiwa wamevuka mipaka ya nchi. Na kwa mujibu wa Ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) iliyotolewa leo, idadi ya watu wanaofariki dunia kutokana na virusi vya homa ya ini inaongezeka. Ugonjwa huo ni wa pili kwa kusababisha vifo vya watu milioni 1.3 kwa mwaka, sawa na ugonjwa wa kifua kikuu, ambao ni ugonjwa wa kuambukiza unaosababisha vifo vingi zaidi kwa sasa. Hata hivyo WHO inasema lengo la kutokomeza Homa ya ini ifikapo 2030 bado linapaswa kufikiwa.Na katika mashinani tutaelekea nchini Sudan Kusini kusikia ujumbe kuhusu hatari vilipuzi na mabomu ya kutegwa ardhini, salia hapo tafadhali.
Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Tue, 09 Apr 2024 - 11597 - Mariam Suleiman: Wanawake tuna ujuzi, tuna uweo na tunaweza
Mwanamke akiwezeshwa anaweza, huo ndio umekuwa usemi wa Umoja wa Mataifa ukipigia chepuo wanawake kujumishwa katika kila Nyanja ya Maisha ili waweze kujikwamua kiuchumi na kuchangia katika maendeleo ya jamii. Usemi huo unaungwa mkono na mwanamke mkimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC ambaye sasa anaishi Kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya.
Kutana na Mariam Suleiman ambaye kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR anasema vita ilimfungisha virago Congo DRC hadi hapa kambini Kakuma, ingawa ilimvurugia amani yake haikumkatishia ndoto zake za kuendelea na ufundi wa kuchomelea vyuma na pia kuwa mkufunzi wa kazi hiyo.
“Katika kuchomelea vyuma ninafurahia sana kufanyakazi kazi hiyo ninapokwenda kazini na kujikuta ni mwanamke peke yangu uwanjani na hivyo ninajivunia sana kwa sababu sio kazi rahisi kwenda hapo ukiwa mwanamke peke yako katikati ya wanaume 15. Hivyo ninajivunia sana kuwa mchomelea vyuma na mkufunzi wa kuchomelea na kutengeneza vyuma”
Kwa Mariam matunda ya kazi yake yako dhahiri.
“Moja ya kazi zangu zinazovutia ambazo nimefanya ni lango kuu la kliniki 4”
Pamoja na mafanikio hayo Marian anatamani kusoma zaidi kuongeza ujuzi.
“Nilisoma hadi daraja la sita hiyo ni ngazi ya Diploma. Natamani kuchimba ndani zaidi ya hii tasnia ya kuchomelea vyuma lakini hapa Kenya hatuna hiyo kozi. Ipo katika taasisi ya uchomeleaji vyuma ya Afrika Kusini. Ningependa kwenda huko na kusoma uchomeleaji vyuma chini ya maji.”
Na kwa kuwa yeye ameweza anaamini hakuna kinachomshinda mwanamke kwani
“Wanawake tuna uwezo, wanawake tuna ujuzi, wanawake tunaweza kufanyakazi zinazofanywa na wanaume, wanawake tunaweza kufurahia kazi zetu, wanawake hebu tusimame kidete tunaweza”
Mon, 08 Apr 2024 - 11596 - Raia nchini DRC wasimulia jinsi wanavyonufaika na miradi iliyofanikishwa na MONUSCO
Kadri siku za MONUSCO kuondoka nchini DRC zinavyokaribia, vivyo hivyo wananchi wanufaika wa miradi iliyofanikishwa na ujumbe huo wanazidi kujitokeza kuelezea hisia zao, kwani ujumbe huo unatakiwa uwe umeondoka nchini humo mwishoni mwa mwaka huu wa 2024.
Miongoni mwa wanufaika ni shule ya msingi Lubumba hapa Kamanyola na Mwalimu Mkuu Texas Chekabiri anaelezea hali ilivyokuwa. Assumpta Massoi amefuatilia na kutuelezea zaidi katika makala hii.
Mon, 08 Apr 2024 - 11595 - 08 APRILI 2024
- Huko Gaza, watoa misaada ya kibinadamu wakiwa na wasiwasi mkubwa juu ya mipango ya Israel kuvamia eneo la Rafah hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa Palestina imeanza mchakato wa kuwa mwanachama rasmi wa Umoja wa Mataifa kwani hivi sasa ujumbe wake ni uangalizi usioipatia hadhi ya kupiga kura. Mchakato huo unaanzia ndani ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.Mwanamke akiwezeshwa anaweza, huo ndio umekuwa usemi wa Umoja wa Mataifa ukipigia chepuo wanawake kujumishwa katika kila Nyanja ya Maisha ili waweze kujikwamua kiuchumi na kuchangia katika maendeleo ya jamii. Usemi huo unaungwa mkono na mwanamke mkimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC ambaye sasa anaishi Kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya. Katika makala makala ambapo Assumpta Massoi anatupeleka jimboni Kivu Kusini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kusikia manufaa ya uwepo wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MONUSCO ambao sasa unafunga virago baada ya kuhudumu kwa miaka 22.Na katika mashinani tutakuwa Tanzania kuangalia endapo lengo la ujumuishwaji wanawake katika huduma za kifedha litatimia ifikapo mwaka 2030.
Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Mon, 08 Apr 2024 - 11594 - Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kujadili ombi la Palestina kuwa mwanachama
Huko Gaza, watoa misaada ya kibinadamu wakiwa na wasiwasi mkubwa juu ya mipango ya Israel kuvamia eneo la Rafah hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa Palestina imeanza mchakato wa kuwa mwanachama rasmi wa Umoja wa Mataifa kwani hivi sasa ujumbe wake ni uangalizi usioipatia hadhi ya kupiga kura. Mchakato huo unaanzia ndani ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Ratiba ya mikutano hii leo hapa katika makao Makuu ya Umoja wa Mataifa inaonesha kuwa Baraza la Usalama lenye wajumbe 15 kuanzia saa nne kamili asubuhi mpaka saa sita kamili mchana kwa saa za New York Marekani, litakutana kwanza katika kikao cha faragha na kisha kikao kitafunguliwa kwa umma kusikiliza wanapojadili ombi la Palestina kuwa mwanachama wa Umoja wa Mataifa.
Palestina imekuwa ikishiriki katika masuala mbalimbali ndani ya Umoja wa Mataifa lakini kwa ngazi ya muangalizi na sasa uongozi wa Palestina inataka hadhi hiyo kubadilishwa na kuwa mwanachama kama wanachama wengine 193 wa Umoja wa Mataifa.
Wajumbe katika baraza hilo la UN katika mazungumzo yao watazingatia ombi la Wapalestina la mwaka 2011 baada ya ombi lililowasilishwa kwa njia ya maandishi wiki iliyopita na Bwana Riyad Mansour, Waziri wa Mambo ya Nje wa Mamlaka ya Palestina ambaye pia ni Mwakilishi wa Kudumu wa Umoja wa Mataifa.
Wakati tukisubiri kusikia nini kitajadiliwa na Baraza hilo, huko Ukanda wa Gaza hali bado si hali kwani watoa misada ya kibinadamu wana wasiwasi mkubwa juu ya uvamizi unaopangwa kufanywa na Israel katika eneo la Rafah ambalo limefurika wapalestina waliokimbia kutoka maeneo mbalimbali ikiwemo kusini, kati na kaskazini mwa Gaza kufuatia mapigano yanayoendelea baina ya wanamgambo wa kipalestina wa Hamas na wanajeshi wa Israel.
Mratibu wa Umoja wa Mataifa wa Misaada ya Kibinadamu katika eneo la Palestina linalokaliwa kwa mabavu, Jamie McGoldrick, akizungumza na Idhaa ya Umoja wa Mataifa hapo jana alisema kuwa “Mpango unaendelea wa uvamizi wa Rafah, ambao unaweza kusababisha hadi watu 800,000, kuyakimbia makazi yao…. Tulipata tabu sana kuleta mahitaji muhimu hapa kama vitu ambavyo si vyakula, malazi, nyenzo mbalimbali na maji…. Hatuna tena uwezo na rasilimali kwa sasa. Na tunatatizika sana kujiandaa.”
Ili kuongeza kiwango cha usaidizi wa kibinadamu kufika eneo hilo, Umoja wa Mataifa unaunga mkono wito wa bandari ya Ashdod ya Israel kufunguliwa tena hulo kaskazini mwa Gaza, ili misaada zaidi ipatikane kupitia nchi ya Jordan.
Mon, 08 Apr 2024 - 11593 - UNICEF na jitihada za kuimarisha huduma za Afya ya Akili kwa vijana nchini Rwanda
Makala hii inaeleza safari ya matumaini na uthabiti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNICEF Rwanda linaposhirikiana na Rwanda Biomedical Center (shirika kuu la kitaifa la utekelezaji wa afya lenye jukumu la kufanya utafiti wa kisayansi, kutoa huduma za uchunguzi, na kutekeleza afua za kiafya ili kulinda taifa la Rwanda dhidi ya magonjwa na matishio mengine ya kiafya) kuleta mapinduzi katika huduma za afya ya akili kwa vijana. Katika mpango huu wa kutia moyo, UNICEF inavunja vizuizi na kukuza ujasiri kwa kutoa usaidizi muhimu kama vile nasaha shuleni
Fri, 05 Apr 2024 - 11592 - Mlo shuleni wawawezesha wasichana kuepuka ndoa za utotoni Sudan Kusini
Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa chakula duniani WFP nchini Sudan Kusini kupitia programu yake ya chakula shuleni imefanikiwa kuwasaidi wasichana wengi kuepukana na ndoa za utotoni.
Sudan Kusini ni moja kati ya mataifa yenye viwango vya chini vya watu wanaojua kusoma na kuandika hususani kwa wasichana. Jamii katika taifa hilo la afrika ya mashariki huwaoza mabinti ikiwa ni njia moja wapo ya familia kujipatia mali na hivyo mtoto wa kike hujikuta akikosa haki yake ya msingi ya kupata elimu.
Huko Kapoeta Mashariki katika jimbo la Equatoria mashariki, shule moja ya msingi ambayo hatutaitaja jina imekuwa kimbilio la wasichana walio katka hatari ya kuolewa katika umri mdogo, mmoja wa wanafunzi wa shule hiyo ni Grace mwenye umri wa miaka 16 anasema shule hiyo imekuwa nikama peponi.
“Nilipokuwa kijijini, wakati baba yangu alikuwa hai, maisha yalikuwa sawa na nilifurahia kila kitu maishani. Lakini mara baada ya baba yangu kufariki, hapo ndipo maisha yangu yakawa magumu, kaka yangu alitaka niolewe katika umri mdogo, na hapo ndipo maisha yakawa magumu”.
Grace anasema anachosikita ni kuwa watoto wa kike hawaheshimiki.
“Kwa sababu mimi ni mtoto wa kike maisha ya kijijini sio mazuri, tunatazamwa kama chanzo cha utajiri, na sisi ndio tunalazimika kufanya kazi za mashambani, kitu chochote kinachohusiana na shule hakithaminiwi, na hawataki hata kujua ni nini. Wao wanaona kama kitu kisicho na maana, hawajui chochote kuhusu elimu, na hawako tayari kwa hilo”.
Hellen Locham ni mwalimu wa shule anayosoma Grace na anasema wamekuwa wakihamasisha jamii kuhusu umuhimu wa shule kwa wasichana.
“Hawa wasichana wanaitwa "washindi" kwa sababu wasichana hawa wanalazimishwa kuolewa wakiwa na umri wa miaka 9, na wengine huposwa wangali wadogo, na walifanikiwa kukimbia vijijini, wakiteseka njiani na wamefanikiwa kuja shuleni”. Tumekuwa tukiwaambia watu ikiwa unapata msichana ambaye anapitia changamoto, msichana ambaye amelazimishwa kuolewa, wanaweza kupata elimu wanayotaka".
Mwalimu Hellen Locham anasema mbali na shule kupokea wasichana lakini wanalishukuru zaidi shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani kwa kuwawezesha kupata chakula shuleni.
Chakula kuwa shuleni ni muhimu sana, ikiwa hakuna chakula na haujala kitu huwezi kuwa katika nafasi ya kuwa darasani, huwezi kufanya chochote, WFP imesaidia sana shule hii, wakati wa likizo hali inekuwa ngumu kwa wasichana hawa kuwa shuleni ikiwa hakuna chakula. Wengi wao wangaliweza kukimbia, wangaliweza kurudi makwao, wangesema bora niende kuteseka kuliko kufa hapa kwa njaa.
WFP inaendelea kusaidia wasichana walio hatarini zaidi kwa kuwaatia msaada wa chakula shuleni wakati wa likizo.
Fri, 05 Apr 2024 - 11591 - 05 APRILI 2024
- Kesho kutwa jumapili ikiwa ndio itatimu miezi sita ya mzozo wa Gaza, huko Mashariki ya Kati, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo amezungumza na waandishi wa habari jijini New York, Marekani akirejelea wito wake wa sitisho la mapigano kwa misinigi ya kiutu, kuachiliwa kwa mateka wote bila masharti, ulinzi wa raia na misaada ya kiutu ifikie walengwa bila vikwazo vyovyote huku akikgusia pia Israeli kutumia akili mnemba kwenye operesheni zake.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa chakula duniani WFP nchini Sudan Kusini kupitia programu yake ya chakula shuleni imefanikiwa kuwasaidi wasichana wengi kuepukana na ndoa za utotoni. Katika makala Anold Kayanda anatupeleka nchini Rwanda kusikia programu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF Rwanda kudhibiti tatizo la changamoto ya afya ya akili kwa vijana balehe.Na katika mashinani tutaelekea nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC kusikia simulizi ya mkimbizi wa ndani”.
Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Fri, 05 Apr 2024 - 11590 - Kuelekea miezi 6 ya mzozo wa Gaza, Guterres apinga matumizi ya akili mnemba kusaka wahalifu
Kesho kutwa jumapili ikiwa ndio itatimu miezi sita ya mzozo wa Gaza, huko Mashariki ya Kati, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo amezungumza na waandishi wa habari jijini New York, Marekani akirejelea wito wake wa sitisho la mapigano kwa misinigi ya kiutu, kuachiliwa kwa mateka wote bila masharti, ulinzi wa raia na misaada ya kiutu ifikie walengwa bila vikwazo vyovyote huku akikgusia pia Israeli kutumia akili mnemba kwenye operesheni zake.
Guterres akianza hotuba yake kwa kuelezea kuwa Jumapili hii inatimu miezi sita tangu mashambulizi hayo na kuelezea kuwa tarehe 7 Oktoba ni siku ya machungu kwa Israel na dunia, kwani Umoja wa Mataifa na yeye binafsi wanaomboleza vifo vya waisrael 1,200 waliouawa hadi sasa. Hakuna kinachohalalisha mashambulizi yale ya Hamas, amesema Guterres akisema pia katika kipindi cha miezi sita pia wapalestina zaidi ya 32,000 wameuawa na wengine zaid iya 75,000 wamejeruhiwa. Maisha ya watu yametwamishwa na heshima ya sheria ya kimataifa ya kibinadamu imesambaratishwa.
Akarejelea ziara yake ya hivi karibuni kwenye kivuko cha Rafah ambako anasema nilikutana na wasaidizi wa kiutu wabobezi walionieleza wazi kuwa janga hili na machungu ya Gaza si ya kawaida na hawajawahi kushuhudia kokote.
Na zaidi ya yote anasema aliona misururu mirefu ya malori yenye shehena za misaada yakiwa yamezuiwa kuingia Gaza.
Anasema pindi milango ya misaada inapofungwa, milango ya njaa inafunguliwa. Zaidi ya watu milioni moja wanakabiliwa na njaa. Watoto hivi sasa wanakuga kwa njaa na kukosa maji. Hakuna kinachohalalisha adhabu hii ya jumla kwa wananchi wa Palestina.
Ameelezea pia kuchukizwa na kitendo cha Israel kutumia Akili Mnemba kusaka wahalifu Gaza tena kwenye maeneo yenye watu wengi.
Akili Mnemba inapaswa kutumika kwa manufaa na sio kuchangia kwenye kusongesha vita.
Amekumbusha kuwa wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa na mashirika ya kiraia na waandishi wa habari nao wameuawa kwenye mzozo huo. Na zaidi ya yote.
Vita dhidi ya habari imeongeza machungu.. kuficha ukweli na kurushiana lawama. Kuwanyima waandishi wa habari wa kimataifa kibali cha kuingia Gaza kunaruhusu kusambaa kwa habari potofu na za uongo.
Ametamatisha hotuba yake ya dakika 7 kwa kutaka pia uchunguzi huru wa kilichotokea Gaza, utekelezaji wa kikamilifu wa azimio la wiki iliyopita la Baraza la Usalama la kutaka sitisho la mapigano na misaada ifikie walengwa kwani baa la njaa linajongea Gaza.
Fri, 05 Apr 2024 - 11589 - Ujumuishwaji wa wanawake katika huduma za kifedha ni muhimu - Nangi Massawe, Benki Kuu Tanzania
Lengo namba 5 la maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa au SDG5 linahimiza kila nchi kuhakikisha wanawake wanawezeshwa na kujumuishwa katika kila nyanja ya Maisha ili kuhakikisha ifikapo mwaka 2030 hawasalii nyuma katika maendeleo.
Moja ya masuala yanayotiliwa msukumo zaidi hivi sasa ni ujumuishwaji wa wanwake katika masuala ya huduma za kifedha n anchi nyingi zimeanza kuchukua hatua ikiwemo Tanzania. Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili amezungumza na Nangi Moses Massawe kutoka Benki Kuu ya Tanzania ambaye ni meneja wa kitengo cha huduma jumuishi za kifedha.
