Podcasts by Category
Fahamu masuala kadha wa kadha kuhusu uchumi kama vile, namna ya kupambana na umaskini, mfumuko wa bei, kushamiri kwa matumizi ya dola na athari za kuyumba kwa uchumi wa dunia kwa nchi za Afrika. Mada hizi zinafanyiwa utafiti wa kina na zinazungumzwa kwa lugha rahisi inayoeleweka ili kukufanya uelewe na usichoke kusikiliza .
- 224 - Wataalamu: Uchumi Samawati utumiwe vizuri kwa maendeleo endelevu
Kulingana na Benki ya Maendeleo ya Afrika, uchumi wa bluu barani Afrika una uwezo wa kuchangia pakubwa katika ukuaji wa uchumi na maendeleo ya bara hilo.
Uchumi wa bluu unatajwa kuchangia dola za Marekani trilioni 1 kila mwaka, Sekta ya uvuvi ikiwa kitovu kikuu na kuajiri zaidi ya watu milioni 12.
Profesa Omary Mbura, mtaalamu na mhadhiri wa masuala ya uchumi kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam, anaangazia sekta hii.
Thu, 11 Apr 2024 - 223 - Umuhimu wa ushirikiano kati ya sekta binafsi na uma
Shughuli za sekta binafsi na uwekezaji ni vyanzo vikuu ya ukuaji wa uchumi, uzalishaji wa ajira na maendeleo endelevu.
Kwa wastani, sekta binafsi inachangia zaidi ya Asilimia 80 ya mapato ya serikali kwa watu wa kipato cha chini na cha kati, kupitia kodi ya kampuni, kodi ya rasilimali na mapato ya kodi kwa wafanyakazi.
Sekta hii inazalisha zaidi ya asilimia 90 ya ajira katika nchi zinazoendelea kiuchumi.
Mon, 04 Mar 2024 - 222 - Ukulima wa matunda Kenya na changamoto zakeMon, 04 Mar 2024
- 221 - Changamoto za uhamiaji na fursa zake kwa uchumi
Uhamiaji unaweza kuwa nguzo muhimu kwa maendeleo ya uchumi wa Afrika ikiwa mtu anaweza kutoa mwelekeo bora wa fedha zinazotumwa na wageni kuelekea uwekezaji na ufadhili wa maendeleo katika nchi za Afrika.
Diasporas wanachangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii ya nchi zetu ambazo kimsingi ni nchi za asili lakini pia nchi mwenyeji.
Wanafanya hivyo kwa kuhamisha pesa, ujuzi, teknolojia, mifano ya utawala, maadili, na mawazo. Serikali ya Senegal inafahamu mabadiliko yanayohitajika tunapojitahidi kutekeleza Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) na Mkataba wa Kimataifa wa Uhamiaji Salama, Ulio na Utaratibu na wa Kawaida nchini Senegali.
Mon, 04 Mar 2024 - 220 - Kuberoshwa kwa huduma ya intaneti Kenya na ilivyochochea ubunifuMon, 04 Mar 2024
- 219 - Mzozo kati ya Kenya na Tanzania kuhusu mashirika yake ya ndege
Msikilizaji, hatimaye nchi ya Tanzania imeondoa zuio ililoweka juma hili kwa ndege za shirika la Kenya KQ, uamuzi iliyokuwa imeuchukua baada ya Nairobi kukataa kutoa kibali kwa ndege za mizigo za shirika la Tanzania kushusha na kupakia kutokea Kenya.
Uamuzi huo msikilizaji ulisababisha mawaziri wa pande zote kukutana na Jumanne ya wiki hii wakakubaliana kumaliza tofauti zilizojitokeza na sasa safarai za ndege za Kenya na zile za Tanzania zitaruhusiwa.
Mon, 04 Mar 2024 - 218 - Mustakabali wa Jumuiya mwaka 2024
Makala ya Gurudumu la uchumi juma hili inaangazia mustakabali wa jumuiya ya Afrika Mashariki kiuchumi kwa mwaka 2024, hasa baada ya athari za uviko 19 za tangu mwaka 2020 na sasa mdororo wa uchumi wa dunia, ambao umesababisha mataifa masikini, ikiwemo ya ukanda kushuhudia kupanda kwa gharama ya maisha.
