Filtrar por gênero

Radio Maria Tanzania

Radio Maria Tanzania

Radio Maria Tanzania

Haraka sana ilienea kote Italia, tayari katika miaka ya 90, uzoefu huu wa kipekee wa redio uliamsha shauku katika sehemu zingine za ulimwengu. Baadaye, kila mara chini ya uelekezi na usaidizi wa Radio Maria Italia, Radio Maria nyingine iliibuka Amerika (kuanzia na Peru), Afrika (kwanza Burkina Faso), sehemu nyingine za Ulaya… na hivyo Familia ya Ulimwengu ya Radio Maria ilizaliwa mnamo Juni 1998, na kuwa NGO inayotambuliwa na UN, yenye makao makuu ya kisheria huko Roma. Madhumuni yake ni kuendeleza mradi wa kimisionari, kujibu maombi yanayotoka katika maeneo yote ya dunia, kuhakikisha uhalisi wa chapa, kutoa usaidizi wa kiufundi kwa RM zote, na kukuza mabadilishano na usaidizi kati ya kila redio. Familia ya Ulimwengu inadumisha mahusiano ya mara kwa mara ya taarifa na Baraza la Kipapa la Mawasiliano ya Kijamii la Kiti Kitakatifu

499 - Fahamu uhusiano wa utandawazi na wito wako.
0:00 / 0:00
1x
  • 499 - Fahamu uhusiano wa utandawazi na wito wako.

    Karibu ungane na Martin Joseph katika kipindi cha Fahamu Wito Wako, Muwezeshaji ni Padre Innocent Bahati Mushi, kutoka Chuo Kikuu cha Nelson Mandela, Jimbo Kuu la Arusha, mada anayozungumzia ni mambo ya utandawazi.

    Fri, 03 May 2024 - 47min
  • 498 - Amka na Mama Pasaka [Sehemu ya kumi na mbili]
    Fri, 03 May 2024 - 50min
  • 497 - Je, Mei mosi ni sikukuu ya Kikanisa au ya Kiserikali?

    Karibu katika kipindi cha Maswali Yahusuyo Imani, kutoka seminari Kuu ya Mtakatifu Augustino Peramiho, Jimbo Kuu la Songea, na Frateri Jackob Venusto Mkandawile anajibu swali lililoulizwa je, Mei mosi ni sikukuu ya Kikanisa au ya Kiserikali, na kwanini Mtakatifu Yosefu aliwekwa msimamizi wa Wafanyakazi?

    Fri, 03 May 2024 - 29min
  • 496 - Fahamu Historia ya Rozari Takatifu.

    Karibu katika kipindi cha Maswali yahusuyo Imani na Frateri  Ayubu Polykap Mwashibili, kutoka Parokia ya Mtakatifu Yohane Mbatizaji Jimbo kuu la Mbeya  Swali la Msikilizaji linalojibiwa linasema Rozari Takatifu ni nini? na naomba nijue na Historia yake

    Fri, 03 May 2024 - 55min
  • 495 - Fahamu maana ya Mirathi na faida zake.

    Karibu uungane na Mtangazaji Elizabeth Masanja katika Kipindi cha Ijue Sheria, Mwezeshaji ni Mheshimiwa Hassan Mlanga, Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo  Bomani Iringa Mjini, Mada tunayojifunza siku ya leo ni maana ya Mirathi, faida yake na mchakato wa ufuatiliaji.

    Fri, 03 May 2024 - 50min
Mostrar mais episódios