Thu, 04 Apr 2024 - 11588 - Jifunze Kiswahili: Tofauti ya maneno “Adhuhuri na Alasiri.”Thu, 04 Apr 2024
- 11587 - 04 APRILI 2024
- Leo ni siku ya kimataifa ya uelimishaji kuhusu mabomu ya kutegwa ardhini na msaada wa kuchukua hatua dhidi ya mabomu hayo. Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, mabomu, vilipuzi na vifaa vingine vya mlipuko vinaendelea kuua na kujeruhi watu katika maeneo mengi yenye changamoto kubwa za migogoro duniani na matokeo yake vifaa hivyo vya mlipuko, kwa wastani hukatili maisha ya mtu mmoja kila saa, na waathirika wakubwa wakiwa ni watoto.Mratibu wa Misaada ya Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa katika eneo la Palestina linalokaliwa kwa mabavu, Jamie McGoldrick anaelekea Gaza leo. Umoja wa Mataifa unaeleza kuwa mapigano makali kati ya wanajeshi wa Israel na makundi yenye silaha ya Palestina yanaendelea kuripotiwa katika sehemu kubwa ya Ukanda wa Gaza. Mfumo wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni (WHO) wa Ufuatiliaji kuhusu Mashambulizi dhidi ya Huduma za Afya (SSA) wameeleza kuwa inatia wasiwasi kwamba nchini Ukraine wahudumu wa afya katika gari za wagonjwa na wafanyakazi wengine wanaotoa huduma za usafiri wa afya wanakabiliwa na hatari ya kujeruhiwa na kifo mara 3 zaidi ya ile ya wafanyakazi wengine wa huduma za afya.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili, mchambuzi wetu Dkt. Josephat Gitonga, kutoka Kenya ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi kwenye kitivo cha tafsiri na ukalimani anatufafanulia tofauti ya “Adhuhuri na Alasiri.”.
Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Thu, 04 Apr 2024 - 11586 - UNCTAD, UNECA, Kenya kuunda viashirio vipya vya kupima usawa wa kijinsia katika sekta ya biashara.
Umoja wa Mataifa umekuwa ukipigia upatu lengo namba tano la Malengo Endelevu ya Umoja huo linalohimiza usawa kwa wote katika nyanja zote ifikapo mwaka 2030. Hata hivyo ili kuelewa jinsi biashara inavyoathiri wanaume na wanawake ni muhimu kuunda sera za biashara zinazojumuisha zaidi na zenye usawa ambazo zinakuza usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa kiuchumi kwa wote,hii inahitaji takwimu nzuri za kitaifa kuhusu jinsia katika biashara.
Kwa msaada wa shirika la Umoja wa Mataifa la biashara na maendeleo UNCTAD na Tume ya Umoja wa Mataifa ya Kiuchumi ya Afrika UNECA, Kenya inaunda viashirio vipya vya kupima usawa wa kijinsia katika sekta ya biashara. Evarist Mapesa amefuatilia taarifa hiyo kwa kina na kutuandalia makala hii.
Wed, 03 Apr 2024 - 11585 - Mbinu za medani tulizopatiwa ni za kimataifa- Afisa FARDC
Siku zikizidi kuhesabiwa kwa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO, kuondoka nchini humo, ujumbe huo unaendelea kutekeleza wajibu wake wa kujengea uwezo jeshi la serikali, FARDC kuweza kukabili vikundi vilivyojihami ambavyo vinatajwa kuhusika na asilimia 65 ya matukio ya ukiukwaji wa haki za binadamu nchini humo mwezi Februari mwaka huu, kwa mujibu wa ripoti ya pamoja ya Umoja wa Mataifa na serikali. Je, FARDC linajengewa uwezo gani? Assumpta Massoi anafafanua zaidi.
Hapa si uwanja wa vita bali ni uwanja wa mazoezi! Wanajeshi 30 wa FARDC au jeshi la serikali nchini DRC wakiwa kwenye mafunzo ya kulenga shabaha. Mbele kuna karatasi lililochorwa binadamu na sasa wanatakiwa kulenga maeneo mbali mbali ya mwili yaliyowekwa alama.
Ni mbinu wanazopatiwa na walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Brazil, hapa Beni jimboni Kivu Kaskazini ili waweze kukabiliana na waasi kwenye maeneo misituni. Kapteni Rombaut Mukoka ni Afisa wa jeshi la FARDC na anasema, “Mafunzo haya ni muhimu sana. Yanapaswa kuendelea ili hatimaye wanajeshi wetu waweze kunufaika. Hizi mbinu walizojifunza ni mpya sana kwetu na zinatambulika katika medani za kimataifa.”
Mafunzo ya kulenga shabaha yanaendelea na kisha mkufunzi kutoka Brazil anajongea kwenye picha ile akiwa na mmoja wa wanafunzi ili kuonesha ni wapi haswa wanapaswa kulenga.
Jenerali Luciano Alfred Matamba ni Mkuu wa kikosi cha kujibu mashambulizi, FIB cha MONUSCO mjini Beni na anafafanua lengo la mafunzo hayo yaliyofanyika kwa wiki tatu.
“Lengo la mafunzo haya ni kuwapatia mbinu na ufundi za kuendesha operesheni msituni. Kama unavyofahamu hapa Kivu Kaskazini tuko kwenye eneo la operesheni ambalo kwa kiasi kikubwa ni pori na mashambulizi yanayofanywa na waasi wa ADF yanahitaji mbinu mtu kuwa na hizo mbinu za kupigana msituni. FARDC [EF EI AR DE SE] ni wadau wetu ambao tunapaswa kushirikiana nao kwa mujibu wa azimio la Umoja wa Mataifa namba 2717 [Mbili Saba Moja Saba]. Ni pale tu ambapo tutajifunza pamoja na kuwa na mbinu sawa ndio tutaweza kutatua matatizo yaliyoko hapa.”
Wed, 03 Apr 2024 - 11584 - 03 APRILI 2024
- Mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa leo kwa mara nyingine yameonya kwamba bila dalili zozote za usitishaji mapigano Gaza hali ya kibinadamu inaendelea kuwa janga huku mashambulizi ya Israel yakiendelea kukatili maisha, kufurusha watu na kusababisha uharibifu usioelezeka na njaa nayo ikiongeza hofu ya hatma ya watu wa eneo hilo.Siku zikizidi kuhesabiwa kwa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO, kuondoka nchini humo, ujumbe huo unaendelea kutekeleza wajibu wake wa kujengea uwezo jeshi la serikali, FARDC kuweza kukabili vikundi vilivyojihami ambavyo vinatajwa kuhusika na asilimia 65 ya matukio ya ukiukwaji wa haki za binadamu nchini humo mwezi Februari mwaka huu, kwa mujibu wa ripoti ya pamoja ya Umoja wa Mataifa na serikali. Makala inatupeleka nchini kenya ambako serikali ya nchi hiyo kwa kushirikiana na mashirika ya Umoja wa Mataifa wanaunda viashiria vipya ya kupima usawa wa kijinsia katika biashara.Na mashinani tunakupeleka nchini Tanzania kusikia ujumbe kuhusu jinsi ambavyo miradi ya maji mkoani Kigoma inavyowasaidia wanfunzi.
Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Wed, 03 Apr 2024 - 11583 - UN - Bila usitishaji mapigano hali ya kibinadamu inaendelea kuwa tete Gaza
Mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa leo kwa mara nyingine yameonya kwamba bila dalili zozote za usitishaji mapigano Gaza hali ya kibinadamu inaendelea kuwa janga huku mashambulizi ya Israel yakiendelea kukatili maisha, kufurusha watu na kusababisha uharibifu usioelezeka na njaa nayo ikiongeza hofu ya hatma ya watu wa eneo hilo.
Asante Anold kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA usiku wa kuamkia leo makombora ya Israel yameendelea kuvurumishwa kuelekea Gaza Kaskazini, Khan Younis na Rafah ambako takriban Wapalestina milioni 1.2 sasa wanaishi katika makazi rasmi na yasiyo rasmi na hivyo kuwaongezea hofu ya mustakbali wa maisha yao.
Pia shirika hilo linasema fursa ya kufikisha misaada ya kibinadamu kwa wenye uhitaji mkubwa bado ni mtihani hasa kutokana na mamlaka ya Israel kuendelea kulinyima vibali shirika la UNRWA kufikisha msaada muhimu wa chakula na mahitaji mengine hasa Gaza Kaskazini.
Hatua hiyo kulingana na shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura OCHA imezidisha njaa kwa watu ambao tayari wako taaban na mapigano yanayoendelea.
Tangu Machi mosi OCHA inasema Israel imekataa kuruhusu asilimia 30 ya operesheni za kibinadamu Gaza Kaskazini na kuathiri kwa kiasi kikubwa operesheni za UNRWA.
Watoto 27 wameripotiwa kufa njaa kutokana na utapiamlo hadi sasa huku shirika la Kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF likionya kwamba Maisha ya maelfu wengine yako hatarini ukizingatia ukweli kwamba tangu Oktoba 7 mwaka jana watoto zaidi ya 13,000 wameuawa kutokana na vita inayoendelea lakini njaa nayo ni tishio kubwa.
Kuhusu uharibifu wa miundombinu uliosababishwa na vita inayoendelea ripoti ya pamoja ya tathimini ya Umoja wa Mataifa na Benk ya Dunia iliyotolewa leo inasema uharibifu huo unakadiriwa kuwa takriban dola bilioni 18.5 ambao ni sawa na asilimia 97 ya pato la taifa la Ukingo wa Magharibi na Gaza kwa mwaka 2022.
Na hapa Makao Makuu leo Umoja wa mataifa umepokea barua rasmi kutoka kwa mamlaka ya Palestina ikiomba kuwa mwanachama kamili wa Umoja wa Mataifa badala ya nafasi ya uangalizi iliyonayo sasa.
Wed, 03 Apr 2024 - 11582 - Bado kazi ipo kupigania haki za mwanamke kote duniani - Paulina Ngurumwa
Kinara wa elimu nchini Tanzania Paulina Ngurumwa anasema bado kazi ipo kupigania haki za mwanamke kwa hiyo harakati hizo hazitakiwi kupoa. Paulina Ngurumwa ni mwanaharakati wa haki za kijamii kupitia shirika la KINNAPA Development Programme.
KINNAPA Development Programme ni shirika lisilo la kiserikali lililoanzishwa na wanajamii ya Wilaya ya Kiteto, Mkoani Manyara, kaskazini mwa Tanzania likiwa ni chombo cha kutatua matatizo yao hasa ya ardhi. Shirika hili lilianzishwa mwaka 1992 na kwa miaka hiyo yote linajivunia kuendelea kufanikisha malengo yake na sasa hata limepanua mawanda ya huduma zake kama anavyoeleza mmoja wa viongozi Paulina Nguruma, katika mahojiano aliyoyafanya na Anold Kayanda wa Idhaa hii hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa.
Tue, 02 Apr 2024 - 11581 - 02 APRILI 2024
- Leo maafisa wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa wamelaani vikali mauaji ya wafanyakazi wa misaada 7 wa shirika lisilo la kiselikali au NGO la World Central Kitchen yaliyofanywa na jeshi la Israel, maafisa hao wakirejea kueleza hofu yao kwamba hakuna mahali palipo salia kuwa salama Gaza.Tume ya pamoja ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa na serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya UNJHRO imesema kumekuwa na ongezeko la asilimia 14 ya visa vya ukiukwaji wa haki za binadamu nchini DRC. Leo ni siku ya kimataifa ya kuelimishana kuhusu usonji maudhui yakiwa kutoka kuishi kuelekea kwenye ustawi, kwa watu wenye usonji au kwa kiingereza Autism, ambapo kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani, WHO, usonji hukumba mtoto mmoja kati ya kila watoto 160 duniani.Na mashinani tunaelekea Gaza kuona ni kwa jinsi gani mashambulizi ya Israel ya hivi majuzi yameathiri huduma za afya katika hospitali ya Al-Shifa.
Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Tue, 02 Apr 2024 - 11580 - Mradi wa maji warejesha matumaini kwa familia Wajir
Maji ni uhai, ni kauli mbiu ya miaka nenda rudi, lakini imesalia ndoto kwa wengi duniani hasa wakati huu mabadiliko ya tabianchi yanachochea ukame unaovuruga maisha ya binadamu, wanyama na mimea. Nchini Kenya katika kaunti ya Wajir, iliyoko kaskazini-mashariki mwa taifa hilo la Afrika Mashariki, uhaba wa maji ulisababisha familia kupoteza mifugo yao, mazao kukauka na ustawi wa jamii kutoweka. Lakini shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, kwa kushirikiana na serikali ya Kaunti walianzisha mradi wa ujenzi wa kuchimba visima wa Giriftu kwa ili jamii iwe na uhakika wa kupata maji wakati wowote. Mradi umezaa matunda na ndio msingi wa makala yetu ya leo inayoletwa na Assumpta Massoi.
Mon, 01 Apr 2024 - 11579 - Griffiths: Jaribio la kuitenga UNRWA lazima likome
Mratibu Mkuu wa Misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura wa Umoja wa Mataifa Martin Griffiths amesema shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA ni uti wa mgongo wa operesheni za Kibinadamu Gaza hivyo jaribio la kulitenga shirika hilo lazima likome.
Bwana Griffiths ametoa kauli hiyo leo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa X zamani Twitter akisistiza kuwa juhudi zozote za kusambaza misaada ya kibindamu kwenye Ukanda wa Gaza bila kupitia shirika la UNRWA haziwezi kufanikiwa na watu zaidi ya milioni 2 wanaitegemea UNRWA ili kuendelea kuishi.
Ameendelea kusema kwamba hadi sasa hakuna shirika lingine lolote lenye uwezo wa kufika kila kona ya Gaza, uzowefu na imani ya jamii ya kutekeleza majukumu yake kama lilivyo shirika la UNRWA.
Wakati huohuo shirika la UNRWA limeonya kwamba mashambulizi ya Israel yameendelea tena usiku wa kuamkia leo huko Gaza Kaskazini Khan Younis na Rafah ambako watu milioni 1.2 wanapata hifadhi na kusababisha vifo zaidi.
Huku lile la afya la Umoja wa Mataifa WHO likisema wakati timu yake ikiwa katika operesheni ya kibinadamu katika hospital ya Al-Aqsa jana Jumapili maeneo ya hospital yalipigwa na shambulio la anga lililokatili maiasha ya watu 4 na kujeruhi wengine 17.
Nalo shirika la mpango wa chakula duniani WFP limesema linajitahidi kwa kila hali kutoa msaada wa chakula unaohitajika sana kwa watu milioni 1.45 Gaza lakini msaada huo hautoshi na bila usitishaji vita hawawezi kumfikia kila mtu na hivyo kufanya Maisha ya watu wengi kusalia hatarini.
Mon, 01 Apr 2024 - 11578 - 01 APRILI 2024
- Mratibu Mkuu wa Misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura wa Umoja wa Mataifa Martin Griffiths amesema shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA ni uti wa mgongo wa operesheni za Kibinadamu Gaza hivyo jaribio la kulitenga shirika hilo lazima likome.Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kituo kilichojengwa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO kimesaidia vijana kukabiliana na habari potofu na za uongo ambazo huchochea ukosefu wa amani kwenye taifa hilo la Maziwa Makuu barani Afrika. Katika makala Assumpta Massoi kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF nchini Kenya, anakupeleka kaunti ya Wajir kuona jinsi mradi wa maji ulivyoleta matumaini kwa familia na jamii.Na mashinani tutaelekea nchini Tanzania kusikia ujumbe kuhusu afya kwa watoto.
Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Mon, 01 Apr 2024 - 11577 - Kituo cha amani DR Congo chakabili habari potofu na za uongo
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kituo kilichojengwa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO kimesaidia vijana kukabiliana na habari potofu na za uongo ambazo huchochea ukosefu wa amani kwenye taifa hilo la Maziwa Makuu barani Afrika.
Jean Claude Batumike, ambaye ni Mkuu wa kituo cha vijana cha Amani, kilichoko eneo la Kamanyola huko jimboni Kivu Kusini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC akizungumza kupitia video ya MONUSCO iliyochapishwa kwenye mtandao wa Instagramanasema kituo hicho kilipojengwa watu walijihisi wako na amani zaidi.
Anasema kituo cha amani kilijengwa kwa ajili ya amani ili kuondoa migogoro kwa vijana na jamii kwa ujumla. Kituo kina kompyuta, mtandao wa intaneti wakati wote na skrini kubwa ambapo katika video hiyo wanaonekana vijana wakipita hapa na pale huku wakipatiwa maelezo na Bwana Batumike.
Akilinganisha hali kabla na baada ya kujengwa kwa kituo hicho, Bwana Batumike anasema, “mara nyingi wakati tulikuwa na mizozo hapa kwenye eneo letu, hakukuweko na mahali ambapo watu wanaweza kwenda na kutatua mizozo, lakini tangu wamejenga hiki kituo cha Amani, kushikakuweko na mzozo wa vijana au jamii, wanakimbilia kituo cha Amani, wanakaa pamoja na kutatua mizozo na hatimaye mambo yanakuwa mazuri zaidi.”
Bwana Batumike akaelezea kuwa kituo cha Amani kinasaidia kukabili habari za uongo na potofu kwa kuwa kituo kina mtandao wa uhakika wa intaneti, kompyuta na skrini na wanaweza kupata habar iza ukweli.
“Mara nyingi vijana wanapokuwa na habari za wasiwasi ambazo hawana uhakika nazo ni rahisi kufika kituo cha Amani, wanajiunganisha kwenye intaneti, wanarambaza na kusogoa na wengine kwa mtandao na kupata habari za ukweli. Na katika sehemu yenye mzozo, unahitaji kupata habari za uhakika,” anasema Bwana Batumike.