Nimezungumza na Johnson Denge, mchambuzi wa masuala ya uchumi akiwa nchini Kenya.
Mon, 04 Mar 2024 - 217 - Matarajio ya Wafanyabiashara kwa mwaka 2024
Makala ya Gurudumu la Uchumi juma hili, inaangazia namna wafanyabiashara wamejipanga katika mwaka 2024, kuhakikisha biashara zao zinashamiri licha ya changamoto za kiuchumi zinazoikabili dunia kwa sasa.
Mwandishi wetuj Victor Moturi, kwa niaba ya mtayarishaji wa makala haya, Emmanuel Makundi, amezungumza na wafanyabiashara nchini Kenya, ambao mwaka uliopita, walilalama kupata changamoto za kifedha na hata upandaji wa bidhaa na kukosekana kwa dola.
Mon, 04 Mar 2024 - 216 - Matarajio ya Jumuiya ya Afrika Mashariki 2024
Makala ya Gurudumu la uchumi juma hili inaangazia mustakabali wa jumuiya ya Afrika Mashariki kiuchumi kwa mwaka 2024, hasa baada ya athari za uviko 19 za tangu mwaka 2020 na sasa mdororo wa uchumi wa dunia, ambao umesababisha mataifa masikini, ikiwemo ya ukanda kushuhudia kupanda kwa gharama ya maisha.
Nimezungumza na Johnson Denge, mchambuzi wa masuala ya uchumi akiwa nchini Kenya.
Thu, 11 Jan 2024 - 215 - Mkutano wa China na Afrika pamoja na ziara za viongozi nchi za Magharibi barani Afrika
Makala ya Gurudumu la Uchumi juma hili inaangazia mkutano wa nchi ya Uchina na viongozi wa Afrika uliofanyika wiki kadhaa zilizopita, pamoja na ziara za viongozi wa nchi za Marekani, Uingereza na Ujermani kwenye nchi za Afrika Mashariki na Magharibi.
Ziara zao zinaashiria nini katika muktadha wa kiuchumi? Emmanuel Makundi amezungumza na Profesa Wetengere Kitojo, kuangazia haya kwa kina.
Thu, 02 Nov 2023 - 214 - Kwanini Bostwana imefanikiwa kwenye sekta ya madini ?
Kwenye sehemu yetu ya pili na ya mwisho kuhusu namna nchi ya Bostwana ilivyopiga hatua kwenye sekta ya madini na uchumi wake kwa kutegemea Almasi, tutasikia kutoka kwa wadau mbalimbali akiwemo mwekezaji binafsi Siddarth Gothi , Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo KGK Bostwana, na mchambuzi binafsi wa siasa, Marisa Lourenco, kutoka Afrika Kusini kuhusu mafanikio hayo lakini pia changamoto katika sekta hiyo.
Wed, 25 Oct 2023 - 213 - Fursa za uwekezaji nchini Bostwana kwa nchi za Afrika Mashariki
Kati ya Oktoba 11 hadi 14 mwezi Oktoba, Bostwana iliandaa maonesho ya Kimataifa ya kibiashara jijini Gaborone, yaliyofanyika pembezoni mwa Jukwaa la kwanza wa kibiashara kati ya nchi hiyo na Umoja wa Ulaya.
Bostwana ambayo uchumi wake mkubwa unategemea sekta ya madini, hasa Almasi ikiwa ya pili duniani kwa bidhaa hiyo baada ya Urusi, ilitumia fursa hiyo kujitangaza na kuvutia wawekezaji zaidi.
Nchi hiyo ya Kusini mwa Afrika ambayo inataka kuwa nchi ya kipato cha juu kufikia 2036 kwa kupanua uchumi wake kwenye sekta nyingine kama kilimo na utalii, ni miongoni mwa mataifa duniani, ambayo taasisi za Kimataifa kama IMF na Benki ya dunia, zinasema uchumi wake unakuwa kwa kasi.
