Podcasts by Category

SIRI ZA BIBLIA

SIRI ZA BIBLIA

SIRI ZA BIBLIA

Maarifa ya ki-Mungu na namna ya kuliishi kusudi lako

119 - ZABURI 1
0:00 / 0:00
1x
  • 119 - ZABURI 1

    Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.
    2Bali sheria ya Bwana ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.
    3Naye atakuwa kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa.
    4Sivyo walivyo wasio haki; Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
    5Kwa hiyo wasio haki hawatasimama hukumuni, Wala wakosaji katika kusanyiko la wenye haki.
    6Kwa kuwa Bwana anaijua njia ya wenye haki, Bali njia ya wasio haki itapotea.

    --- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/siri-za-biblia/message
    Mon, 17 Jan 2022 - 01min
  • 118 - FAIDA TANO ZA MAOMBI YA KUFUNGA: SIRI ZA BIBLIA


    1. Maombi ya kufunga yanaweza kukufanya uongezeke kiimani.
    Mathayo 17:21 ‘’ [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.] ‘’

    2. Macho yako ya ndani yatakuwa yanaona vizuri.

    Zaburi 119:18 ‘’ Unifumbue macho yangu niyatazame Maajabu yatokayo katika sheria yako. ‘’

    . 3. Mwili wako utakuwa umetiishwa.
    Wakolosai 3:5 ‘’ Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu;‘’

    4. Kupokea maana ni ahadi ya MUNGU kujibu maombi yako.

    Yeremia 29:13 ‘’Nanyi mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.'' Tena Biblia inasema ''Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa;-Mathayo 7:7'' na kwa sababu MUNGU analiangalia neno lake alitimize basi hata aliposema tuombe ni hakika atajibu maana yeye hajipingi na Neno lake, labda tu sisi tuombe vibaya na tupungukiwe na imani katika maombi yetu.

    5. Utamruhusu ROHO MTAKATIFU kukutumia.

    1 Kor 12:11 ‘’ lakini kazi hizi zote huzitenda ROHO huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye. ‘’

    --- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/siri-za-biblia/message
    Sun, 24 Oct 2021 - 02min
  • 117 - USHINDE UBAYA KWA WEMA: SIRI ZA BIBLIA

    Maisha Mapya Katika Kristo

    1 Kwa hiyo, ndugu zangu, nawasihi kwa rehema zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu na inayompendeza Mungu, hii ndiyo ibada yenu yenye maana. 2Msifuatishe tena mfano wa ulimwengu huu, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu. Ndipo mtaweza kuonja na kuhakikisha ni nini mapenzi ya Mungu yaliyo mema, yanayopendeza machoni pake na ukamilifu.

    3 Kwa ajili ya neema niliyopewa nawaambia kila mmoja miongoni mwenu, asijidhanie kuwa bora kuliko impasavyo, bali afikiri kwa busara kwa kulingana na kipimo cha imani Mungu aliyompa. 4Kama vile katika mwili mmoja tulivyo na viungo vingi, navyo viungo vyote havina kazi moja, 5vivyo hivyo na sisi tulio wengi, tu mwili mmoja katika Kristo, nasi kila mmoja ni kiungo cha mwenzake. 6Tuna karama zilizotofautiana kila mmoja kutokana na neema tuliyopewa. Kama ni unabii na tutoe unabii kwa kadiri ya imani. 7Kama ni kuhudumu na tuhudumu, mwenye kufundisha na afundishe, 8kama ni kutia moyo na atie moyo, kama ni kuchangia kwa ajili ya mahitaji ya wengine na atoe kwa ukarimu, kama ni uongozi na aongoze kwa bidii, kama ni kuhurumia wengine na afanye hivyo kwa furaha.

    Alama Za Mkristo Wa Kweli

    9 Upendo lazima usiwe na unafiki. Chukieni lililo ovu, shikamaneni na lililo jema. 10Pendaneni ninyi kwa ninyi kwa upendo wa ndugu. Waheshimuni na kuwatanguliza wengine. 11Msiwe wavivu, bali mwe na bidii katika roho mkimtumikia Bwana. 12Kuweni na furaha katika tumaini, katika dhiki kuweni na saburi, dumuni katika maombi. 13Changieni katika mahitaji ya watakatifu, wakaribisheni wageni.

    14Wabarikini wale wanaowatesa, barikini wala msilaani. 15Furahini pamoja na wenye kufurahi, lieni pamoja na wale waliao. 16Kaeni kwa amani ninyi kwa ninyi. Msijivune, bali mwe tayari kushirikiana na wanyonge. Wala msiwe watu wenye kujivuna kwamba mnajua kila kitu.

    17 Msimlipe mtu yeyote ovu kwa ovu. Jitahidini ili mtende yaliyo mema machoni pa watu wote. 18Kama ikiwezekana, kwa upande wenu kaeni kwa amani na watu wote. 19Wapendwa, msilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu, maana imeandikwa: “Ni juu yangu kulipiza kisasi, nitalipiza,” asema Bwana. 20Badala yake:

    “Kama adui yako ana njaa, mlishe;

    kama ana kiu, mpe kinywaji.

    Kwa kufanya hivyo,

    unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake.”

    21Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema.

    --- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/siri-za-biblia/message
    Sat, 23 Oct 2021 - 03min
  • 116 - ZIITE BARAKA ZAKO KWA MAOMBI HAYA: SIRI ZA BIBLIA

    1 Kor 16:9 

    kwa maana nimefunguliwa mlango mkubwa wa kufaa sana, na wako wengi wanipingao.

    --- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/siri-za-biblia/message
    Fri, 22 Oct 2021 - 05min
  • 115 - SIRI ZA BIBLIA: USIOGOPE,NIKO PAMOJA NAWE NIKUOKOE

    Mistari mbalimbali ambayo Mungu amezungumza nasi katika maandiko kwenye Biblia,kuhusu kutokuogopa "USIOGOPE"

    --- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/siri-za-biblia/message
    Tue, 21 Sep 2021 - 13min
Show More Episodes