Mon, 01 Apr 2024 - 11576 - Kituo cha malezi ya watoto nchini Kenya chatekeleza azma ya Umoja wa Mataifa
Mkutano wa 68 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW68 ulifunga pazia hivi majuzi jijini New York Marekani ukipigia chepuo uwekezaji kwa wanawake na wasichana, na leo tunabisha hodi nchini Kenya wasichana waliokumbwa na ujauzito utotoni na kukatishwa ndoto za kuendelea na masomo au kupata ajira wamepata jawabu la changamoto wanazokumbana nazo pindi wakijifungua watoto wao. Changamoto kama vile mahali pa kumwacha mtoto kwa malezi ili aweze kuendelea na shule au kupata ajira.
Umoja wa Mataifa unasema kila mtu ana haki ya elimu hata kama amepata changamoto gani maishani. Na ndipo ushirikiano kati ya mashirika ya kiraia lile la “Work for life”, pamoja na lile la “A Pack a Month”, linalohusika na utoaji wa misaada mbali mbali ikiwemo taulo za kike kwa wazazi wenye mahitaji na wasichana wanaokwenda shule walizindua kituo cha malezi ya watoto wachanga nyakati za mchana katika eneo la Ngong nchini Kenya. Mradi unaungwa mkono na wadau kadhaa ikiwemo serikali ya Kenya. Selina Jerobon ni msimulizi wetu kupitia mada hii iliyofanikishwa na Redio washirika DOMUS ya huko Kenya.
Thu, 28 Mar 2024 - 11575 - Jifunze Kiswahili: Ufafanuzi wa neno “UDENDA”Thu, 28 Mar 2024
- 11574 - 28 MACHI 2024
- Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina (UNRWA) leo Machi 28 limetahadharisha kuhusu ujio wa baa la njaa katika Ukanda wa Gaza. UNRWA imesema yenyewe ni uti wa mgongo wa misaada ya kibinadamu Gaza lakini bado misafara yao ya chakula imezuiwa kufika kaskazini, ambako baa la njaa linajongea. Wakati huo huo Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) limesema kati ya hospitali 36 katika Ukanda wa Gaza, ni 10 tu ambazo zimesalia zikifanya kazi japo nazo kwa kiasi kidogo.Ripoti ya Ofisi ya Haki za Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa iliyochapishwa leo inataka hatua za haraka na za ujasiri ili kukabiliana na hali ya "janga" nchini Haiti. Ripoti imeeleza kuwa magenge yanaendelea kutumia unyanyasaji wa kingono kuwatendea unyama, kuwaadhibu na kuwadhibiti watu. Wanawake wamebakwa hata baada ya kushuhudia waume zao wakiuawa mbele yao. Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), pamoja na wadau wake 123, Alhamis ya leo limetangaza kuwa linatafuta dola bilioni 1.4 mwaka huu ili kukidhi mahitaji ya wakimbizi milioni 2.3 wa Sudan Kusini wanaoishi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Ethiopia, Kenya, Sudan na Uganda. Janga la wakimbizi wa Sudan Kusini linasalia kuwa ndilo kubwa zaidi barani Afrika.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno “UDENDA”.
Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Thu, 28 Mar 2024 - 11573 - Simulizi za raia wanaokimbia mashambulizi kaskazini mwa MsumbijiWed, 27 Mar 2024
- 11572 - Innoss B kushirikiana na WFP kusongesha lishe na elimu DRC
Mwanamuziki Innocent Balume, al maaruf Innoss’B ametangazwa kuwa muungaji mkono wa ngazi ya juu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP katika kusongesha milo yenye afya na lishe bora nchini mwake Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.
Nimeshuhudia njaa mara nyingi sana wakati wa utoto wangu, kabla ya kwenda shule tulikuwa na njaa na kabla ya kulala tulikuwa na njaa, ndivyo asemavyo mwanamuziki Innocent Balume, al maaruf Innoss’B ambaye ametangazwa kuwa muungaji mkono wa ngazi ya juu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP katika kusongesha milo yenye afya na lishe bora nchini mwake Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Taarifa ya WFP iliyotolewa Kinshasa, mji mkuu wa DRC imemnukuu Mkurugenzi Mtendaji wa WFP Cindy McCain akisema “ninafurahia sana kumkaribisha kwenye timu yetu ya WFP, tukiwa na Innos tutaweza kuwa na athari chanya kwenye vita dhidi ya njaa na utapiamlo DRC.”
Innos amenukuliwa akisema njaa ilikuwa sehemu ya maisha yake wakati akiwa mtoto na kwamba “kila siku unalazimika kufirikia leo nitakula vipi? Nitapataje chakula hii leo? Hakukuwa na matumaini.”
Sasa mwanamuziki huyu aliyejipatia umaarufu sio tu nchini mwake bali pia Afrika na dunia nzima kutokana na mitindo yake ya AfroBeat na Rumba amepatiwa jukumu na WFP kutumia muziki wake kuelimisha jamii umuhimu wa lishe bora na elimu nchini mwake DRC.
Innos ambaye ni mzaliwa wa Goma, mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini, mashariki mwa DRC, anasema njaa ilikuwa kichocheo cha muziki na hivyo aliona ana deni kwa jamii yake ya kusaidia kuongeza uelewa na hamasa kuhusu tatizo hilo.
Kupitia video ya WFP Innoss’B akiwa kwenye moja ya mashamba ya mboga za majani nchini DRC, akiambatana na wanawake na kwingine akiwa na wanafunzi anasema, “leo nina furaha kwa sababu kwa mara moja nina fursa ya kuwa karibu na jambo ambalo linanigusa mno. Kuhakikisha kila mtu ana afya njema . Kuhakikisha kila mtu ana nguvu, kuhakikisha kila mtu anaweza kupata chakula. Ujumbe huo utasikika . Hivyo niña furaha sana, hii itakuwa ni safari nzuri. Nina furaha.”
Mkurugenzi Mtendaji wa WFP, ambaye kwa mara ya kwanza alikutana na Innoss’B mjini Goma, miaka 14 iliyopita, wakati huo Innoss akiwa na umri wa miaka 13, amesema amekuwa anajivunia sana kuona kila kitu alichofanikiwa kama msanii na msongeshaji wa utu wa kibinadamu.
Amesema kujituma kwake katika kujenga mustakabali bora kwa wananchi wa DRC ni hamasa ya dhati.
Innos anasema anaamini kwenye nguvu ya muziki na utamaduni katika kuleta mabadiliko chanya. Kushirikiana na WFP kunaniruhusu kuchangia katika kutatua masuala nyeti ya lishe na elimu nchini mwangu. Kwa pamoja tunaweza kuleta mabadiliko yenye maana kwa maisha ya vijana.”
Peter Musoko ambaye ni Mwakilishi Mkazi wa WFP nchini DRC anasema wanafuraha kubwa kushirikiana na Innos’B na kutumia nguvu ya muziki kusongesha ustawi wa DRC na wananchi wake. “Kwa kuunganisha nguvu, tunaweza kuchochea hatua chanya na kutatua changamoto kubwa ya utapiamlo na ukosefu wa uhakika wa chakula.”
Wakati huu ambapo WFP inaendelea na jitihada za kuimarisha uhakika wa kupata chakula DRC, ushirikiano na Innoss’B unaongeza sauti muhimu katika kampeni hiyo.
Hata hivyo WFP inasema ukata ni tatizo kwa sasa kwani bajeti yake kwa DRC ina pengo la dola milioni 548.5, fedha ambazo zinahitajika kwa kipindi cha miezi sita ijayo kuweza kukidhi mahitaji ya kiutu yanayoongezeka kila uchao.
Wed, 27 Mar 2024 - 11571 - 27 MACHI 2024
- Juhudi na ushirikiano wa pamoja wa wahudumu wa afya, vituo na Jamii, vimefanikisha kukomesha mlipuko wa kipindupindu uliozuka nchini Zambia kwa mujibu wa Shirika Umoja wa Mataifa la Afya Duniani WHO nchini Zambia, ambalo limeeleza kwamba ugunduzi wa mapema na matibabu husaidia kukabiliana na ugonjwa huo na kupunguza idadi ya vifo.Mwanamuziki Innocent Balume, al maaruf Innoss’B ametangazwa kuwa muungaji mkono wa ngazi ya juu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP katika kusongesha milo yenye afya na lishe bora nchini mwake Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC. Makala tunaangazia mgogoro ambao hauripotiwi sana kaskazini mwa Msumbiji umesababisha mamia kwa maelfu ya familia kuwa wakimbizi, ambao wanaendelea kutatizika kutafuta chakula, malazi na usalama.Na mashinani tutaelekea nchini Jamhuri ya Kidemocrasia ya Congo DRC kusikia ujumbe wa mlinda amani wa kuhusu elimu kwa wasichana.
Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Wed, 27 Mar 2024 - 11570 - WHO Zambia yashirikiana na Serikali kutokomeza Kipindupindu
Juhudi na ushirikiano wa pamoja wa wahudumu wa afya, vituo na Jamii, vimefanikisha kukomesha mlipuko wa kipindupindu uliozuka nchini Zambia kwa mujibu wa Shirika Umoja wa Mataifa la Afya Duniani WHO nchini Zambia, ambalo limeeleza kwamba ugunduzi wa mapema na matibabu husaidia kukabiliana na ugonjwa huo na kupunguza idadi ya vifo.
Jioni moja Philta Samazimva alilalamika ghafla tumbo kuuma, baada ya kuharisha sana, mama yake mzazi Hildar Samazimba alimpeleka kliniki.
Baadhi ya watu hapa walisema usiende hospitali mtoto atapona, hakuna kitu watakachompatia mtoto na atakufa. Lakini nilipoona jinsi mtoto wangu alivyokuwa anaonekana, nilisema wacha niwahi kliniki.
Philta alipelekwa kwenye kituo cha matibabu cha Heroes Cholera, ambapo alipata ahueni baada ya matibabu. Dr Mavis Chisala, Ni Daktari wa magonjwa ya watoto katika kituo cha kutibu kipindupindu cha Mashujaa.
"Tumekuwa tukihakikisha tunamfuatilia mgonjwa wetu, kwa sababu kwa watoto wanaimarika haraka sana unapochukua hatua sahihi kwa wakati muafaka.
Kiwango cha vifo vya wagonjwa wa kipindupindu katika vituo vya afya ni asilimia 1.3, ikilinganishwa na asilimia 3.3 kwa ujumla, kutokana na kazi inayofanywa na matabibu hao kwa ushirikiano na WHO ambao umerejesha matumaini kwa Samazimba
“ kikubwa tulifanya kazi kwa ushirikiano, ninawashukuru Wauguzi, matabibu kwa kazi waliyoifanya, kwasababu sikujua kama mtoto wangu atapona
WHO imeisaidia wizara ya afya nchini Zambia kurekebisha miongozo ya huduma za kliniki na kununua vifaa tiba na vifaa vingine kwa ajili ya kukabiliana na mlipuko wa kipindupindu. Dkt. Kalima Nawa, kiongozi mkuu wa kituo cha matibabu cha mashujaa wa kipindupindu anasema Hold under……03 sec “tunatarajia kuendelea kufanya kazi na WHO katika mlipuko huu, na pia kupanga kwa ajili ya milipuko ya baadaye na kutusaidia kujiandaa kwa hayo”.
Kipindupindu kinatibika kwa urahisi iwapo kitagunduliwa kwa wakati.
Wed, 27 Mar 2024 - 11569 - 26 MACHI 2024
- Ripoti ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Hatua Maalum za Ulinzi dhidi ya Unyonyaji na Unyanyasaji wa Kingono imewekwa wazi hii leo.Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi (UNHCR) limetoa wito wa kuchukuliwa hatua za haraka kutokana na ongezeko la hatari kwa watu waliokimbia makazi yao mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Na wakati mradi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) unaohusu Wahamiaji Wasiofahamika waliko ukitimiza miaka kumi, ripoti mpya ya shirika hilo iliyopewa jina ‘Muongo mmoja wa kukusanya taarifa za vifo vya wahamiaji’ inaonesha mienendo ya kutisha ya vifo na kupotea kwa wahamiaji katika muongo mmoja uliopita na kwamba mtu mmoja kati ya watatu hufariki duniani katika harakati za kukimbia migogoro katika nchi yake.Katika mashinani tunakuletea ujumbe wa Mhandisi Denis Arbogast, Msimamizi wa mradi wa maji Kasulu mkoani Kigoma nchini Tanzania, mradi inayofadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na wadau wake.
Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Tue, 26 Mar 2024 - 11568 - Nyumba salama kwa waathirika wa unyanyasaji wa kingono Sudan Kusini
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS kwakushirikiana na wadau wake wamefungua nyumba salama huko Andari Magharibi katika jimbo la Equatoria kwa ajili ya kusaidia manusura wa unyanyasaji wa kingono unaohusiana na migogoro nchini humo. Leah Mushi na maelezo zaidi.
Kwa mujibu wa Mkuu wa zamani wa UNMISS ofisi ya Yambio, Christopher Muchiri Murenga, mradi huu ulioanzishwa na kitengo cha ushauri cha ulinzi wa wanawake cha UNMISS na umefadhiliwa na Muungano wa Ulaya pamoja na Shirika la Rural Action Aid lengo likiwa ni kuwasaidia waathirika wa unyanyasji wa kijinsia unaohusiana na migogoro.
Bwana Murenga anasema,“kama sehemu ya kutafuta amani ya kudumu na jumuishi nchini Sudan Kusini, imebidi tuwalete manusura pamoja ili waweze kuponya majeraha yao. Kisha watakuwa wanajamii wenye tija, wakichangia ustawi wa kijamii na kiuchumi wa serikali.”
Kituo hiki kinatoa ushauri nasaha, kuponya watu wenye kiwewe pamoja na mafunzo ya stadi za maisha na kinalenga kusaidia manusura 195. Mmoja wa wanufaika ni Azande ambaye katika video ya UNMISS amefichwa sura yake wakati akieleza masahibu aliyopitia akisema, “tulipotoka porini nilikuwa na kiwewe, walitupa ushauri nasaha na mawazo yote mabaya yaliyokuwa akilini mwangu yaliondoka na sasa niko thabiti zaidi. Mimi ni miongoni mwa wale ambao sasa wanajifunza ushonaji. Wakati nipo msituni nilijifungua mtoto wa kike sasa ana umri wa miaka 6. Ana matatizo ya tumbo kwa sababu wakati mjamzito nilikuwa nakula vitu vya hatari ndio maana sasa naomba msaada wa dawa kwa ajili yake.”
Kiongozi wa kikundi cha wanawake katika eneo la Ezo Henrica Elias anasema nyumba hii itasaidia wasichana na wanawake wengi sana kwa kuwa, “kituo hiki ni kama ndoto inayotimia, imetuletea furaha ambayo hatuwezi kuieleza. Yaliyotusibu sisi wanawake na wasichana wakati wa mzozo ni yakutisha. Mambo mengi mabaya yalitendeka katika vijiji vyetu, ambapo wasichana wadogo na wavulana pia walitekwa nyara.”
Migogoro nchini Sudan Kusini imesababisha tajriba ya kuhuzunisha kwa vijana wengi wa kike na wa kiume, hasa wale ambao walilazimika kujiunga na makundi yenye silaha nchini humo.
Mon, 25 Mar 2024 - 11567 - Guterres: Tekelezeni kikamilifu mkataba wa mwaka 1994 wa kuwalinda wafanyakazi wa UN
Ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Mshikamano na Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa Walio vizuizini na wasiofahamika waliko, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito kwa ulimwengu kuenzi ujasiri na kujitolea kwa wafanyakazi wanaotoa huduma za kibinadamu kila mahali kokote waliko kwa kuahidi kuwalinda na kuwaunga mkono wanaposaidia kujenga dunia yenye amani zaidi na ya utu kwa ajili ya watu wote. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.
Siku hii ya Kimataifa ya Mshikamano na Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa Walio vizuizini na wasiofahamika waliko huadhimishwa kila mwaka Machi 25 katika kumbukumbu ya kutekwa nyara kwa Alec Collett, mwandishi wa habari wa zamani ambaye alikuwa akifanya kazi katika Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) wakati alipotekwa nyara na mtu aliyekuwa na silaha mwaka wa 1985 na baadaye mwili wake kupatikana katika Bonde la Bekaa nchini Lebanon mwaka wa 2009 yaani miaka 24 baadaye.
Maadhimisho ya siku hii, katika miaka ya hivi karibuni yamekuwa hata ana umuhimu mkubwa zaidi kutokana na kuongezeka kwa mashambulizi dhidi ya Umoja wa Mataifa.
Katibu Mkuu Guterres kupitia ujumbe wake kwa maadhimisho ya mwaka huu anatoa takwimu za hivi karibuni akieleza kwamba tangu mwaka juzi 2022, wafanyakazi 381 wa Umoja wa Mataifa wamewekwa kizuizini ikiwa ni pamoja na wafanyakazi 7 mnamo mwezi Januari na Februari mwaka huu 2024. Kwa jumla, wafanyakazi 27 wa Umoja wa Mataifa bado wako kizuizini.
Bwana Guterres anasema leo ni ukumbusho mzito wa hatari kubwa zinazowakabili wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa wanapofanya kazi yao muhimu chini ya bendera ya Umoja wa Mataifa na kwamba, "Mioyo yetu iko pamoja na familia zao na wafanyakazi wenzao”, na kwamba hatakataa tamaa kutaka waachiliwe na kurudi salama."
Kiongozi huyo wa Umoja wa Mataifa anazisihi nchi zote kutekeleza kikamilifu Mkataba wa mwaka 1994 wa Usalama wa Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa na Washirika wao, na pia Itifaki ya Hiari ya mwaka 2005 ya Mkataba huo.