Je, Bostwana ina fursa zipi za uwekezaji hasa kwa mataifa ya Afrika Mashariki ? Wakati wa maonesho hayo, nilitembelea banda la Kenya, na leo kwenye Makala yetu ya Gurudumu la Uchumi, utamsikia Balozi wa Kenya nchini Bostwana.
Fri, 20 Oct 2023 - 212 - IMF, benki ya dunia zaonya kuhusu kudorora kwa uchumi wa mataifa ya Afrika
Ukuaji wa uchumi wa nchi za Afrika zilizoko Kusini mwa Jangwa la Sahara, unatarajiwa kupungua kasi mwaka huu, kutokana na kudorora kwa uchumi wa mataifa ya Afrika Kusini, Nigeria na Angola, hii ni kwa mujibu wa ripoti ya Benki ya Dunia.
Ukuaji wa kikanda utapungua hadi 2.5% mwaka 2023 kutoka 3.6% mwaka jana, imesema ripoti hiyo.
Mtayarishaji amezungumza na Johnson Denge, mtaalamu na mchambuzi wa masuala ya uchumi, kuangazia ripoti hizi kwa kina.
Aidha kwa mujibu wa IMF Uchumi wa dunia unakua lakini sio kwa kasi, ambapo inakadiria kuwa ukuaji wa uchumi wa dunia utapungua kutoka asilimia 3.5 mwaka 2022 hadi asilimia 3 mwaka huu na asilimia 2.9 mwaka ujao.
IMF inasema Mfumuko wa bei ambao haujumuishi bei ya chakula na nishati pia unatarajiwa kupungua, ingawa polepole zaidi. Nchi nyingi zikitajwa kutokuwa na uwezekano wa kurudisha mfumuko wa bei hadi 2025.
Wed, 11 Oct 2023 - 211 - Viongozi wa dunia wajadili malengo endelevu ya umoja wa Mataifa
Mwezi uliopita, viongozi wa dunia walikutana jijini New York, Marekani katika mkutano wa 78 wa baraza la umoja wa Mataifa, ambapo walijadiliana masuala mbalimbali ikiwemo usalama wa dunia na ukuaji wa uchumi pamoja na mikakati ya kufikia ajenda ya mwaka 2030 na haja ya kuongeza kasi kutekeleza malengo 17 endelevu.
Kuzungumzia yaliyojiri, mtayarishaji wa makala haya alimualika Ebenezer Suleiman Mathew Ikomba, balozi wa vijana wa Tanzania kwenye umoja wa Mataifa.
Katika mijadala mingi, vijana walitajwa kuwa sehemu kubwa ya nguvu kazi ya dunia na kwamba kupitia ubunifu, uwajibikaji na harakati za kuhamasisha nchi kufikia malengo endelevu, basi dunia itakuwa sehemu salama.
Makala ya Gurudumu la uchumi juma hili inaangazia yaliyotokana kwenye mkutano huo na namna gani vijana wanaweza kushiriki katika ujenzi wa dunia salama na yenye amani ambayo itachochea maendeleo na ukuaji wa uchumi.
Thu, 05 Oct 2023 - 210 - Tatizo la uhaba wa dola ya Marekani kwenye nchi za Afrika MasharikiFri, 22 Sep 2023
- 209 - Biashara ya madini yaimarika nchini DRC
Wiki hii tunaangazia huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambako kunaripotiwa ongezeko kubwa la uzalishaji wa madini ya shaba na kobalt katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. Takwimu kutoka sekta ya madini, zinaonesha kuwa uzalishaji wa kobalt imeongezeka na kufikia zaidi ya Tani Laki moja, baada ya serikali kuwekeza asilimia 43 ya bajeti yake ya taifa kwenye sekta hiyo.
Kwenye Makala haya, mwandishi wetu wa Lubumbashi Denise Maheho, amezungumza na watafiti wa madini na mashirika ya kiraia, katika eneo la Katanga.