Mon, 25 Mar 2024 - 11566 - 25 MACHI 2024
Hii leo jaridani mwenyeji wako ni Anold Kayanda akianzia na siku ya kimataifa ya kukumbuka watumishi wa UN wanaoshikiliwa vizuizini na wasiofahamika waliko, kisha anakwenda Sudan Kusini na harakati za kusaidia manusura wa ukatili wa kingono. Makala ni harakati za kumkomboa mwanamke na mashinani arejea Sudan Kusini.
- Ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Mshikamano na Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa Walio vizuizini na wasiofahamika waliko, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito kwa ulimwengu kuenzi ujasiri na kujitolea kwa wafanyakazi wanaotoa huduma za kibinadamu kila mahali kokote waliko kwa kuahidi kuwalinda na kuwaunga mkono wanaposaidia kujenga dunia yenye amani zaidi na ya utu kwa ajili ya watu wote. Assumpta Massoi anaeleza zaidi.Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS kwakushirikiana na wadau wake wamefungua nyumba salama huko Andari Magharibi katika jimbo la Equatoria kwa ajili ya kusaidia manusura wa unyanyasaji wa kingono unaohusiana na migogoro nchini humo. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi.Makala leo inatupeleka Nairobi Kenya ambako mkutano wa maandalizi wa asasi za kiraia umekunja jamvi hivi karibuni na Stella Vuzo wa kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa nchini Kenya UNIS Nairobi alizungumza na Carole Osero-Ageng'o Mwenyekiti mwenza wa mkutano huo. Anazungumzia harakati za kumkomboa mwanamke.Mashinani ni mlinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini kutoka taifa la Bhutan.
Mon, 25 Mar 2024 - 11565 - Maji yanaweza kuleta amani au kuchochea migogoro
Ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Maji, Kevin Keitany wa redio washirika wetu Domus FM ya nchini Kenya amezungumza na baadhi ya wakazi wa Kaunti ya Kajiado nchini humo kuhusu umuhimu wa uwepo wa maeneo mengi ya kupata maji katika jamii. Dhima ya Siku ya Kimataifa ya Maji ya mwaka huu wa 2024 ni "Maji kwa ajili ya amani" ikieleza kuwa kunapokuwa na ushirikiano katika suala la maji inaleta athari chanya kukuza maelewano, kuhamasisha ustawi na kujenga uwezo wa kukabiliana na changamoto za pamoja.
Fri, 22 Mar 2024 - 11564 - 22 MACHI 2024
Hii leo jaridani ikiwa ni Siku ya maji duniani, tunaangazia utunzaji wa vyanzo vya maji. Pia tunamulika mkutano wa Kamisheni ya hali ya wanawake duniani, CSW68 ambao umekunja jamvi hii leo. Makala tuankupeleka nchini Kenya na mashinani nchini Tanzania kufuatilia jinsi ambayo miradi ya maji inavyoleta manufaa kwa jamii.
- Leo ni siku ya maji duniani chini ya kauli mbiu Maji kwa amani ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake kwa siku hii amehimiza nchi kuhakikisha zinashirikiana na kuwa na makubaliano ya kutumia vyanzo vya maji.Mkutano wa 68 wa Kamisheni ya hali ya wanawake duniani, CSW68 umekunja jamvi hii leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataia jijini New York, Marekani na miongoni mwa washiriki ni Matika Maiseli, Meneja wa Rasilimali Watu na Utawala kutoka Mamlaka ya Afya na Mimea na Viuatilifu, TPHPA iliyo chini ya Wizara ya Kilimo nchini Tanzania. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema ubaguzi wa rangi ni jinamizi linaloathiri nchi na jamii kote duniani chimbuko lake likitokana na sera za ukoloni na utumwa. Kupitia ujumbe wake wa siku ya kimataifa ya kutokomeza ubaguzi wa rangi hii leo inayojikita na mada ya watu wenye asili ya Afrika katika kutambuliwa kwao, kupewa haki na maendeleo, ametaka kutokomezwa kwa jinamizi hilo kwani linapokonya fursa, kunyima utu, kukiuka haki, kupora maisha na pia kuyaharibu.Katika mashinani tutakupeleka nchini Tanzania kusikia ujumbe kuhusu jinsi ambavyo miradi ya maji imeleta nafuu kwa jamii.
Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Fri, 22 Mar 2024 - 11563 - Tunawezesha wakulima wanawake Tanzania ili wapate masoko ndani na nje ya nchi - Matika Maiseli, TPHPA
Mkutano wa 68 wa Kamisheni ya hali ya wanawake duniani, CSW68 umekunja jamvi hii leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataia jijini New York, Marekani na miongoni mwa washiriki ni Matika Maiseli, Meneja wa Rasilimali Watu na Utawala kutoka Mamlaka ya Afya na Mimea na Viuatilifu, TPHPA iliyo chini ya Wizara ya Kilimo nchini Tanzania.
Assumpta Massoi wa Idhaa hii ya Umoja wa Mataifa amezungumza naye kufahamu ni nini anaondoka nacho kutoka mkutano huu uliolenga kusongesha usawa wa kijinsia, uwezeshaji wanawake na kutokomeza umaskini.
Fri, 22 Mar 2024 - 11562 - Umoja wa Mataifa yataka nchi kuwa na makubaliano ya ushirikiano wa matumizi ya vyanzo vya maji
Leo ni siku ya maji duniani chini ya kauli mbiu Maji kwa amani ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake kwa siku hii amehimiza nchi kuhakikisha zinashirikiana na kuwa na makubaliano ya kutumia vyanzo vya maji.
Katika ujumbe wake huo Guterres ameeleza kuwa mpaka sasa ulimwenguni “Nchi 153 zinashirikiana vyanzo vya maji lakini ni nchi 24 pekee zenye makubaliano kwa vyanzo vyao vyote vya maji wanavyoshirikiana.”
Amesema hali haipaswi kuwa hivyo na nchi zinatakiwa “kutekeleza Mkataba wa Maji wa Umoja wa Mataifa ambao lengo lake ni kuhamasisha usimamizi wa rasilimali za maji za pamoja kwa njia endelevu.”
Hii leo kukiwa na mikutano mbalimbali pamoja na ripoti za mashirika ya Umoja wa Mataifa, kimataifa, kitaifa na asasi za kiraia zinazoelezea matumizi ya maji pamoja na changamoto zake ulimwenguni, Mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa ametaka watu wote kutambua kwamba kushirikiana katika kulinda vyanzo vya maji kunaweza kuimarisha na kudumisha amani.
Kama Kauli mbiu ya mwaka huu inavyosema “Maji kwa amani” Guterres amesema “Hatua zinachokuliwa kwa ajili ya maji ni hatua kwa ajili ya amani na hii inahitajika zaidi kuliko wakati mwingine wowote. Usimamizi wa maji unaweza kuimarisha ushirikiano wa kimataifa na uhusiano kati ya jamii, na kujenga uwezo wa kukabiliana na majanga yaletwayo na mabadiliko ya tabianchi. Unaweza pia kuendeleza maendeleo kuelekea Malengo ya Maendeleo Endelevu SDGs ambayo ni msingi wa jamii zenye amani, ikiwa ni pamoja na kuboresha afya, kupunguza umaskini na ukosefu wa usawa, na kuimarisha usalama wa chakula na maji.
Amehitimisha kwa kutoa wito kwa jamii yote kujitolea kufanya kazi pamoja, kufanya maji kuwa nguvu ya ushirikiano, maelewano na utulivu, na hivyo kusaidia kuunda ulimwengu wa amani na ustawi kwa wote.
Fri, 22 Mar 2024 - 11561 - Jifunze Kiswahili: Ufafanuzi wa neno "Panda"Thu, 21 Mar 2024
- 11560 - 21 MACHI 2024
- Wakati hali ya kibinadamu ikiendelea kuwa mbayá Gaza mashirika ya Umoja wa Mataifa likiwemo lile la afya duniani WHO yamerejea wito wa kutaka kusitishwa mapigano mara moja na kuhakikisha misaada ya kibinadamu inaingia Gaza ambako maisha ya zaidi ya watu milioni 1 yako hatarini kwa njaa..Leo ni siku ya kimataifa ya ugonjwa unaoathiri uwezo wa mtu kujifunza au downsyndrome mwaka huu ikibeba maudhui ya kutokomeza unyanyapaa yakimchagiza kila mtukuwajumuisha watu wenye downsyndrome kwenye nyanja zote za maisha na kutowabagua. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema ubaguzi wa rangi ni jinamizi linaloathiri nchi na jamii kote duniani chimbuko lake likitokana na sera za ukoloni na utumwa. Kupitia ujumbe wake wa siku ya kimataifa ya kutokomeza ubaguzi wa rangi hii leo inayojikita na mada ya watu wenye asili ya Afrika katika kutambuliwa kwao, kupewa haki na maendeleo, ametaka kutokomezwa kwa jinamizi hilo kwani linapokonya fursa, kunyima utu, kukiuka haki, kupora maisha na pia kuyaharibu.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili mtaalam wetu leo ni Nicholus Makanji mhadhiri katika chuo Kikuu cha Zetech Limuru Kenya akitufafanulia maana ya neno “PANDA”
Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Thu, 21 Mar 2024 - 11559 - Watoto Gaza waamua vita isiwe sababu ya kunyong’onyea wakati huu wa mwezi mtukufu wa Ramadhani
Huko Ukanda wa Gaza, vita inayoendelea tangu Oktoba 7 mwaka 2023 baada ya Hamas kurusha makombora Israel na kisha Israel kuamua kujibu mashambulizi licha ya kusababisha vifo vya watu 31,000 wengi wao wakiwa wanawake na watoto, watoto waliosalia wameona mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani usipite hivi hivi. Wakiwa katika kambi ya wakimbizi wa ndani ya Deir El Balah katikati mwa Gaza, watoto hao wameona furaha ni bora kuliko machungu ya njaa, ukimbizi, ukosefu wa huduma muhimu za kijamii unaowakabili. Mwandishi wa Idhaa ya Kiarabu ya Umoja wa Mataifa huko Gaza, Ziad Talib amefika hapo ili kufahamu hasa msingi wa hatua ya watoto hao na ndio makala ya leo inayosimuliwa na Assumpta Massoi.
Wed, 20 Mar 2024 - 11558 - WHO: Madaktari Gaza wanafanyakazi kutwa kucha kuokoa maisha bila kutia chochote tumboni
Wahudumu wa afya Gaza wanafanya kazi mchana kutwa na usiku kucha wakihaha kuokoa Maisha ya wagonjwa na majeruhi katika hospitali chache zilizosalia zikifanyakazi bila kutia chochote tumboni kwa mujibu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO.
WHO inasema wafanyakazi hao wanaolazimika kufanyakazi saa 24 kuokoa maisha ya watu kama ambavyo wanakosa vifaa muhimu na vitendeakazi vingine vivyo hivyo wanakosa chakula cha kutosha kama ilivyo kwa maelfu mengine ya raia wa Gaza.
Timu ya WHO iliyozuru Hospitali ya Al-Aqsa katikati mwa Ukanda wa Gaza ili kupeleka vifaa muhimu imezungumza na wafanyakazi kuhusu hali zao, ikiwa ni pamoja na hali yao ya lishe.
Bashar Abdelkader, ambaye ni daktari wa kujitolea katika hospitali hiyo, amesema madaktari wanapewa chakula lakini wanakosa viambato muhimu vya lishe, hasa mchele na mboga nichache.
Ameongeza kuwa mlo mmoja unaweza kugawiwa kwa watu wawili na zaidi ya yote,chakula haitoshi kwa daktari wa zamu wanofanyakazi kwa saa 24 hospitalini hapo.
Tahani al-Samra, ambaye pia ni daktari wa kujitolea katika hospitali ya al-Aqsa amesema "Tunakabiliwa na utapiamlo na ukosefu wa nyenzo tunazohitaji. Kwa sasa hakuna mboga za asili za majani, matunda au virutubisho vingine muhimu. Tunategemea vyakula vya makopo, ambavo bei yake inapanda kwa kasi."
WHO na washirika wake wanafanya operesheni ya hatari kubwa wakihaha kupeleka dawa, mafuta na chakula kwa wahudumu wa afya na wagonjwa.
Lakini maombi ya ufikishaji wa bidhaa mara nyingi hukataliwa au kutatizwa. Uharibifu wa barabara na mapigano yanayoendelea, ikiwa ni pamoja na ndani na karibu na hospitali, pia yanatatiza utoaji wa misaada.
WHO imeonya kwamba bila kuwepo hatua kubwa na za haraka za utoaji wa chakula, maji na vifaa vya msingi, hali ya Gaza, ambako njaa inaathiri karibu watu wote, karibu familia zote zinalazimika kuruka mlo kila siku na watu wazima wanapunguza kiwango cha ulaji wao wa kula.
Nusu ya watu wote ambao ni watu milioni 1.1 huko Gaza, wamechoka kabisa na hakuna usambazaji wa chakula na uwezo wao wa kukabiliana na njaa mbaya ni mdogo.
Umoja wa Mataifa unasema “Hii ndiyo idadi kubwa zaidi kuwahi kurekodiwa katika orodha ya watu wanaokabiliwa na njaa kali Gaza.”
Wed, 20 Mar 2024 - 11557 - 20 MACHI 2024
Hii leo jaridani tunaangazia hali ya huduma za afya katika ukanda wa Gaza, na harakati za chanjo kwa watoto nchini Yemen. Makala tunasalia huko huko Gaza na mashinani inatupeleka nchini Tanzania kusikia ujumbe kuhusu siku ya furaha duniani.
- Wahudumu wa afya Gaza wanafanya kazi mchana kutwa na usiku kucha wakihaha kuokoa Maisha ya wagonjwa na majeruhi katika hospitali chache zilizosalia zikifanyakazi bila kutia chochote tumboni kwa mujibu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO.Katika kuhakikisha watoto wanapata chanjo zote zinazohitajika, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF nchini Yemen limekuja na mbinu ya kutumia watoto kuhamasisha jamii kupeleka watoto kupata chanjo. Makala inatupeleka Gaza huko Mashariki ya Kati kupata taswira tofauti na ile ambayo imezoeleka kwa takribani miezi sita sasa. Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi katika makala hii iliyoandaliwa na Ziad Talib, mwandishi wa Habari wa Idhaa ya Kiarabu ya Umoja wa Mataifa huko Gaza.Katika mashinani ikiwa leo ni siku ya furaha duniani Sabrina Moshi wa redio washirika SAUT FM ya mkoani mwanza kaskazini magharibi mwa Tanzania ameuliza wananchi furaha ina maana gani kwao.
Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Wed, 20 Mar 2024 - 11556 - UNICEF yatumia watoto kuhamasisha jamii kupata chanjo nchini Yemen
Katika kuhakikisha watoto wanapata chanjo zote zinazohitajika, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF nchini Yemen limekuja na mbinu ya kutumia watoto kuhamasisha jamii kupeleka watoto kupata chanjo.
Mtoto Leen mwenye umri wa miaka 10 kutoka nchini Yemen, anasema kupitia mpango wa ufadhili wa mtoto, programu inayotumia watoto kwenda kuhamasisha jamii kupata chanjo ili wawe na afya bora amefanikisha watoto 150 kupata chanjo katika jamii yake.
Akieleza hasa jumuku lake Leen anasema ‘Nawasisitiza walezi, umuhimu wa kupata chanjo na pia nacheza na watoto pale wanapokuwa wanachomwa sindano za chanjo ili kuwafanya wajisikie vizuri”
Katika kipindi cha miaka mwili UNICEF imefanikiwa kuwapatia mafunzo watoto 1000 ambao kwa pamoja wamefanikiwa kushawishi watoto 33,000 kupatiwa chanjo.
Watoto hao kama Leen huambatana na mtu mzima ambaye ni muhamasishaji wa jamii kwenda kuhamasisha familia kuhusu chanjo za kawaida ambazo watoto wanapaswa kupata.
Mmoja wa waliohamasishwa na mtoto Leen ni Somaia Mohammed, mama wa watoto watatu.
“Nilikuwa najizuia kwenda kuwapatia chanjo watoto wangu, hata hivyo baada ya Leen kunitembelea nyumbani kwangu baada ya mtoto wangu kuugua surau na kunielezea kama ningekuwa nimewapatia chanjo watoto wangu wasingeugua kiasi hicho nilihamasika na ushauri wao na kutembelea kituo cha afya kuwapatia chanjo watoto wangu.”
Na mtoto Leen anafurahi kuona jirani yake Somaia na watoto wake watatu wamepata chanjo baada ya kumtembelea mara kadhaa.
Anasema kati ya mambo aliyokuwa akimwambie wakati akienda kumhamasisha alikuwa akisema “Angalia nilivyo na afya bora na nilivyo na nguvu naweza kwenda shuleni sababu nimepata chanjo zote zinazohitajika”
Wed, 20 Mar 2024 - 11555 - 19 MACHI 2024
- Mashirika Umoja wa Mataifa yanayotoa msaada wa kibinadamu huko Gaza hii leo yamesisitiza azma yao ya kusaidia wakazi wa eneo hilo ambako watoto walio hatarini kufa kutokana na njaa kali iliyosababishwa na miezi mitano ya mashambulizi ya Israel na kushindwa kufikishiwa misaada inazidi kuongezeka.Mwaka 2023 ulikuwa mwaka wenye joto zaidi duniani katika rekodi zote zilizowahi kunukuliwa, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la hali ya hewa duniani, WMO katika ripoti yake iliyotolewa hii leo huko Geneva, Uswisi, rekodi za viwango vya joto ardhini, baharini zikivunjwa, barafu na theluji ncha ya kusini zaidi mwa dunia navyo vikiyeyuka. Na ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kazi duniani, ILO inaonesha kitendo cha sekta binafsi kutumikisha watu huzalishafaida isiyo halali yad ola bilioni 236 kwa mwaka ikiwa ni ongezeko la asilimia 37 tangu mwaka 2014.Katika mashinani tutaelekea katika ukanda wa Gaza ambapo kulingana na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, katika mwezi mmoja utapiamlo uliokithiri umeongezeka maradufu kaskazini mwa ukanda huo..
Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Tue, 19 Mar 2024 - 11554 - LANDESA yaelezea ni vipi ushiriki wao CSW68 unaleta nuru kwa wanawake Tanzania
Mkutano wa 68 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW68 ukiendelea hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa imeendelea kuzungumza na washiriki ili kufahamu yale wanayofanya kutekeleza maudhui ya kipaumbele ya mwaka huu ya kumwezesha mwanamke na mtoto wa kike ili hatimaye kupunguza umaskini na kuimarisha usawa wa kijinsia. Shirika la kiraia la kutetea haki ya ardhi kwa wanawake, LENDESA tawi la Tanzania linaloungwa mkono na shirika la Umoja wa Mataifa la kushughulikia masuala ya wanawake ni miongoni mwa washiriki ambapo Assumpta Massoi wa Idhaa hii amezungumza na Khadija Mrisho, anayeongoza kampeni ya kimataifa ya Linda Ardhi ya Mwanamke au Stand For Her Land. Khadija anaanza na kile kilichowaleta.
Mon, 18 Mar 2024 - 11553 - FAO: Baa la njaa lanyemelea Gaza
Hali ya uhakika wa kupata chakula huko Gaza, ni tete na baa la njaa linanyemelea kwenye majimbo ya kaskazini mwa eneo hilo imesema ripoti mpya ya hali ya chakula Gaza iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO, likisema jawabu la kuondokana na hali hiyo ni amani.
Rein Paulsen, Mkurugenzi wa Ofisi ya Masuala ya Dharura na Mnepo FAO akizungumza hii leo huko Roma, Italia wakati wa kutolewa kwa ripoti hiyo ya uchambuzi wa viwango vya uhakika wa kupata chakula au IPC kwa Ukanda wa Gaza, anasema takwimu zinajenga taswira ya hali ya kutia wasiwasi mkubwa. Na pindi tunapofikiria kuhusu Gaza Kaskazini, ambako hali ni mbaya zaidi, uchambuzi wa sasa unatuonesha kuwa njaa ni dhahiri katika kipindi cha kuanzia sasa na Mei 2024.
Hii ina maana tunapotazama mwelekeo wa takwimu za hali ya upatikanaji chakula na lishe tunaona hali ya kutisha. Kusini, hali nayo imezidi kuwa mbaya na huko tunashikilia makadirio yetu ya uwezekano wa baa la njaa.”
Ripoti inaonesha kuwa mwendelezo wa uhasama umesambaratisha sekta ya kilimo, ambayo familia za Gaza inategemea kwa ajili ya kujipatia kipato.
“Watu wote kwenye ukanda wa Gaza wanakabiliwa na viwango vya juu vya ukosefu mkubwa wa chakula ukiwekwa katika kiwango cha 3, na 4. Hii inaamanisha nusu ya idadi ya watu wote wa eneo hilo, takribani milioni 1.1 wanaweza kukabiliwa na janga kubwa la ukosefu wa uhakika wa chakula la kiwango cha 5.”
Hivyo amesema usaidizi wa haraka unahitajika kurejesha uzalishaji wa chakula na kwa mujibu wa ripoti
“Inatueleza kuwa baadhi ya mifugo iko hai, na inaweza kusaidiwa na ndio maana FAO inajikita kusaidia mahitaji ya kujipatia kipato Ukanda wa Gaza. Kwa sasa tumepata kibali cha kupeleka tani 1500 za ujazo za chakula cha mifugo.”
Amesema uhai wa mifugo utakuwa hakikisho la upatikanaji wa maziwa kwa familia, maziwa ambayo yatakuwa ni lishe bora kwa watoto na hivyo kukabili utapimlo uliokithiri miongoni mwa watoto.
Akatamatisha akisema, “uhakika wa kupata chakula utawezekana kukiweko na amani. Na haki ya kupata chakula ni haki ya msingi. Hili linapaswa kuzingatiwa na wadau wote.”
Mon, 18 Mar 2024 - 11552 - 18 MACHI 2024
Hii leo jaridani tunaangazia baa la njaa unalowakumba waPalestina katika ukanda wa Gaza, na kesi zinazohusisha wanajeshi wa nchi ya Sudan Kusini. Makala tunasalia hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa, na mashinani tunakupeleka nchini Kenya, kulikoni?
- Hali ya uhakika wa kupata chakula huko Gaza, ni tete na baa la njaa linanyemelea kwenye majimbo ya kaskazini mwa eneo hilo imesema ripoti mpya ya hali ya chakula Gaza iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO, likisema jawabu la kuondokana na hali hiyo ni amani.Timu kutoka Kurugenzi ya Haki na Sheria ya Jeshi la Ulinzi wa Wananchi wa Sudan Kusini (SSPDF) mwishoni mwa wiki kwa usaidizi wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS), imehitimisha tathmini yake katika Kaunti ya Maridi jimboni Equatorial Magharibi kutathmini kesi zinazohusisha wanajeshi wa nchi hiyo. Assumpta Massoi wa Idhaa hii akizungumza na Khadija Mrisho, Afisa kutoka shirika la kiraia la kutetea haki ardhi kwa mwanamke LANDESA tawi la Tanzania yeye akiwa kiongozi wa kampeni ya kimataifa ya Linda Ardhi ya Mwanamke. Akiwa hapa New York, Marekani akishiriki mkutano wa 68 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW68, anaelezea kile walichojifunza. Lakini anaanza na kile kilichowaleta.Katika mashinani tutaelekea Ngong nchini Kenya kusikia ujumbe unaotia moyo wasichana waathirika wa mimba za utotoni.
Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Mon, 18 Mar 2024 - 11551 - Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wasaidia jeshi la Sudan Kusini kutathmini kesi dhidi ya askari
Timu kutoka Kurugenzi ya Haki Sheria ya Jeshi la Ulinzi wa Wananchi wa Sudan Kusini (SSPDF) mwishoni mwa wiki kwa usaidizi wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS), imehitimisha tathmini yake katika Kaunti ya Maridi jimboni Equatorial Magharibi kutathmini kesi zinazohusisha wanajeshi wa nchi hiyo.
Tathimini itawezesha kufunguliwa mashtaka kwa askari wa jeshi ambao wanashukiwa kufanya uhalifu mkubwa, ikiwa ni pamoja na unyanyasaji wa kingono na aina nyingine za unyanyasaji wa kijinsia.
Mama Sarah Bennert, mwanaharakati na mwakilishi wa wanawake anasema hatua hii inawakilisha ishara ya haki na uwajibikaji.
"Tuna masuala mengi yanayotukabili hapa kama wanawake. Wakati mwingine unaripoti kesi na haki imechelewa na unabaki kukata tamaa na bila msaada wowote. Sasa, kwa uwepo wa timu ya tathmini hapa chini tunatumai kesi hizo zote walizozizingatia zitasikilizwa kwa sababu baadhi yetu ambao bado tuna kesi tuna kiwewe."
Idrissa Sylvaine ni Mshauri wa haki sheria wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS) anasema,
“Tathmini hiyo itasaidia kukuza utawala wa sheria, kuleta haki kwa waathiriwa na kuwawajibisha askari wa SSPDF. Tathmini hiyo pia itachangia katika mchakato wa amani nchini Sudan Kusini.”
Mon, 18 Mar 2024 - 11550 - Ushirkiano wa dhati waliotuonesha ulifanya wananchi waachane na mpango wa kuwapiga mawe MONUSCO- Chifu Makofi
Hii leo huko jimboni Kivu Kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kikosi cha 10 cha Tanzania (TANZBATT-10) kilichoko kwenye brigedi ya mapigano (FIB) ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO imekabidhi majukumu kwa kikosi cha 11, TANZBATT-11, katika hafla iliyofanyika eneo la Beni-Mavivi. Msimulizi wetu ni Kapteni Abubakari Muna, Afisa Habari wa TANZBATT-10.
Mkuu wa TANZBATT-10 Luteni Kanali John Peter Kalabaka amekabidhi bendera ya Tanzania kwa Kamanda wa TANZBATT-11 Luteni Kanali Vedasto Ernest Kikoti ikiwa ni ishara ya kuanza majukumu ya ulinzi wa amani, katika tukio ambalo mgeni rasmi alikuwa Kaimu Kamanda wa FIB-MONUSCO Kanali Alex Tamson Malenda.
Akizungumza kwenye hafla hiyo Luteni Kanali Kalabaka amesema kwenye upande wa operesheni wameweza kukabili na kupunguza mashambulizi yanayofanywa na vikundi vilivyojihami kwenye eneo la ulinzi la TANZBATT-10 halikadhalika kuepusha mauaji ya raia wasio na hatia na pia kuepusha vitendo vya ubakaji.
“Kijamii tumeweza kushirikiana na jamii ya hapa Beni-Mavivi na pia kuwapatia misaada mbali mbali ya kijamii,” amesema Mkuu huyo wa TANZBATT-10.
Luteni Kanali Vedasto Ernest Kikoti ambaye amepokea jukumu la ulinzi akaeleza bayana kuwa watatekeleza majukumu yao vyema kwa kuzingatia taratibu za Umoja wa Mataifa na kwamba watakuwa tayari kuendelea kushirikiana na raia.
“Tunaomba wananchi wakubali na waelewe dhamira hiyo, waukubali Umoja wa Mataifa ili kuupa nafasi uweze kutekeleza wajibu wake wa kulinda wananchi wa DRC,” ameeleza Luteni Kanali Kikoti.
Makofi Bukuka Gervain ambaye ni Chifu wa eneo hilo akashukuru TANZBATT-10 kwa ushirikiano walioonesha wakati wote wa kipind ichao cha ulinzi wa amani Beni-Mavivi na kueleza kuwa Kamanda wa Kikosi hicho alikuwa yuko karibu sana na wanajamii akitolea mfano wakati wa michezo ikiwemo mpira wa miguu.
“Ushirikiano wao na sisi umewezesha raia kufungua nyoyo zao na kuondokana na fikra zao za kupiga mawe MONUSCO barabarani. Sasa barabara zilibaki wazi na MONUSCO wakafanya kazi yao vema,” amesema Chifu Makofi
Meja Fatuma Haruna Makula, wa TANZBATT-11 ameahidi kuendeleza uhusiano mzuri kati ya wanajeshi wanawake kutoka Tanzania na wanawake wa Beni-Mavivi akisema, “wanawake maafisa na askari tuliokuja hapa wote tumepita mafunzo mbali mbali kuhusu suala zima la ulinzi wa amani. Tutahakikisha wanashiriki vema shughuli za ulinzi wa mani kwa mujibu wa taratibu za Umoja wa Mataifa chini ya MONUSCO.”
TAGS: Amani na Usalama
News: TANZBATT 10, TANZBATT-11
REgion.: Afrika
Focus: DRC
UN/Partner: MONUSCO
Fri, 15 Mar 2024 - 11549 - Wasichana ni majaji watarajiwa, wafuate ndoto zao katika masomo ya Uanasheria - Hakimu Pamela Achieng
Maadhimisho ya kwanza ya Siku ya Majaji Wanawake duniani yalifanyika tarehe 10 Machi 2022, ikiangazia Haki katika Mtazamo wa Kijinsia. Umoja wa Mataifa umeendelea kuadhimisha siku hii kama sehemu ya juhudi za kimataifa za kuhakikisha usawa wa kijinsia na kushughulikia masuala ya uadilifu wa mahakama yanayohusiana na jinsia. Huku mkutano wa 68 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW68 ukiendelea hapa jijini New York Marekani, nchini Kenya Selina Jerobon wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa kupitia video iliyoandaliwa na washirika wetu Redio Domus amekutana na Pamela Achieng, Hakimu katika mahakama ya Ngong iliyo katika Kaunti ya Kajiado ambaye anaanza kwa kuelezea ni kwa nini kama mwanamke aliamua kuingia katika tasnia hii.
Fri, 15 Mar 2024 - 11548 - 15 MACHI 2024
- Hii leo huko jimboni Kivu Kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kikosi cha 10 cha Tanzania (TANZBATT-10) kilichoko kwenye brigedi ya mapigano (FIB) ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO imekabidhi majukumu kwa kikosi cha 11, TANZBATT-11, katika hafla iliyofanyika eneo la Beni-Mavivi. Msimulizi wetu ni Kapteni Abubakari Muna, Afisa Habari wa TANZBATT-10.Mkutano wa 68 wa Kamisheni ya Hali ya wanawake duniani, CSW68 ukiwa umeingia siku yake ya 5 leo, Idhaa hii ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa imekuwa ikizungumza na washiriki kutoka mataifa mbalimbali. Leo ni baadhi ya washiriki kutoka Tanzania, vinara wa elimu wanaofadhiliwa na Mfuko wa Malala. Katika makala ambapo hivi majuzi kuliadhimishwa Siku ya Majaji Wanawake Duniani ambayo Umoja wa Mataifa umeendelea kuiadhimisha kila mwaka tarehe 10 Mwezi wa Machi kama sehemu ya juhudi za kimataifa za kuhakikisha usawa wa kijinsia na kushughulikia masuala ya uadilifu wa mahakama yanayohusiana na jinsia na tunakupeleka nchini Kenya kusikia ujumbe wa Hakimu Pamela Achieng.Katika mashinani tunakuletea ujumbe wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC akisimulia jinsi alivyotekwa na makundi yaliyojihami ya waasi lakini hatimaye sasa amenasuliwa na amerejea kwenye jamii kwa msaada wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO.
Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Fri, 15 Mar 2024 - 11547 - CSW68: Vinara wa elimu kutoka Tanzania wajizatiti kuhakikisha sauti za wasichana zinasikika
Mkutano wa 68 wa Kamisheni ya Hali ya wanawake duniani, CSW68 ukiwa umeingia siku yake ya 5 leo, Idhaa hii ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa imekuwa ikizungumza na washiriki kutoka mataifa mbalimbali. Leo ni baadhi ya washiriki kutoka Tanzania, vinara wa elimu wanaofadhiliwa na Mfuko wa Malala.
Zahra Salehe Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali linaloitwa ICCAO anaeleza ujumbe mkubwa waliokuja nao.
“Tumeletwa hapa kwa ajenda moja ya elimu na ujumbe mkubwa tuliokuja nao ni wa kuhakikisha sauti za wasichana na wanawake vijana zinasikika kwenye majukwaa makubwa kama haya CSW68 na sisi ajenda kubwa ambayo tunaiona kwas asa ni ‘reentry’ ambayo ni ruhusa ya msichana kurudi shule baada kupitia changamoto kubwa. Tisimuache mtu nyuma kwa sababu ya sababu mbalimbali ambazo zote zimeletwa na kutokuwa na usawa wa kijinsia. Wanaendelea na wanaendelea kutimiza ndoto zao.”
Paulina Ngurumwa kutoka taasisi ya KINNAPA anakubaliana na anachosema kinara wa elimu mwenzake na anasema wanapambana na vikwazo dhidi ya elimu ya wanawake ingawa bado kuna ugumu
“Hatuna mabweni, hatuna mahali pa kuwaweka kwa hiyo tunajikuta kuna mzigo mwingi. Kwa hiyo wito wetu wadau kwa ngazi ya ulimwengu, kwa ngazi ya mataifa, kwa ngazi ya taifa letu la Tanzania tushikamane tuone ni namna gani tunaweza kutafuta hata namna gani tuwapatie hawa watoto mabweni ambayo wanaweza wakasomea na wakakaa pale wakawa katika mazingira salama ili waeze kutimiza ndoto zao.”
Kutokana na changamoto kama hizo Nasra Kibukila kutoka shirika la TEN/MeT anapigia chepuo Bajeti ya nchi inayozingatia jinsia
“Kwa sasa hivi Tanzania tumeshaanza mchakato wa kutengeneza bajeti ya mwaka 2024-2025 na kwas asa hivi iko kwenye ngazi ya wabunge. Tutakapotoka hapa, tutakayojifunza hapa tukirudi nyumbani tunaenda kuwa na mkutano pamoja na wabunge kuweza kuwaelezea yapi tumejifunza kwa jinsi gani kuwa na majeti yenye mrengo wa kijinsia na wao waweze kutusaidia kuhakikisha kuwa pale tutapakuwa na bajeti ya 2024-25inakuwa iko kwenye mrengo wa kijinsia kuweza kuhakikisha kuwa makundi yote maalumu yanakuwa yana bajeti yao kuwawezesha.”
Fri, 15 Mar 2024 - 11546 - Kauli ya ‘usifanye hiki usifanye kile’ inadidimiza ndoto za wasichana – Frida Amani
Makala hii inakupeleka Nairobi, Kenya ambako Priscilla Lecomte wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Mratibu wa hatua dhidi ya majanga ya tabianchi na El Niño anazungumza na Mwanamuziki Frida Amani wa Tanzania. Frida Amani anatoa wito kwa watoto wa kike duniani kutokatishwa tamaa kwa kuambiwa “usifanye shughuli fulani kwa kuwa ni ya kiume” kwani kama yeye angekata tamaa asingeweza kuwa msanii wa Hip Hop ambayo imemfikisha katika majukwaa ya kimataifa kiasi cha kuandaa wimbo wa kuhamasisha ushirikiano wa kimataifa katika kuchukua hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, wimbo ambao umeungwa mkono na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira Duniani (UNEP). Hapa Frida anaanza kwa kueleza kwa nini wimbo alioshirikiana na msanii Dex Mc Bean wa Marekani waliamua kuupa jina Twende na Mpango.