Thu, 07 Sep 2023 - 208 - Nguo za mitumba zapigwa marufuku nchini UgandaFri, 01 Sep 2023
- 207 - MABADILIKO YA TABIA NCHI KWA UCHUMI
Athari za mabadiliko ya tabia nchi kuanzia mafuriko na ukame zimesababisha mamilioni ya raia kupoteza makazi yao, wengi wakitumbukia katika hali ya umasikini na hata kufa njaa, baadhi wakikosa huduma muhimlu ya afya, elimu huku tofauti kati ya walionacho na wasionacho ikiendelea kuongezeka, uchumi wa mataifa ukidorora.
Kwa mujibu wau moja wa Mataifa mpaka kufikia mwaka 2030 watu wanaokadiriwa kufikia milioni 700 huenda wakawa wakuhamahama kutokana na ukame peke yake.
Kuchukua hatua stahiki kukabili mabadiliko ya tabia nchi na athari zake ni jambo lisilohitaji mjadala wa muda mrefu ili kunusuru maisha ya raia pamoja na kufikia malengo endelevu ya umoja wa Mataifa.
Haya yanajiri wakati huu joto likiendelea kuongezeka, nchi zikitumia fedha nyingi kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi badala ya kuwa zingeelekezwa katika kutatua changamoto za maendeleo na kiuchumi hasa kwenye nchi masikini.
Makala ya Gurudumu la uchumi juma hili, inaangazia ni namna gani nchi zinazoendelea zinaweza kukabiliana na athari za hali ya hewa na wakati huohuo kuwaletea wananchi maendeleo
Thu, 10 Aug 2023 - 206 - Je Afrika inawezaje kutumia raslimali watu kwa maendeleo ya uchumi?
Takwimu zinaonyesha kuwa rasilimali watu katika nchi za kusini mwa jangwa la Sahara, ilikuwa ndogo mno ikilinganishwa na mataifa mengine ya dunia, ambapo Uviko 19 na vita vya Urusi nchini Ukraine vilichangia.
Wiki hii Emmanuel Makundi anaangazia wito wa wakuu wa nchi za ukanda ili kuangalia namna bora zaidi ya kutumia nguvu kazi iliyoko barani Afrika kwa maendeleo.
Wed, 02 Aug 2023 - 205 - DRC: Kushuka kwa thamani ya fedha na changamoto la wakimbizi wa ndani
Wimbi la wakimbizi wa ndani pamoja nakushuka kwa thamani ya pesa za kongo dhidi ya dola za Marekani kumesababisha kupanda kwa gharama za maisha katika miji kadhaa nchini jamuhuri yakidemokrasia ya Kongo.
Makal aya Gurudumu la uchumi juma hili inaangazia kwa kina hali hii na mtayarishaji Emmanuel Makundi, ameshirikiana na mwandishi wa Goma Benjamini Kasembe pamoja na kuzungumza na mtaalamu wa uchumi kutoka Bukavu Bengeya Machozi.
Wed, 26 Jul 2023 - 204 - Ujuzi kwa vijana na teknolojia
Makala ya Gurudumu la uchumi juma hili, inaangazia siku ya "ujuzi kwa vijana duniani' inayoadhimishwa kila tarehe 15 ya mwezi Julai kila mwaka, lengo ni kuwawezesha walimu, wakufunzi na vijana kutumia ujuzi wao kwa maendeleo.
Leo mtayarishaji amezungumza na Tukupala Mwalyolo, msichana anayeunda ndege zisizo na rubani 'drone', pamoja na Emmanuel Cosmas Msoka, kijana mbunifu wote wakitumia teknolojia kutafuta suluhu na wako Tanzania.
Wed, 12 Jul 2023 - 203 - Faida ya mfumo wa malipo ya pamoja barani Afrika
Mwezi Januari mwaka 2022, benki kuu pamoja na wakuu wa nchi za umoja wa Afrika, waliunga mkono mchakato ulioanzishwa na benki ya Afrexim, ambayo ilitengeneza mfumo wa malipo uliolenga kurahisisha ufanyaji wa malipo na manunuzi kati ya nchi na nchi, mtu na mtu na biashara kwa biashara barani Afrika.