Wed, 13 Mar 2024 - 11545 - Watoto waliouawa Gaza ni wengi kuliko miaka 4 ya vita duniani
Wakati kukiwa na ripoti za mashambulizi kwa njia ya anga yanayotekelezwa na Israel huko Gaza usiku wa kuamkia leo, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina UNRWA limesema idadi ya watoto waliouawa katika miezi ya hivi karibuni ni kubwa kuliko miaka minne ya mizozo duniani.
Phillipe Lazzarini ambaye ni Mkuu wa shirika hilo la msaada kwa wakimbizi wa kipalestina hii leo kupitia mtandao wake wa X zamani Twitter ameandika ujumbe alioambatanisha na mchoro unaoonesha mambo mamwili kushoto kwenye rangi ya buluu idadi ya watoto waliouawa kutokana na vita tangu mwaka 2019 mpaka 2022 ambao ni 12, 193 na kulia ni idadi ya watoto waliouawa Gaza tangu mwezi Oktoba mwaka jana 2023 mpaka mwezi Februari 2024 ambao ni zaidi ya 12,300.
Na ndipo akaandika ujumbe kuwa “Vita hii ni vita dhidi ya watoto. Ni vita dhidi ya utoto wao na mustakabali wao.”
Mkuu huyo wa UNRWA akaendelea na ujumbe wake na kusema kuwa “Sitisheni mapigano sasa kwa ajili ya watoto wa Gaza“.
Kwa mujibu wa takwimu kutoka mamlaka za afya huko Gaza, mpaka sasa zaidi ya wapalestina 31,184 wameuawa na wengine 72,889 kujeruhiwa.
Mpaka kufikia tarehe 12 ya mwezi huu wa Machi, wanajeshi 247 wa Israel wameripotiwa kuuawa na wengine 1,475 kujeruhiwa tangu kuanza kwa operesheni za ardhini kwa mujibu wa takwimu za jeshi la Israel.
Sio mashambulizi tu ya mabomu yanayo gharimu maisha ya watoto na wakazi wa Gaza, janga la njaa nalo pia lipo hatihati kukumba wananchi hao ambao a misaada ya kibiandamu kuwafikia imekuwa changamoto kubwa.
Mashirika ya Umoja wa Mataifa ya kibinadamu yamekuwa yakirejea kutoa maonyo kuhusu hali mbaya ya Gaza ambapo mtu mmoja kati ya wanne anakaribia kukumbwa na njaa.
Mpaka sasa takriban watu 25 wamekufa kutokana na utapiamlo mkali na upungufu wa maji mwilini kaskazini mwa Gaza kulingana na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada, OCHA, 21 kati yao wakiripotiwa kuwa watoto.
Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF, limeonya kuwa vijana ni miongoni mwa wale ambao hawawezi kustahimili njaa na magonjwa, huku vijana milioni moja wakiwa tayari wameondolewa makwao kutokana na vita, na watoto 17,000 wasio na wasindikizaji au waliotenganishwa nao sawa na 1% ya watu milioni 1.7 ya wananchi wa Gaza wamelazimika kuyakimbia makazi yao.
Juhudi za ushirikiano wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa kusaidia kupunguza hali hiyo ya kukatisha tamaa zinaendelea na hapo jana Shirika lake la Mpango wa Chakula Duniani WFP lilifanikiwa kufikisha Msaada mjini Gaza ambapo hawakuwahi kufika tangu tarehe 20 Februari.
Shirika jingine la UN lile la Afya WHO na wadau wake nao walifanikiwa kufikia hospital mbili zilizoko Gaza Kaskazini Al Shifa na Al Helo una kufikisha misaada ya vifaa tiba pamoja na mafuta ya kuendeshea mitambo ya hospitali.
Hata hivyo mkuu wa shirika hilo la WHO Dkt.Tedros Adhanom Ghebreyesus kupitia mtandao wa X alisema kuwa Hospitali ya Al Shifa ilikuwa na inafanya kazi sehemu ndogo tu na inahitaji haraka wafanyakazi maalum wa afya.
Mahitaji yanasalia kuwa makubwa na ya haraka katika hospitali ya Al Helou, Dkt. Tedros aliongeza, huku huduma zikiwa chache katika idara zote, pamoja na uhaba wa mafuta, chakula, vifaa vya upasuaji na wafanyikazi wa matibabu.
Wed, 13 Mar 2024 - 11544 - 13 JANUARY 2024
- Wakati kukiwa na ripoti za mashambulizi kwa njia ya anga yanayotekelezwa na Israel huko Gaza usiku wa kuamkia leo, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina UNRWA limesema idadi ya watoto waliouawa katika miezi ya hivi karibuni ni kubwa kuliko miaka minne ya mizozo duniani kote.Idadi ya vifo vya watoto wenye umri wa chini ya miaka 5 duniani kote imepungua na kufikia kiwango cha chini zaidi kuwahi kufikiwa katika historia, ambapo takwimu mpya zilizotolewa na Umoja wa Mataifa zinaonesha kuwa mwaka 2022 idadi ya vifo ilikuwa chini ya milioni 4.9, sawa na pungufu kwa asilimia 51 tangu mwaka 2000. Makala inatupeleka Nairobi, Kenya ambako Priscilla Lecomte wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Mratibu wa hatua dhidi ya majanga ya tabianchi na El Niño anazungumza na Mwanamuziki Frida Amani wa Tanzania. Frida Amani anatoa wito kwa watoto wa kike duniani kutokatishwa tamaa kwa kuambiwa “usifanye shughuli fulani kwa kuwa ni ya kiume” kwani kama yeye angekata tamaa asingeweza kuwa msanii wa Hip Hop ambayo imemfikisha katika majukwaa ya kimataifa kiasi cha kuandaa wimbo wa kuhamasisha ushirikiano wa kimataifa katika kuchukua hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, wimbo ambao umeungwa mkono na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira Duniani (UNEP).Katika mashinani tutaelekea nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kusikia ujumbe wa mlinda amani mwanamke.
Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Wed, 13 Mar 2024 - 11543 - Juhudi za mashirika zafanikisha kupunguza vifo vya watoto wenye umri wa chini ya miaka 5
Idadi ya vifo vya watoto wenye umri wa chini ya miaka 5 duniani kote imepungua na kufikia kiwango cha chini zaidi kuwahi kufikiwa katika historia, ambapo takwimu mpya zilizotolewa na Umoja wa Mataifa zinaonesha kuwa mwaka 2022 idadi ya vifo ilikuwa chini ya milioni 4.9, sawa na pungufu kwa asilimia 51 tangu mwaka 2000.
Ama hakika ni mafanikio makubwa kwani video iliyoambatana na habari hizi njema inaonesha madaktari, wakunga, wahudumu wa afya wakiwemo wale wa kijamii huko, Afrika, wakijituma kwa dhati kutoa huduma kuanzia kwa wajawazito, huduma za mama na mtoto hadi chanjo.
Mathalani Sierra Leone anaonekana mhudumu wa afya akifika moja ya kaya kutoa huduma ya chanjo dhidi ya Numonia au vichomi.
Cambodia, Malawi, Mongolia na Rwanda zimetajwa kuwa ni nchi ambamo idadi ya vifo vya watoto hao imepungua kwa zaidi ya asilimia 75 kati ya 2000 na 2022.
Ripoti imetolewa na kundi la mashirika na taasisi ya Umoja wa Mataifa, IGME, linaloongozwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF ambalo Mkurugenzi Mtendaji wake Catherine Russell amepongeza juhudi za mtu mmoja mmoja, serikali, wakunga, wahudumu wa afya wakiwemo wale wa kijamii.
Amesema kujituma kwao katika kuhakikisha watoto wanafikishiwa huduma bora na fanisi za afya tena kwa gharama nafuu, kumethibitisha kuwa dunia ina ufahamu na mbinu za kuokoa maisha.
Licha ya mafanikio hayo, ripoti inaonya kuwa bado safari ni ndefu kufikia lengo la kutokomeza vifo vya watoto vinavyoweza kuzuilika, kwa kuwa mamilioni wanaendelea kufariki dunia kutokana na magonjwa yanayotibika, changamoto za ujautizo, vichomi au numonia, kuhara na malaria.
Idadi kubwa ya vifo hivyo ni katika nchi za Afrika zilizo Kusini mwa jangwa la Sahara na kusini mwa Asia, hali inayodhihirisha tofauti za kikanda katika upatikanaji wa huduma bora za afya.
Ripoti imetambua pia ukosefu wa utulivu kiuchumi, mizozo, mabadiliko ya tabianchi na changamoto zilizoachwa kutokana na janga la COVID-19, ikisema mambo hayo yanazidi kuchochea tofauti za usawa kwenye utoaji wa huduma za afya.
Kundi hilo linaitwa IGME na linajumuisha mashirika ya Umoja wa Mataifa likiwemo la kuhudumia watoto, UNICEF, la afya, WHO, Benki ya Dunia na kitengo cha Idadi ya Watu cha Idara ya Umoja wa Mataifa ya Masuala ya Kiuchumi na Kijamii, DESA.
IGME ilianzishwa mwaka 2004 kuwezesha wasihrika kubadilishana takwimu na kuboresha mbinu kwa ajili ya takwimu za vifo vya watoto na kufuatilia maendeleo kuelekea kufikia malengo kuhusu uhai wa mtoto.
Wed, 13 Mar 2024 - 11542 - Je wafahamu maana ya neno "Kupwemka?"Thu, 14 Mar 2024
- 11541 - 14 MACHI 2024
- Baada ya Kenya kutangaza kusitisha mpango wake wa kupeleka askari wa kuleta utulivu nchini Haiti hadi pale hali ya kisiasa itakapotengamaa, Umoja wa Mataifa umetoa wito kwa Jumuiya ya kimataifa kusaidiana katika kuunda operesheni ya usaidizi kwa watu wa Haiti haraka iwezekanavyo.Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu dawa za kulevya (CND), imeanza mkutano wake hii leo huko Vienna Austria kukagua maendeleo yaliyopatikana katika kushughulikia tatizo la dawa za kulevya duniani na jinsi ya kuhakikisha utekelezaji wa ahadi za kimataifa. Na kukiwa na ripoti za kwamba leo Wapalestina 6 wameuawa kwa kupigwa risasi na wengine 83 wakijeruhiwa wakati wakisubiri malori ya misaada huko Gaza, Mkuu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya kibinadamu OCHA, Martin Griffiths kupitia ukurasa wa mtandao wa X ametoa wito wa kulindwa kwa operesheni za misaada ya kibinadamu inayohitajika sana Gaza.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mkuu wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anachambua maana ya neno “KUPWEMKA”.
Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Thu, 14 Mar 2024 - 11536 - 12 MACHI 2024
- Meli iliyosheheni misaada ya kibinadamu imeanza safari yake kutoka Cyprus kuelekea Gaza ikiwa na shehena ya tani 200 za misaada ya kuokoa maisha kwa ajili ya wananchi wa Gaza.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP hii leo linaonya kuwa litalazimika kusitisha misaada ya kuokoa maisha nchini Chad ifikapo mwezi ujao wa Aprili iwapo litakosa ufadhili wa haraka kwa ajili ya kusaidia wakimbizi. Na mkutano wa 68 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW68, ukiendelea hapa jijini New York Marekani hii leo kutakuwa na mikutano ya kujadili mambo mbalimbali ikiwemo hali ya wanawake nchini Afghanistan, kuziba pengo la kujinsia kwenye elimu, athari za umaskini na uhalifu katika huduma ya utoaji mimba pamoja na mkutano wa kuangalia jinsi mabunge yanayozingatia jinsia katika kuendeleza usawa wa kijinsia ili kumaliza umaskini.Katika mashinani tunakuletea ujumbe wa Marynsia Mangu, kijana kutoka Tanzania na Afisa Mtendaji Mkuu wa shirika lisilo la kiserikali la Success Hands Tanzania anayeshiriki mkutano wa 68 wa Kamisheni ya hali ya wanawake duniani, CSW68 hapa New York, Marekani akielezea matarajio yake kwenye mkutano huu.
Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Tue, 12 Mar 2024 - 11535 - Mlo shuleni umeongeza idadi ya wanafunzi wangu shule ya Salama: Mwalimu Beatrice Nyakoa Osaka
Shule ya Salama iliyo katika eneo la Huruma karibu na mtaa wa mabanda wa Mathare jijini Nairobi Kenya hivi karibuni imeanza programu ya mlo shuleni kupitia mradi wa kampuni ya ‘Food for Education”. Hatua hiyo imenfa idadi ya wanafunzi wanaosoma shule hiyo kuongezeka kutoka 1, 900 hadi 2,300. Mlo shuleni ni moja ya masuala ambayo yanapigiwa debe kubwa na Umoja wa Mataifa sio tu kwa sababu ya kuhakikisha lishe bora kwa mamia ya maelfu ya wanafunzi ambao wengi hawawezi kupata mlo nyumbani bali pia kuongeza idadi ya watoto wanaohudhuria masomo. Stella Vuzo afisa habari wa kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa nchini Kenya UNIS Nairobi amefunga safari hadi shuleni Salama na kuzungumza na mwalimu mkuu wa shule hiyo Beatrice Nyakoa Osaka anayeenza kwa kufafanua umuhimu wa mradi huo shuleni kwake hasa kutokana na eneo walipo.
Mon, 11 Mar 2024 - 11534 - Mashambulizi na umwagaji damu vinaendelea Gaza licha ya kuanza kwa Ramadhan mauaji - Guterres
Leo ni mwanzo wa mwezi mktukufu wa Ramadhan ambapo Waislamu kote duniani husherehekea na kuchagiza tunu za amani, maridhiano na mshikamano lakini uhasama unaendelea hususani sehemu mbalimbali duniani ikiwemo Gaza ambako mauaji , na mashambulizi hayajakoma amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akizungumza na waandishi wa habari mjini New York Marekani hii leo.
Hivyo ndivyo alivyoanza Katibu Mkuu katika tarifa yake fupi kwa waandishi wa habari akikumbusha kuwa ni hivi majuzi tuliingia mwezi wa sita tangu shambulio la kigaidi la Hamas nchini Israel na mashambulizi mabaya ya Israel huko Gaza.
Ameo leo ana ombi kubwa ambalo ni “kuheshimu dhamira ya Ramadhani kwa kunyamazisha mtutu wa bunduki na kuondoa vikwazo vyote ili kuhakikisha utoaji wa misaada ya kuokoa maisha kwa kasi na kiwango kikubwa kinachohitajika.”
Pia ametaka wakati huohuo kwa kuzingatia dhamira ya Ramadhani kuwaachilia mateka wote wanaoshikiliwa mara moja.
Katibu Mkuu ameonya kwamba “Macho yadunia yanatazama. Macho ya historia yanatazama. Hatuwezi kuyapa kisogo yanayoendelea ni lazima tuchukue hatua kuepusha vifo vinavyoweza kuzuilika.”
Amesema Dunia imeshuhudia mwezi baada ya mwezi mauaji ya raia na uharibifu wa miundombinu ya raia kwa kiwango ambacho hakijawahi kutokea katika miaka yangu yote akiwa Katibu Mkuu.
Na kwamba msaada wa kuokoa Maisha kwa raia Gaza unaingia kwa vikwazo vikbwa na wakati mwingine hauingii kabisa.
Amesema hivi sasa Sheria ya kimataifa za kibinadamu ziko katika hali mbaya.Na tishio la Israel kushambulia Rafah zinaweza kuwatumbukiza kuzimu zaidi watu wa Gaza.
Amesema pamoja na kwamba viongozi wa Dunia na wahudumu wa kibinadamu wamekuwa wakitoa wito wa kusitishwa mapigano wito mahsusi umetoka kwa familia za waathirika wa vita hivi.
Sitasahau mikutano yangu pamoja nao na wamesimama kwenye jukwaa hili na kukuhutubia wameungana kwa ujasiri mkubwa na maumivu yasiyopimika.
Familia za mateka wa Israeli ambao wameeleza mateso na uchungu wao na wameomba kuachiliwa mara moja kwa wapendwa wao.
Pia alikutana na familia za waathirika wa Gaza ambazi zimeomba uhasama kutishishwa mara moja “Kama mmoja wa wanafamilia hao alisema, Hatuko hapa kwa ajili ya rambirambi. Hatupo hapa kwa ajili ya kuomba msamaha. Tuko hapa kwa ajili ya kuchukuliwa hatua za haraka. Je, hili ni kubwa sana kuliomba? Ni lazima tusikilize na kutii sauti hizo.” Amesesisitiza Guterres.
Pia amesema leo anatoa ombi la usitishaji uhasama Sudan kwa ajili ya Ramadhani na kukumbusha kwamba hivi karibuni mwezi Aprili kutakuwa na Sikukuu za Pasaka na sikukuu ya Wayahudi ya Passover hivyo huu ni wakati wa kuonyesha huruma, kuchukua hatua na kurejesha Amani.
Mon, 11 Mar 2024 - 11533 - Mlo shuleni umeongeza idadi ya wanafunzi wangu shule ya Salama: Mwalimu Beatrice Osaka
Shule ya Salama iliyo katika eneo la Huruma karibu na mtaa wa mabanda wa Mathare jijini Nairobi Kenya hivi karibuni imeanza programu ya mlo shuleni kupitia mradi wa kampuni ya ‘Food for Education”. Hatua hiyo imenfa idadi ya wanafunzi wanaosoma shule hiyo kuongezeka kutoka 1, 900 hadi 2,300. Mlo shuleni ni moja ya masuala ambayo yanapigiwa debe kubwa na Umoja wa Mataifa sio tu kwa sababu ya kuhakikisha lishe bora kwa mamia ya maelfu ya wanafunzi ambao wengi hawawezi kupata mlo nyumbani bali pia kuongeza idadi ya watoto wanaohudhuria masomo. Stella Vuzo afisa habari wa kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa nchini Kenya UNIS Nairobi amefunga safari hadi shuleni Salama na kuzungumza na mwalimu mkuu wa shule hiyo Beatrice Nyakoa Osaka anayeenza kwa kufafanua umuhimu wa mradi huo shuleni kwake hasa kutokana na eneo walipo
Mon, 11 Mar 2024 - 11532 - 11 MACHI 2024
Hii leo jaridani tunaangazia ujumbe wa Katibu Mkuu kuhusu mwezi mktukufu wa Ramadhan, na uwezeshaji wa wanawake wakulima nchini Malawai. Makala na mashinani tunakupeleka nchini Kenya, kulikoni?
- Leo ni mwanzo wa mwezi mktukufu wa Ramadhan ambapo Waislamu kote duniani husherehekea na kuchagiza tunu za amani, maridhiano na mshikamano lakini uhasama unaendelea hususani sehemu mbalimbali duniani ikiwemo Gaza ambako mauaji , na mashambulizi hayajakoma amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akizungumza na waandishi wa habari mjini New York Marekani hii leo.Nchini Malawi Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa maendeleo ya Kilimo IFAD unatekeleza mradi wa kuwasaidia wanawake wa vijijini kukabiliana na ukosefu wa usawa wa kijinsia na sasa wananachi wanafaidi matunda yake. Makala inatupeleka katika shule ya Salama iliyo katika eneo la Huruma karibu na mtaa wa mabanda wa Mathare jijini Nairobi Kenya hivi karibuni imeanza programu ya mlo shuleni kupitia mradi wa kampuni ya ‘Food for Education”. Hatua hiyo imenfa idadi ya wanafunzi wanaosoma shule hiyo kuongezeka kutoka 1, 900 hadi 2,300. Mlo shuleni ni moja ya masuala ambayo yanapigiwa debe kubwa na Umoja wa Mataifa sio tu kwa sababu ya kuhakikisha lishe bora kwa mamia ya maelfu ya wanafunzi ambao wengi hawawezi kupata mlo nyumbani bali pia kuongeza idadi ya watoto wanaohudhuria masomo.Na mashinanitunasalia nchini Kenya kumulika jinsi mradi wa FAO umemwezesha msichana mwenye ulemavu kuondokana na msongo wa mawazo na kisha kujikwamua kiuchumi.
Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Mon, 11 Mar 2024 - 11531 - IFAD: Mradi wa ukulima nchini Malawi waboresha maisha ya na usawa kijinsia katika jamii
Nchini Malawi Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa maendeleo ya Kilimo IFAD unatekeleza mradi wa kuwasaidia wanawake wa vijijini kukabiliana na ukosefu wa usawa wa kijinsia na sasa wananachi wanafaidi matunda yake.
Mradi huo uitwao TRADE ulioanzishwa mwaka 2022 na serikali ya Malawi kwa kushirikiana na IFAD inalenga kubadilisha kilimo kupitia mpango wake wa Mseto na Ujasiriamali.
Amos Mailosi ni Afisa Mazingira wa kanda Mabadiliko ya Tabianchi wa mradi huo wa TRADE na anasema jambo muhimu katika mradi wao ni kuhakikisha familia zinafanya kazi na kufikia maamuzi pamoja.
“Moja ya eneo muhimu katika programu yetu ya TRADE ni kuhamasisha suala la ushirikishwaji wa kijinsia ndani ya jamii. Kwa hivyo, tunajaribu kuwawezesha wanawake na wanaume, na wavulana na wasichana, kushiriki kwa usawa katika afua. Ili kwa pamoja waweze kutambua umuhimu wa kufanya maamuzi ya pamoja katika ngazi ya kaya.”
Kwa miaka mwili sasa mafanikio yameanza kuoneskana, na mmoja wa wanufaika hao ni Alefu Ofesa na mume wake Lloyd ambao wamekuwa wakulima kwa miaka 20 lakini kwa takriban miaka miwili wamebadili kilimo kuwa biashara. Mabadiliko haya yamefuatitia Alefa na wanawake wenzake kijijini kupatiwa Msaada na mafunzo ya mbinu mpya za kilimo ambazo zimewasaidia kukabiliana na mvua zisizokuwa na uhakika katika ukanda huo.
“Mradi huu umekuwa ukihimiza wanawake kushiriki katika kilimo. Kwa ujuzi na maarifa tuliyopatiwa tuna uhakika kuhusu kile kinachohitajika kufanywa ili kuboresha uzalishaji, kwa mfano upandaji kwa kutumia mistari miwili. Wanawake wengi hapa sasa ni wataalam wa shughuli za kilimo na kwa sababu ya faida wanazopata, wengi wametambua umuhimu wa kujiunga pamoja.”
Alefa amepanga kutumia mapato ya ziada wanayopata kwa ajili ya kuwapatia elimu watoto wao na kununua kigari cha ng'ombe kwa ajili ya usafiri.
Sio tu kwamba familia yake sasa ina chakula cha kutosha kwa mwaka mzima, lakini sasa anaweza pia kuuza sehemu ya kile anachovuna, na anapanga kupanua biashara yake ili kuuza kwenye masoko katika vijiji vya jirani.
Mon, 11 Mar 2024 - 11530 - KIGOMa: Mafunzo ya kilimo hifadhi kutoka FAO chaongeza mavuno mahindi kutoka magunia 4 hadi 45
Sasa ni makala inayotupeleka mkoani Kigoma, kaskazini-magharibi mwa Tanzania ambako huko shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo, FAO limetekeleza kwa vitendo ujumbe wa mwaka huu wa siku ya wanawake duniani, Wekeza kwa Wanawake, Songesha Maendeleo, kwa kuwapatia mafunzo ya ufugaji bora wa kuku na mbuzi, halikadhalika kilimo hifadhi kisichoharibu mazingira. Sasa manufaa yako dhahiri kwani wanawake wameinuka kiuchumi. Miongoni mwao ni Hadija Alisido, mkazi wa kijiji Muhange, wilaya ya Kakonko. Katika makala hii inayoletwa kwako na Assumpta Massoi wa Idhaa hii, Hadija anaelezea alivyoinuliwa na FAO.
Fri, 08 Mar 2024 - 11529 - 08 MACHI 2024
Hii leo jaridani mwenyeji wako ni Flora Nducha anamulika siku ya wanawake duniani kuanzia habari ya kwanza hadi ya mwisho maudhui yakiwa Wekeza kwa wanawake - songesha maendeleo.
- Katika kusherehekea siku ya wanawake duniani kote Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amewapongeza wanawake na wasichana kwa kupata mafanikio makubwa na kuondoa vikwazo, kuvunja fikra potofu na kuchochea maendeleo kuelekea dunia yenye haki na usawa zaidi.Nchini Afrika Kusini katika jimbo la Western Cape kufuatia mafunzo kuhusu unyanyasaji wa kijinsia yaliyotolewa na kikundi cha wanawake cha Ilitha Labantu kwa vituo kadhaa vya polisi, sasa kuna ushahidi wa wazi kwamba vituo vya polisi vimeweka mazingira rafiki ya kuwasikiliza wanawake walionyanyaswa kuliko ilivyokuwa hapo awali. Anold Kayanda ameufuatilia mradi huo.Makala inatupeleka Kigoma nchini Tanzania kumsikia shuhuda Hadija Alisido ambaye amenufaika na miradi ya FAO.Mashinani tunabisha hodi Mwanza nchini Tanzania kupata maoni kuhusu siku ya wanawake duniani. Karibu!
Fri, 08 Mar 2024 - 11528 - Ukatili dhidi ya wanawake Afrika kusini: Polisi 'wanolewa' sasa mambo ni shwari
Nchini Afrika Kusini katika jimbo la Western Cape kufuatia mafunzo kuhusu unyanyasaji wa kijinsia yaliyotolewa na kikundi cha wanawake cha Ilitha Labantu kwa vituo kadhaa vya polisi, sasa kuna ushahidi wa wazi kwamba vituo vya polisi vimeweka mazingira rafiki ya kuwasikiliza wanawake walionyanyaswa kuliko ilivyokuwa hapo awali. Anold Kayanda ameufuatilia mradi huo. Karibu Anold utueleze zaidi.
(Taarifa ya Anold Kayanda)
Asante sana Flora Nducha. Shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya wanawake (UN Women) linasema kiwango cha unyanyasaji dhidi ya wanawake na wasichana nchini Afrika Kusini ni miongoni mwa viwango vya juu zaidi duniani na wanafafanua wakisema kwamba mwanamke mmoja kati ya watano walio katika uhusiano amepitia ukatili wa kimwili uliofanywa na mpenzi wake.
Wengi zaidi wameteseka na aina nyingine za vurugu kutoka kwa wanaume wanaowajua na wasiowajua lakini changamoto zaidi ni namna ya kuyashughulikia masuala haya kwani matukio mengi ya unyanyasaji hayaripotiwi kwa mamlaka kutokana na imani ndogo kwa vyombo vya sheria.
Ella Mangisa, Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo la Ilitha Labantu anasema ulikuwa unakuta mwanamke anayekimbia hali ya vurugu, akifika polisi ataambiwa arudi nyumbani akaelewane na mnyanyasaji wake au kuambiwa haya ni masuala ya kibinafsi wanayohitaji kutatua wao wenyewe."
Kupitia ushirikiano na UN Women na wadau wengine ndipo Ilitha Labantu mwaka 2021 ilizindua mpango wa kufanya kazi na Huduma ya Polisi ya Afrika Kusini (SAPS) kuwaelimisha maafisa kufanya kazi na waathirika wa ukatili wa kijinsia. Mpango umetekelezwa katika vituo 75 vya polisi huko Cape Metro na Cape Winelands katika Mkoa wa Western Cape.
Ilitha Labantu inapanga kupanua zaidi mpango huo na kushirikisha mashirika mengine yenye utaalamu tofauti. Shirika hilo pia linatarajia kujumuisha maudhui ya mafunzo yao katika mtaala wa vyuo vya polisi kote nchini Afrika Kusini.
Fri, 08 Mar 2024 - 11527 - Kuwekeza kwa wanawake ni jawabu sahihi - Guterres
Katika kusherehekea siku ya wanawake duniani kote Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amewapongeza wanawake na wasichana kwa kupata mafanikio makubwa na kuondoa vikwazo, kuvunja fikra potofu na kuchochea maendeleo kuelekea dunia yenye haki na usawa zaidi. Leah Mushi na maelezo zaidi.
Katika ujumbe wake kwa siku hii Katibu Mkuu Guterres amesema “Pamoja na juhudi wanazozifanya kila siku bado wanakabiliwa na vikwazo vikubwa. Mabilioni ya wanawake na wasichana wanakabiliwa na kuenguliwa, ukosefu wa haki na ubaguzi, ilhali janga lililojikita la ukatili dhidi ya wanawake lilikimomonyoa ubinamu.”
Amesema ni vyema kuongeza juhudi ikiwemo za kisheria katika kukabiliana na changamoto zinazowakabili wanawake kwani kwa kasi ya sasa itachukua miaka miatatu kupata usawa.
Akieleza nini kifanyike amesema “ tunapaswa kuwekeza kwenye miradi ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na kuchochea ujumuishaji wanawake na uongozi wa wanawake kwenye uchumi, teknolojia za kidijitali, ujenzi wa amani na hatua kwa tabianchi.Yote hii inategemea kupatikana kwa fedha kwa ajili ya maendeleo endelevu ili nchi ziwe na fedha za kuwekeza kwa wanawake na wasichana.”
Kauli mbiu ya siku ya wanawake kwa mwaka huu ni wekeza kwa wanawake ili kuharakisha maendeleo na Mkuu huyo wa umoja wa Mataifa amesema inatukumbusha kuwa kutokomeza mfumo dume kunahitaji kuweko kwa fedha mezani.
“Tunahitaji pia kuongeza idadi ya wanawake viongozi kwenye sekta ya biashara, Benki Kuu na Wizara za Fedha. Hii inaweza kusaidia kuchochea uwekezaji kwenye sera na miradi inayokidhi mahitaji ya wanawake na wasichana.
Haki za wanawake zimedhihirisha kuwa njia ya haki ya jamii zenye haki, amani na ustawi. Hii ni vema kwetu sote.
“Kwa Pamoja, hebu na tuchukue hatua za haraka kufanya kuwa halisia.”
Usawa kwa woteNalo shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wanawake UN Women linaadhimisha siku hii kwa kufanya mkutano mkubwa katika makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani utakao wakutanisha pamoja viongozi wa ngazi za juu wa Umoja wa Mataifa na wadau wengine wa masuala ya wanawake.
UN Women wamesema katika mwaka huu ambapo karibu nusu ya watu duniani wanaishi katika nchi zinazoshiriki katika uchaguzi, Siku hii ya Kimataifa ya Wanawake ni fursa muhimu ya kufafanua siku zijazo tunazotaka.
Wakati mizozo, mabadiliko ya tabianchi na jamii zenye mgawanyiko zikididimiza miongo kadhaa ya maendeleo katika usawa wa kijinsia, UN Women inatoa wito waku "Wekeza kwa wanawake ili Kuharakisha Maendeleo" ili hatimae dunia iweze kufikia faida ya usawa wa kijinsia kwa wote.
Fri, 08 Mar 2024 - 11526 - 07 Machi 2024
Hii leo jaridani tunaangazia miradi inayotekelezwa na Umoja wa Mataifa huko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo -DRC kusaidia wanawake ikiwa ni kuelekea siku ya wanawake duniani hapo kesho Machi 8.
Pia utapata fursa ya kusikiliza muhtasari wa habari na kujifunza lugha ya kiswahili ambapo leo ni ufafanuzi wa methali 'AFUNGAYE KIBWEBWE SI BURE ANA MCHEZO'
Thu, 07 Mar 2024 - 11525 - Wanawake na wasichana wakiwezeshwa jamii zinanufaika - Wanabiashara Kenya
Wiki hii Ijumaa tarehe 8 Machi 2024, ulimwengu utaadhimisha Siku ya Wanawake Duniani ambapo mwaka huu ina maudhui “Wekeza kwa wanawake: Harakisha maendeleo,” lakini Shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya wanawake, UN Women linasema ni dhahiri kwamba ulimwengu bado unakabiliwa na migogoro mingi, kuanzia mizozo ya kijiografia hadi viwango vya umaskini vinavyoongezeka, ukosefu wa usawa na kuongezeka kwa athari za mabadiliko ya tabianchi.
Kwa kuwekeza kwa wanawake, tunaweza kuibua mabadiliko na kuharakisha mpito kuelekea dunia yenye afya, usalama na usawa zaidi kwa wote. Nchini Kenya tunakutana na mama mjasiriamali ambaye alianza kwa kufanya kazi na shirika lisilo la kiserikali liitwalo Sime Food, ambalo linahusika na kilimo endelevu, lishe bora, na stadi za biashara ndogo ndogo ili wawe na maarifa na ujuzi unaohitajika ili kupatia familia zao lishe bora mwaka mzima na kuuza masalio ili kusaidia kulipia mahitaji mengine ya kaya. Baada ya kupata mafunzo hayo na fedha za kuanzisha biashara zake, Lucy anachochea kinamama na vijana wa kike wajiunge naye katika sekta ya biashara ili waweze kujikwamua kiuchumi. Selina Jerobon wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa amefuatilia na kutuandalia makala hii.
Wed, 06 Mar 2024 - 11524 - 06 MACHI 2024
- Takriban miezi 11 tangu majenerali wapinzani watangaze vita nchini Sudan, wahudumu wa kibinadamu wa Umoja wa Mataifa leo walionya kwamba mzozo huo unaweza kusababisha janga kubwa zaidi la njaa duniani.Harakati za ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO, za kuondoka nchini humo zikiendelea, tunamulika hatua chanya zilizochukuliwa na ujumbe huo katika kunusuru vijana waliokuwa wanatumikishwa na waasi mashariki mwa nchi hiyo. Katika makala na tukielekea Siku ya Wanawake Duniani ambayo mwaka huu ina maudhui “Wekeza kwa wanawake: Harakisha maendeleo,”, tunatembelea wajasiriamali Kajiado nchini Kenya kusiki ni kwa jinsi gani wanawezakujiumudu kiuchumi.Na mashinani tunaelekea nchini Uganda kumsikia mkimbizi kutoka nchini Sudan Kusini.
Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Wed, 06 Mar 2024 - 11523 - Mtoto Charles: MONUSCO imenitoa msituni, asanteni sana
Harakati za ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO, za kuondoka nchini humo zikiendelea, tunamulika hatua chanya zilizochukuliwa na ujumbe huo katika kunusuru vijana waliokuwa wanatumikishwa na waasi mashariki mwa nchi hiyo.
Miongoni mwao ni Charles, mwenye umri wa miaka 16 ambaye si jina lake halisi. Yeye alitumikishwa msituni na waasi kwa kipindi cha miaka miwili.
Akizungumza huku sura yake ikiwa imefichwa kwenye video ya MONUSCO, Charles anakumbuka kuwa walikuwa shambani wanalima wakati waasi wa Mai Mai walipofika na kuwakamata.
“Walitueleza kuwa hawana watu wa kuwasaidia mapigano hivyo wakatuchukua. Tulipofika walituona kuwa tuna mawazo ya kutoroka hivyo walitufungia ndani kwa wiki tatu,” anasema Charles.
Anasema walipotoka fikra za kutoroka zikatoweka, wakafundishwa kupigana msituni na walipigana mara sita. Lakini haikuwa rahisi kwani wenzake 12 waliuawa huku porini wakati wa mapigano huku yeye mwenyewe akishuhudia.