Mfumo huu unafahamika kama Pan-African payments and Settlement System PAPSS, kwa kiasi kikubwa unapunguza changamoto ya ufanyaji malipo kwa kutumia fedha za kigeni kama Dola, ambapo kupitia mfumo huu nchi, biashara au watu wanaweza kubadilishana huduma kwa kutumia fedha ya nchi husika.
Lakini je, ni kwanini bado mfumo huu hauonekani kutoa jibu kwa tatizo lililoko hasa linapokuja suala la malipo au ununuzi wa biadhaa ambapo nchi zinalazimika kutumia dola ?
Mbali na hili tutaangazia pia ikiwa uongezaji wa tozo na kodi ndio suluhu kwa nchi nchi za Afrika kukabikliana na changamloto za kifedha na kiuchumi.
Makala ya Gurudumu la uchumi juma hili, inaenda kuangazia masuala haya kwa kina.
Wed, 31 May 2023 - 202 - Changamoto za kilimo na suluhu endelevu kwa bara AfrikaTue, 30 May 2023
- 201 - Umuhimu wa bara la Afrika kuwa na mfumo wa pamoja wa kufanya malipo kidijiti
Kwa mujibu wa umoja wa Mataifa, malipo ya kidijiti au ya kimtandao yanachangia pakubwa katika kujenga msingi imara wa kufikia maendeleo endelevu, kwanini? Ni kwasababu malipo haya yanapokuwa rahisi, salama, ya wazi na binafsi, yatawezesha ukuaji wa fursa kama nishati, maji na mikopo.
Katika kipindi hiki utamsikia, Lucy Nshuti Mbabazi, kutoka taasisi ya umoja wa Mataifa ya muungano wa Better than Cash, Lacina Kone, mkurugenzi wa Smartafrica pamoja na Kwizela Aristide Basebya, mtafiti wa Teknolojia za Mawasiliano ya Umma na Matumizi yake serikalini, akiwa Beijing, China.
Wed, 17 May 2023
Podcasts similar to Gurudumu la Uchumi
- Global News Podcast BBC World Service
- El Partidazo de COPE COPE
- Herrera en COPE COPE
- The Dan Bongino Show Cumulus Podcast Network | Dan Bongino
- Es la Mañana de Federico esRadio
- La Noche de Dieter esRadio
- Hondelatte Raconte - Christophe Hondelatte Europe 1
- Curiosidades de la Historia National Geographic National Geographic España
- Dateline NBC NBC News
- 財經一路發 News98
- La rosa de los vientos OndaCero
- Más de uno OndaCero
- La Zanzara Radio 24
- L'Heure Du Crime RTL
- El Larguero SER Podcast
- Nadie Sabe Nada SER Podcast
- SER Historia SER Podcast
- Todo Concostrina SER Podcast
- 安住紳一郎の日曜天国 TBS RADIO
- アンガールズのジャンピン[オールナイトニッポンPODCAST] ニッポン放送
- 辛坊治郎 ズーム そこまで言うか! ニッポン放送
- 飯田浩司のOK! Cozy up! Podcast ニッポン放送
- 吳淡如人生實用商學院 吳淡如
- 武田鉄矢・今朝の三枚おろし 文化放送PodcastQR
Other Business Podcasts
- Tanguy Pastureau maltraite l'info France Inter
- Les experts BFM Business
- BFM Bourse BFM Business
- C'est votre argent BFM Business
- Tout pour investir BFM Business
- Forward Leadership George Moustakelis
- Une Vie de Liberté Une Vie de Liberté
- Midnight Zen Wilton Ng
- Radio Bichon Le podcast des passionnés du bâtiment
- On n'arrête pas l'éco France Inter
- SMART BOURSE SMART BOURSE
- Good Morning Business BFM Business
- Classic Pedro Melo Menezes
- Afrique économie RFI
- 2050 Investors (en français) Société Générale
- Grands Leaders, les leçons de l'Histoire Radio Classique
- La Martingale Matthieu Stefani | Orso Media
- Ni Buenas Ni Malas Ni Buenas Ni Malas Podcast
- Oriana🌎Analiza Oriana Farías
- Economie & Finance Max Labadie