“Niliumia sana. Chakula nacho kilikuwa shida kupata, maisha yalikuwa magumu mno. Nikafikiria nikaona bora nirejee kwa familia yangu.’
Walichofanya yeye na wenzake, usiku wa saa saba walitoroka hadi mji wa jirani ambako huko walijisalimisha kwa kiongozi mmoja na kumweleza kuwa wamechoka kuishi na kupigana porini.
Kiongozi huyo aliwachukua na kuwapeleka Beni, mji ulioko jimboni Kivu Kaskazini.
Charles anasema kiongozi huyo aliwasaidia kuwakutanisha na shirika la kiraia la ACOPE, mdau wa MONUSCO. Hapo walipata mafunzo kwa wiki tatu ikiwemo utengenezaji majiko banifu yasiyochafua mazingira.
“Sasa maisha ni mazuri hapa na wito wangu kwa wale watoto na vijana walioko msituni wakipigana ni kwamba waondoke huko waache kupigana, waje wajisalimishe kwa serikali ili waweze kujiendeleza.”
Wed, 06 Mar 2024 - 11522 - WFP/UNICEF: Janga kubwa la njaa duniani linanyemelea Sudan miezi 11 baada ya kuzuka vita
Takriban miezi 11 tangu majenerali wapinzani watangaze vita nchini Sudan, wahudumu wa kibinadamu wa Umoja wa Mataifa leo walionya kwamba mzozo huo unaweza kusababisha janga kubwa zaidi la njaa duniani.
Sudan, nchi iliyo kaskazini mashariki mwa Afrika tayari iko katika mzozo mkubwa zaidi wa watu waliofuriushwa makwao duniani kwa mujibu, Shirika la Mpango wa Chakula la Umoja wa Mataifa, WFP.
Na mapigano yanayoendelea kati ya Jeshi la Sudan SAF na kundi hasimu la msaada wa haraka RSF yamesababisha maelfu ya watu kupoteza maisha na wengine milioni nane kuyahama makazi yao ndani ya nchi na wengine kukimbilia nchi jirani.
Hivi sasa watoto milioni 14 wanahitaji haraka msaada wa kuokoa maisha, limesema Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF katika tahadhari yale ya hivi karibuni, huku kukiwa na wasiwasi kwamba mzozo huo unaweza kuenea kwenye mipaka ya Sudan, na kutishia maisha na amani katika eneo hilo, endapo mapigano hayo hayatokoma.
Cindy McCain, ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa WFP amesema "Miaka ishirini iliyopita, Darfur ilikuwa janga kubwa zaidi la njaa duniani na ulimwengu ulijitolea kuchukua hatua. Lakini leo hii watu wa Sudan wamesahaulika. Mamilioni ya maisha ya watu, amani na utulivu wa eneo zima viko hatarini,”
Bi. McCain ameyasema hayo akiwa Sudan Kusini, ambako amekutana na familia zilizokimbia ghasia na hali mbaya ya njaa Sudan na kuingia hiyo jirani zao.
Amesema hivi sasa WFP inahaha kutimiza mahitaji ya chakula na kuongeza kuwa "Nimekutana na kina mama na watoto ambao wamekimbia Sudan ili kuokoa maisha yao sio mara moja, lakini mara nyingi, na sasa njaa inawanyemelea. Madhara ya kutochukua hatua yanakwenda mbali zaidi ya mama kushindwa kulisha mtoto wake na yataathili eneo hilo kwa miaka mingi ijayo”.
WFP inasema leo hii chini ya mtu mmoja kati ya 20 Sudan ndiye anayeweza kumudu kupata chakula, watu 9 kati ya 10 wanakabiliwa na njaa na mgogoro wa chakula umesambaa hadi nchi jirani zinazohifadhi wakimbizi wa Sudan na kuathiri watu zaidi ya milioni 25 Sudan, Sudan Kusini, na Chad.
Wed, 06 Mar 2024 - 11521 - 05 MACHI 2024
- Baada ya kukosa vibali vya kuingia eneo la Gaza Kaskazini tangu katikati ya mwezi Januari mwaka huu, hatimaye shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO limefanikiwa kuingia eneo hilo na kujionea hali ya wananchi na mahitaji ya afya yalivyo pamoja na kupeleka misaada ikiwemo vifaa vya matibabu na mafuta ya kuendeshea mitambo ya hospitali.Huko Geneva Uswisi mkutano wa 55 wa Baraza La Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu umeendelea leo ambapo Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa kuhusu biashara na unyanyasaji wa kingono wa watoto Mama Fatima Singhateh ametaka kutambulika kwa hatua za mtu mmoja mmoja au za pamoja za kupambana na unyanyasaji wa kijinsia na unyonyaji wa watoto katika tasnia ya burudani na vyombo vya habari ili kukomeshwa unyanyasiji huo mara moja. Na tukiwa katika mwezi wa Machi unaoadhimisha siku ya wanawake duniani shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO limezitaka nchi kuhakikisha zinashughulikia changamoto za usawa wa kijinsia kwenye kupambana na madhara ya mabadiliko ya tabianchi kwani takwimu zinaonesha kuwa familia hususan za vijijini zinazoongozwa na wanawake zinaathirika zaidi na mabadiliko ya tabianchi ikilinganishwa na zile zinazoongozwa na wanaume.Na mashinani Jane Kamenya, Mama wa watoto wawili na mfyanyabiashara ya usukaji nywele kutoka kaunti ya Kajiado nchini Kenya ambaye kando na kupata manufaa na kuweza kujikwamua kiuchumi yeye anatoa wito kwa vijana na kinamama wajiunge naye katika jukumu muhimu ya wanawake la kuhakikisha jamii zao wameondokana na umaskini.
Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Tue, 05 Mar 2024 - 11520 - Mchango wa wanawake katika kulinda mazingira ni wa thamani sana: Dkt. Josephine Ojiambo
Katika kuelekea siku ya wanawake duniani ambayo itaadhimishwa Ijumaa wiki hii Machi 8 mchango wa wanawake katika kulinda na kuhifadhi mazingira umeelezwa kuwa ni mkubwa na wa thamani sana. Kandoni mwa mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Baraza la mazingira duniani UNEA6 uliofanyika Nairobi Kenya na kukunja jamvi mwishoni mwa wiki, nada mbalimbali zilijadiliwa ikiwemo mchango wa wanawake. Stella Vuzo afisa habari wa kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa Nairobi UNIS alizungumza na Balozi na mtafiti katika Mradi wa Green Transition nchini Kenya Dkt. Josephine Ojiambo kuzungumzia mchango huo wa wanawake katika kulinda mazingira.
Mon, 04 Mar 2024 - 11519 - UN inaonya kwamba vita ya Gaza yaweza kuchochea machafuko zaidi ya kikanda
Mazungumzo ya kusitisha mapigano Gaza yanaendelea nchini Misri kwa siku ya pili leo huku Kamishina Mkuu wa Haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa akionya kwamba vita ya Gaza iko katika hatari ya kubadili mweleko na kupanua wigo zaidi utakaoathiri kila nchi Mashariki ya Kati na kwingineko.
Asante Anold. Kamishina Mkuu Volker Türk ameliambia Baraza la Haki za Kibinadamu la Umoja wa Mataifa mjini Geneva Uswisi kuwa "Nina wasiwasi mkubwa kwamba katika janga hili la vita cheche yoyote zaidi inaweza kusababisha moto mkubwa zaidi,"
Katika taarifa ya hivi karibuni kuhusu migogoro ya kimataifa kwa Nchi 47 Wanachama wa Baraza hilo, Kamishna Mkuu alisisitiza kwamba jumuiya ya kimataifa inapaswa kufanya "kila linalowezekana ili kuepuka kuenea zaidi kwa vita ya Gaza.”
Maoni yake yanakuja huku kukiwa na wito wa "kusitishwa mara moja kwa mapigano kwa angalau wiki sita zijazo ili kuwezesha kuachiliwa huru kwa mateka wa Israeli.’
Wito huo umetoka kwa Makamu wa Rais wa Merika Kamala Harris, wakati wa mazungumzo ya kimataifa ya kusitisha mapigano nchini Misri Jumapili, ambayo yanayoripotiwa kuhusisha Marekani wajumbe wa Qatar na Hamas lakini hadi sasa hakuna wawakilishi wa Israel.
Bwana Türk amesema “Hatari za kuyumbisha usalama wa kikanda tayari zilionekana kusini mwa Lebanon, akisisitiza kwamba wapiganaji wa wanamgambo wanaoiunga mkono Palestina sasa wanahusika katika hali ya kusikitisha sana ya uhasama na majibizano ya risasi na Israeli, katika msitali wa Bluu wa uangalizi wa Umoja wa Mataifa unaotenganisha nchi zote mbili.
Takriban watu 200 wameuawa nchini Lebanon tangu vita ilipozuka Gaza¸ Kamishna Mkuu amesema miongoni mwa waathirika wakubwa ni, watoto, wahudumu wa afya na waandishi wa habari.
Mkuu huyo wa haki za binadamu ameongeza kuwa “takriban watu 90,000 nchini Lebanon wamekimbia makazi yao kutokana na ghasia hizo, huku kukiwa na uharibifu mkubwa wa vituo vya afya, shule na miundombinu muhimu. Jamii za Israeli pia zimeshuhudia watu 80,000 wakiondolewa kutoka maeneo ya mpakani kwa sababu ya kuongezeka kwa vurugu.”
Mashirika ya kibinadamu yameendelea kuripoti kuhusu hali mbayá na ongezeko la vifo vya raia ambapo lile la kuhudumia watoto UNICEF mwishoni mwa wiki likisema hadi sasa watoto 15 wamepoteza Maisha katika hospitali ya Kamal Adwan mjini Gaza kutokana na utapiamlo na ukosefu wa maji mwilini.
UNICEF imeonya kwamba watoto wengi zaidi watapoteza Maisha katika siku zijazo endapo msaada wa haraka unaohitajika hautofikishwa kunusuru Maisha yao.
Nalo shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wanawake UN Women linakadiria kuwa wanawake 9,000 wameshauawa tangu vita ilipozuka Gaza miezi mitano iliyopita.
Mamlaka ya afya ya Gaza inasema jumla ya watu waliopoteza Maisha tangu kuanza kwa vita Gaza ni zaidi ya 30,400 na inatarajiwa kuendelea kuongezeka.
Mon, 04 Mar 2024 - 11518 - 04 FEBRUARI 2024
- Mazungumzo ya kusitisha mapigano Gaza yanaendelea nchini Misri kwa siku ya pili leo huku Kamishina Mkuu wa Haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa akionya kwamba vita ya Gaza iko katika hatari ya kubadili mweleko na kupanua wigo zaidi utakaoathiri kila nchi Mashariki ya Kati na kwingineko..Nchini Sudan Kusini kwa mwaka jana pekee wateguaji wa mabomu ya ardhini wa Umoja wa Mataifa wamefanikiwa kusafisha eneo lenye ukubwa sawa na viwanja 64 vya mpira wa miguu, na hivyo kuondoa hatari nyingi za milipuko, inaeleza UNMISS ambao ni Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini. Makala tukielekea siku ya wanawake duniani ambayo itaadhimishwa Ijumaa wiki hii Machi nane leo tuko Nairobi Kenya kumulika mchango wa wanawake katika kukabiliana na changamoto ya mazingira. Kandoni mwa mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Baraza la mazingira duniani UNEA6 uliokunja jamvi mwishoni mwa wiki Stella Vuzo afisa habari wa kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa Nairobi UNIS alizungumza na Balozi na mtafiti katika Mradi wa Green Transition nchini Kenya Dkt. Josephine Ojiambo anayeanza kwa kueleza umuhimu wa wanawake katika kulinda mazingira.Na mashinani tutaelekea nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kumsikia mwanafunzi mmoja wa wanufaika wa programu ya (WFP) ya mlo shuleni.
Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Mon, 04 Mar 2024 - 11517 - UNMISS: Kuondoa mabomu ya ardhini Sudan Kusini eneo sawa na viwanja 64 vya soka limesafishwa
Nchini Sudan Kusini kwa mwaka jana pekee wateguaji wa mabomu ya ardhini wa Umoja wa Mataifa wamefanikiwa kusafisha eneo lenye ukubwa sawa na viwanja 64 vya mpira wa miguu, na hivyo kuondoa hatari nyingi za milipuko, inaeleza UNMISS ambao ni Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini.
Kupitia Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya misaada ya kutegua mabomu yaliyotegwa ardhini (UNMAS) asilimia 70 ya vilipuzi ambavyo vilikuwa havijalipuka sasa vimeharibiwa au kuondolewa katika maeneo vilimokuwa na hivyo kuwahakikishia watu makazi salama na maeneo ya kilimo.
Mike Fula Rashid, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kitaifa ya Sudan ya Hatua dhidi ya Vilipuzi (NMAA) anapeleka shukrani kwa Umoja wa Mataifa akisema,
"Tunashukuru kwa msaada ambao UNMAS inatupatia kuhusiana na uondoaji wa vilipuzi kwa sababu ukiangalia uwezo wa kuondoa mabomu nchini Sudan Kusini, asilimia 70 inaungwa mkono na UNMAS huku wafadhili wengine wakichangia asilimia 30 iliyobaki.”
Mon, 04 Mar 2024 - 11516 - Mtu 1 kati ya 4 anaishi na utipwatipwa duniani
Utafiti mpya uliotolewa leo na jarida la kitabibu la Uingereza Lancet na shirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani WHO unaonyesha kwamba, mwaka 2022, zaidi ya watu bilioni 1 duniani sasa wanaishi na unene wa kupindukia ama utipwa tipwa. Duniani kote, unene wa kupindukia kwa watu wazima umeongezeka zaidi ya mara mbili tangu mwaka 1990, na umepanda mara nne kwa watoto na vijana wenye umri wa miaka 5 hadi 19.
Utafiti huo pia unaonyesha kwamba ingawa viwango vya utapiamlo vimepungua, bado ni changamoto kubwa ya afya ya umma katika maeneo mengi, hasa Asia Kusini Mashariki na Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Nchi zenye viwango vya juu zaidi vya utipwatipwa na utapiamlo mwaka 2022 zilikuwa ni mataifa ya visiwa katika Pasifiki na Karibea, Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini.
Mkuu wa WHO Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema utafiti huu mpya unaangazia umuhimu wa kuzuia na kudhibiti unene wa kupindukia tangu utotoni hadi utu uzima kupitia lishe, mazoezi ya mwili, na huduma za kutosha kadri inavyohitajika.
Ghebreyesus ameongeza kuwa ili kupambana na tatizo hilo ni sharti kurejea kwenye mstari ili kufikia malengo ya kimataifa ya kudhibiti unene wa kupindukia itahitaji kazi ya serikali na jamii, ikisaidiwa na sera za WHO na mashirika ya afya ya umma ya kitaifa na sekta binafsi.
Kwa mujibu wa WHO, utapiamlo, katika aina zake zote, ni pamoja na kukonda, kudumaa, uzito mdogo, upungufu wa vitamini au madini, uzito kupita kiasi na unene kupita kiasi, hata hivyo ukosefu wa lishe bora huchangia nusu ya vifo vya watoto chini ya miaka 5 na unene unaweza kusababisha magonjwa yasiyoambukiza kama vile magonjwa ya moyo na mishipa, kisukari na baadhi ya saratani.
Katika Mkutano wa Afya Duniani mwaka 2022, Mataifa Wanachama walikubaliana na Mpango wa WHO wa Kuongeza kasi ya Kusitisha Unene wa Kupindukia, unaounga mkono hatua za ngazi ya nchi hadi 2030. Hadi sasa, serikali 31 zinaongoza njia kudhibiti janga la unene wa kupindukia kwa kutekeleza mpango huo.
Mkurugenzi wa Idara ya Lishe na Usalama wa Chakula wa WHO na mmoja wa waandishi wa utafiti huo Dkt. Francesco Branca amesema kuna changamoto kubwa katika utekelezaji wa sera zinazolenga kuhakikisha upatikanaji wa chakula bora kwa wote na kujenga mazingira ambayo yanakuza shughuli za kimwili na maisha ya afya kwa ujumla kwa kila mtu na kutoa wito kwa nchi kuweka mfumo wa kuzuia na kudhibiti utapwitapwi katika huduma za msingi
Utafiti huo umeweka bayana kwamba ili kukabiliana na utapiamlo kunahitajika hatua za kisekta mbalimbali katika kilimo, ulinzi wa jamii na afya, ili kupunguza uhaba wa chakula, kuboresha upatikanaji wa maji safi na usafi wa mazingira na kuhakikisha upatikanaji wa afua muhimu za lishe kwa wote.
Fri, 01 Mar 2024
Podcasts similar to Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu
- Global News Podcast BBC World Service
- El Partidazo de COPE COPE
- Herrera en COPE COPE
- The Dan Bongino Show Cumulus Podcast Network | Dan Bongino
- Es la Mañana de Federico esRadio
- La Noche de Dieter esRadio
- Hondelatte Raconte - Christophe Hondelatte Europe 1
- Dateline NBC NBC News
- 財經一路發 News98
- La rosa de los vientos OndaCero
- Más de uno OndaCero
- La Zanzara Radio 24
- L'Heure Du Crime RTL
- El Larguero SER Podcast
- Nadie Sabe Nada SER Podcast
- SER Historia SER Podcast
- Todo Concostrina SER Podcast
- 安住紳一郎の日曜天国 TBS RADIO
- TED Talks Daily TED
- アンガールズのジャンピン[オールナイトニッポンPODCAST] ニッポン放送
- 辛坊治郎 ズーム そこまで言うか! ニッポン放送
- 飯田浩司のOK! Cozy up! Podcast ニッポン放送
- 吳淡如人生實用商學院 吳淡如
- 武田鉄矢・今朝の三枚おろし 文化放送PodcastQR